Kwa wataalamu wa siasa za kimataifa mtusaidie

Kwa wataalamu wa siasa za kimataifa mtusaidie

passion_amo1

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2023
Posts
1,828
Reaction score
3,922
Wakuu Heshima mbele.

Marekani imewawekea vikwazo maafisa watano wa Uganda, akiwemo Spika wa Bunge la nchi hiyo, Anita Among, mumewe na Naibu Mkuu wa zamani wa Majeshi ya Ulinzi kutoingia nchini humo kwa tuhuma za ufisadi na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.

Katika taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, imesema kuwa Spika Among amewekewa vikwazo kutokana na kuhusika kwake katika ufisadi mkubwa unaohusishwa na uongozi wake wa kibunge, huku Naibu mkuu wa zamani wa jeshi la Uganda, Luteni Jenerali Peter Elwelu akiwekewa vikwazo kutokana na ‘mauaji ya kiholela’ yaliyofanywa na wanajeshi wa nchi hiyo.

Mwenye ufahamu vikwazo hivi vina athiri vipi mtu binafsi?

SOURCE: SWAHILI TIMES

72363216-5061-4E14-ACBE-1317F6DA8F63.jpeg
 
Hakuna hathari zozote zitakazo wapata hao jamaa kama hawata safiri kwenda marekani,kama unatulia zako nchini kwako poa tu.
 
Wakuu Heshima mbele.

Marekani imewawekea vikwazo maafisa watano wa Uganda, akiwemo Spika wa Bunge la nchi hiyo, Anita Among, mumewe na Naibu Mkuu wa zamani wa Majeshi ya Ulinzi kutoingia nchini humo kwa tuhuma za ufisadi na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.

Katika taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, imesema kuwa Spika Among amewekewa vikwazo kutokana na kuhusika kwake katika ufisadi mkubwa unaohusishwa na uongozi wake wa kibunge, huku Naibu mkuu wa zamani wa jeshi la Uganda, Luteni Jenerali Peter Elwelu akiwekewa vikwazo kutokana na ‘mauaji ya kiholela’ yaliyofanywa na wanajeshi wa nchi hiyo.

Mwenye ufahamu vikwazo hivi vina athiri vipi mtu binafsi?

SOURCE: SWAHILI TIMES

View attachment 3004733
Ili kuleta usawa, Uganda nayo itafute maafisa watano wa Marekani iwawekee vikwazo vya kutoingia Uganda.

Dawa ya moto ni moto!
 
Back
Top Bottom