Mosachaoghoko
Senior Member
- Apr 19, 2011
- 137
- 10
Ni matumaini yangu kuwa mpo salama,kwa upande wangu namshukuru Mungu.
Kwanza kabisa ni-declare interest kwamba mimi ni wa mkoa wa Mara,wilaya ya Serengeti,tarafa ya Ngoreme,kata ya Kenyamonta.
Nina machache leo ya kuzungumza na wana-Mara wenzangu kuhusu mkoa wetu.
Mkoa wa mara ulikuwa na kasifa hivi hasa kalikoletwa na mwl nyerere,kwamba baba wa taifa kutoka mara.Zaidi ya hapo tunabaki na sifa za kijinga tu ambazo kimsingi haziujengi mkoa wetu bali kuudidimiza na sisi tunabaki kuchekelea tu huku nyumba inaungua.
Mji mkuu wa mkoa wa Mara ni Musoma mjini,mtakubaliana nami kuwa mji ule umekuwa kama mtoto aliyesumbuliwa na kwashiakoo kwa muda mrefu,yaani umedumaa,hauna mabadiliko chanya tangu nianze kuwa na ufahamu,bali unakuwa kwa kwenda nyuma.
Wilaya ya Serengeti na Taarime zimekuwa zikisifika kwa fujo na watu wake eti kuitwa majasiri,hizo ni sifa za kijinga na wanaotuita hivyo wanafanya makusudi kutudumaza kimaendeleo.
Wilaya ya Serengeti,Musoma vijijini,na Bunda zinaelekea kugeuka jangwa.Wachoma mikaa wamefyeka kupita kiasi,huku watendaji wa serikali wakiwepo tu.Hawana uchungu maana wengi wao ni wa kupita tu,sisi wakudumu ndo tumeamua kujitengenezea jangwa.
Ujasiri wetu uko wapi kama si ujinga,tuna sehemu kubwa ya ziwa victoria,samaki wanavuliwa,minofu inatolewa,kisha watu wetu wanakula mifupa(mapanki),huo ndio ujasiri.
Mbuga ya Serengeti kwa asilimia kubwa ipo mkoani Mara,lakini kupata nyama kama kitoweo kwa siku hizi kupitia mbuga ni dhambi ambayo adhabu yake ni kupigwa risasi hadi kufa.Kama mtakumbuka zamani kulikuwa na kipindi fulani kwa mwaka wanaruhusu wananchi kuwinda kwa ajiri ya kitoweo.Hakukua na tatizo,wala hatujawahi kusikia wanyama wamepungua,ilikuwa ecosystem ya kawaida kwani sisi ni sehemu ya mbuga.Mfumo umefutwa,mbuga sasa iko na VIP,ukitaka kutangulia mbele ya haki katiza mbugani.Tumebaki kuangalia tu,wamefika mahali twiga wanabebwa na kupelekwa nje,eti mkoa wa Mara ni majasiri,sifa za kijinga.
Madini ya dhahabu yapo kwa wingi mkoani Mara,kuna Nyamongo,Buhemba,Park Nyigoti,Majimoto japo kwa uchache.Tunafaidije kama si kusaidia mkoa wa Mara kuwa na takwimu ya juu kwa virusi vya ukimwi na ukimwi(7.8%)
Eti mkoa wa Mara ni majasiri,sifa za kijinga.
Mkoa umekosa chuo cha maana cha utalii na Hotel management,vipo vya hovyo tu.Vyuo vya maana vipo Arusha na hivyo waajiriwa wengi wa hotel za mbugani wanatoka Arusha,Mara tunabaki kulalamika tu.Eti sisi ni majasiri,sifa za kijinga hizi.
Rais analazimisha kupitisha barabara ya lami mbugani kwa maslahi yake binafsi(Kwa sababu ana hotel mbugani),watu wa mkoa wa mara tumenyamaza tu,wakati tunafahamu madhara yake.Eti majasiri,ujinga huu.
Mbuga ipo kwetu,ukipita barabara ya mbugani unalazimika kulipa ada ya kupita mbugani,kama vile wewe ni mtalii.Huu ni uhuni tunafanyiwa,udau wetu juu ya hii mbuga upo wapi.Kwanini ulazimishwe kukatwa pesa hiyo wakati hukuwa na mpango wa utalii.Eti Mara majasiri.
