passion_amo1
JF-Expert Member
- Dec 3, 2023
- 1,828
- 3,922
Wakuu Heshima mbele.
Marekani imewawekea vikwazo maafisa watano wa Uganda, akiwemo Spika wa Bunge la nchi hiyo, Anita Among, mumewe na Naibu Mkuu wa zamani wa Majeshi ya Ulinzi kutoingia nchini humo kwa tuhuma za ufisadi na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.
Katika taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, imesema kuwa Spika Among amewekewa vikwazo kutokana na kuhusika kwake katika ufisadi mkubwa unaohusishwa na uongozi wake wa kibunge, huku Naibu mkuu wa zamani wa jeshi la Uganda, Luteni Jenerali Peter Elwelu akiwekewa vikwazo kutokana na ‘mauaji ya kiholela’ yaliyofanywa na wanajeshi wa nchi hiyo.
Mwenye ufahamu vikwazo hivi vina athiri vipi mtu binafsi?
SOURCE: SWAHILI TIMES
Marekani imewawekea vikwazo maafisa watano wa Uganda, akiwemo Spika wa Bunge la nchi hiyo, Anita Among, mumewe na Naibu Mkuu wa zamani wa Majeshi ya Ulinzi kutoingia nchini humo kwa tuhuma za ufisadi na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.
Katika taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, imesema kuwa Spika Among amewekewa vikwazo kutokana na kuhusika kwake katika ufisadi mkubwa unaohusishwa na uongozi wake wa kibunge, huku Naibu mkuu wa zamani wa jeshi la Uganda, Luteni Jenerali Peter Elwelu akiwekewa vikwazo kutokana na ‘mauaji ya kiholela’ yaliyofanywa na wanajeshi wa nchi hiyo.
Mwenye ufahamu vikwazo hivi vina athiri vipi mtu binafsi?
SOURCE: SWAHILI TIMES