Tukiendelea kubweteka na sifa hizi za kijinga kuna wakati utafika Mara itatambulishwa kama sehemu ya Arusha,"AMINI NAWAAMBIENI"
Waliotufikisha hapa wanajulikana,imefika wakati Mkoa wa Mara kuanzisha muungano wa vijana wa MKOA.Vijana wa Mara wakiwa na sauti moja,wanaweza kupanga vipaumbele vya mkoa,na mwanasiasa yeyote atakaetaka ridhaa yetu aonyeshe nia ya dhati kabisa ya kushughulikia vipaumbele hivyo.Vijana tunaweza kufanya hivyo,lakini pia umefika wakati wa sisi vijana kuufanyia kitu mkoa wetu pamoja na taifa kwa ujumla.
Nilikuwa naongea na mmoja wa wabunge wa mkoa wa Mara eti anasema mkoa umedhorota kwa sababu vijana wake wengi ni walevi,so what?ana maanisha hakuna mabadiliko?kwanini aliomba uongozi.
Naomba tupeane maoni juu ya mkoa wetu,tukosoane kwa kujenga na ikiwezekana tuje na harakati mpya za kuujenga mkoa wetu.
Mods kama kuna madainayoendana na hii ilishatolewa naomba msii-combine,nataka kupata maoni ya wadau.
Akohi nimekupata vema,ni kweli nina draft ya katiba hapa,nita-share na kila anaetaka.Kuendelea kuzungumza huku tumejificha nyuma ya keybord ni dalili za kushindwa hata kuliko wazazi wetu.Namba zako nimeziona,nitakutafuta baadae kidogo.Nafanya kila lililo ndani ya uwezo wangu ili katiba ipate usajiri,nitaitangaza ili kuungwa mkono,na hapo tutafahamiana sana tu.Mara ni yetu, tuna rasilimali za kutosha,tunahitaji kuijenga.
Ni matumaini yangu kuwa mpo salama,kwa upande wangu namshukuru Mungu.
Kwanza kabisa ni-declare interest kwamba mimi ni wa mkoa wa Mara,wilaya ya Serengeti,tarafa ya Ngoreme,kata ya Kenyamonta.
Nina machache leo ya kuzungumza na wana-Mara wenzangu kuhusu mkoa wetu.
Mkoa wa mara ulikuwa na kasifa hivi hasa kalikoletwa na mwl nyerere,kwamba baba wa taifa kutoka mara.Zaidi ya hapo tunabaki na sifa za kijinga tu ambazo kimsingi haziujengi mkoa wetu bali kuudidimiza na sisi tunabaki kuchekelea tu huku nyumba inaungua.
Mji mkuu wa mkoa wa Mara ni Musoma mjini,mtakubaliana nami kuwa mji ule umekuwa kama mtoto aliyesumbuliwa na kwashiakoo kwa muda mrefu,yaani umedumaa,hauna mabadiliko chanya tangu nianze kuwa na ufahamu,bali unakuwa kwa kwenda nyuma.
Wilaya ya Serengeti na Taarime zimekuwa zikisifika kwa fujo na watu wake eti kuitwa majasiri,hizo ni sifa za kijinga na wanaotuita hivyo wanafanya makusudi kutudumaza kimaendeleo.
Wilaya ya Serengeti,Musoma vijijini,na Bunda zinaelekea kugeuka jangwa.Wachoma mikaa wamefyeka kupita kiasi,huku watendaji wa serikali wakiwepo tu.Hawana uchungu maana wengi wao ni wa kupita tu,sisi wakudumu ndo tumeamua kujitengenezea jangwa.
Ujasiri wetu uko wapi kama si ujinga,tuna sehemu kubwa ya ziwa victoria,samaki wanavuliwa,minofu inatolewa,kisha watu wetu wanakula mifupa(mapanki),huo ndio ujasiri.
Mbuga ya Serengeti kwa asilimia kubwa ipo mkoani Mara,lakini kupata nyama kama kitoweo kwa siku hizi kupitia mbuga ni dhambi ambayo adhabu yake ni kupigwa risasi hadi kufa.Kama mtakumbuka zamani kulikuwa na kipindi fulani kwa mwaka wanaruhusu wananchi kuwinda kwa ajiri ya kitoweo.Hakukua na tatizo,wala hatujawahi kusikia wanyama wamepungua,ilikuwa ecosystem ya kawaida kwani sisi ni sehemu ya mbuga.Mfumo umefutwa,mbuga sasa iko na VIP,ukitaka kutangulia mbele ya haki katiza mbugani.Tumebaki kuangalia tu,wamefika mahali twiga wanabebwa na kupelekwa nje,eti mkoa wa Mara ni majasiri,sifa za kijinga.
Madini ya dhahabu yapo kwa wingi mkoani Mara,kuna Nyamongo,Buhemba,Park Nyigoti,Majimoto japo kwa uchache.Tunafaidije kama si kusaidia mkoa wa Mara kuwa na takwimu ya juu kwa virusi vya ukimwi na ukimwi(7.8%)
Eti mkoa wa Mara ni majasiri,sifa za kijinga.
Mkoa umekosa chuo cha maana cha utalii na Hotel management,vipo vya hovyo tu.Vyuo vya maana vipo Arusha na hivyo waajiriwa wengi wa hotel za mbugani wanatoka Arusha,Mara tunabaki kulalamika tu.Eti sisi ni majasiri,sifa za kijinga hizi.
Rais analazimisha kupitisha barabara ya lami mbugani kwa maslahi yake binafsi(Kwa sababu ana hotel mbugani),watu wa mkoa wa mara tumenyamaza tu,wakati tunafahamu madhara yake.Eti majasiri,ujinga huu.
Mbuga ipo kwetu,ukipita barabara ya mbugani unalazimika kulipa ada ya kupita mbugani,kama vile wewe ni mtalii.Huu ni uhuni tunafanyiwa,udau wetu juu ya hii mbuga upo wapi.Kwanini ulazimishwe kukatwa pesa hiyo wakati hukuwa na mpango wa utalii.Eti Mara majasiri.
Tukiendelea kubweteka na sifa hizi za kijinga kuna wakati utafika Mara itatambulishwa kama sehemu ya Arusha,"AMINI NAWAAMBIENI"
Waliotufikisha hapa wanajulikana,imefika wakati Mkoa wa Mara kuanzisha muungano wa vijana wa MKOA.Vijana wa Mara wakiwa na sauti moja,wanaweza kupanga vipaumbele vya mkoa,na mwanasiasa yeyote atakaetaka ridhaa yetu aonyeshe nia ya dhati kabisa ya kushughulikia vipaumbele hivyo.Vijana tunaweza kufanya hivyo,lakini pia umefika wakati wa sisi vijana kuufanyia kitu mkoa wetu pamoja na taifa kwa ujumla.
Nilikuwa naongea na mmoja wa wabunge wa mkoa wa Mara eti anasema mkoa umedhorota kwa sababu vijana wake wengi ni walevi,so what?ana maanisha hakuna mabadiliko?kwanini aliomba uongozi.
Naomba tupeane maoni juu ya mkoa wetu,tukosoane kwa kujenga na ikiwezekana tuje na harakati mpya za kuujenga mkoa wetu.
Mods kama kuna madainayoendana na hii ilishatolewa naomba msii-combine,nataka kupata maoni ya wadau.
Mgawanyiko upo hata ndani ya vijana wenyewe; pale chuo kikuu cha mlimani (UDSM) nakumbuka kulikua na vyama vitatu vya mkoa wa Mara: kimoja kinajumuisha makabila yote yanahusiana na jamii ya wakurya, kingine makabila yanayohusiana na jamii ya wajita, na kingine kabila la wajaluo! Ukiangalia hata chaguzi zote Musoma mjini nasikia kampeni huwa zinaendana na makundi hayo matatu ya kikabila.
Ingawa ni kweli kuna umuhimu wa kuangalia maendeleo ya mkoa na kuachana na mambo ya migawanyiko iliyoko isiyokua na maana yoyote.
Mimi pia mjita, jamaa amekariri sifa za kijinga mara nyingi hadi post limepoteza ladha, halafu hana solution hata moja yeye ni wa kulalama tu, wacha niende jukwaa la mahusiano........
Nitakutafuta tata ucjali.Mara ni yetu soteSagaka, tutafutane 0767381531
Mihayo,kwa kuanza tayari nime-draft katiba ya Muungano wa Vijana wa Serengeti,naomba tuungani kuiokoa Mara yetu.
Samahani ni makosa tu madogo,ni draft ya Muungano wa Vijana wa Mara(MUVIMA).Utanisamehe wakupita.Nilifikiri ni katiba ya Mkoa wa Mara kumbe ni Serengeti pekee!:A S cry:
Ndugu yangu hawa vijana wa mkoa huu na VIMORO HASA WALIOKO PEMBENI MWA HIFADHI NI VIGUMU SANA KUSAHAU HICHO " IBING'ARA, ANYAMA ORI " Ha ha ha ha ha ha very great power is needed to change them ila tutie nguvu ili tuwatoe kwenye fikra hzo maana ni watanzania wenzetu.
Mm nimekulia huko na kusoma primary na o level huko yaan tulifaulu wengi tu wakati wa kuhitimu elimu ya msingi ila tuliojiunga sec ni kiduchu na hasa wa kutoka mikoa mingine,wengi wao walisema kusomesha mtoto 4 yrs n kupoteza muda wa uzalishaji mali na watoto wao nao walikuwa wanashabikia tu wanashabikia hilo hadi namaliza chuo kikuu pale mliman kulikuwa na vijana kama 4 niliowafahamu kutoka serengeti hii ni aibu AMKEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEENI SASA TUTAWAUNGA MKONO SISI WAKUJA HUKO.
safi sana mkuu, inapendeza kuongea kwa vitendo, tunasubiri mwaliko wako ili tuweze kuchangia japo mawazo ni kweli kile ki-mkoa kimekaa vibaya kidogo na ni jukumu letu kuweka mambo sawa, wana siasa wamekuwepo siku zote na kamwe hawana nia ya kufanya chochote pale zaidi ya kuomba kura kila baada ya mudaTata mwitongo sijajua una umri gani,lakini kama mnaweza naomba tuanzishe "MUUNGANO WA VIJANA WA MARA"Usiokuwa na itikadi yoyote kisiasa(maana siasa zimetufikisha tulipo),utakuwa na nguvu,ili vijana watumie fursa za kiuchumi zilizopo kimkoa,kitaifa na hata kimataifa kujijenga kiuchumi,kimaamuzi na kuiokoa mara yetu.Nabhamwe tole bhamura.Kwa kuanza tu nimeandaa katiba ya muungano huo,imebaki kufany reg.na kuiweka hadharani tayari kwa kuomba kuungwa mkono na vijana wa Mkoa wa Mara.
Mara itajengwa na wana-Mara wenyewe,achana na wadandiaji.Namba zangu za simu ni 0782 577 006,tutafutane ndugu tuzungumzie harakati zetu.Kwahiyo wewe unafurahia wazungu kuja kuwinda wanyama wetu kwa raha mustarehe lakini sisi wenyeji ambao tumekulia mazingira hayo miaka na miaka tunanyanyaswa tusiguse nyama pori kabisa.
Siku za nyuma kulikuwa na msimu wa uwindaji, mara moja kwa mwaka, ambapo uliwekwa utaratibu wa kutoa vibali vya uwindaji kwa wananchi. Hapo ndipo wananchi wanaoishi kuizunguka mbuga ya serengeti walipata nafasi ya kuuziwa nyama pori kutoka kwa wawindaji walioruhusiwa kufanya biashara ya uwindaji wa nyama pori.
Kwamba hushangai wamasai kuachwa kuendelea kuishi ndani ya ngorongoro lakini unashangaa wakurya na waikoma kula kimro/king'ara? Kuna vitu vingine unapovifanya ambavyo vina athari ya moja kwa moja na maisha ya watu lazima uwape kitu mbadala, si suala la kukurupuka tu na kuweka sheria ambazo zinawakandamiza natives na kuwanufaisha wageni, na hili ni tatizo la watanzania kuwapapatikia sana wageni kuliko wasawahili wenzao.
Wakati mwingine mnapojaribu kutoa maoni yenu muwe na adabu, sio mnaropoka tu kama zimewafyatuka. Afterall hapa ni mjadala wa wanamara kwa ajili ya kutafuta namna ya kujikwamua na madhila tuliyonayo, sasa nyie mliopata nafasi ya kujikwamua kupitia rasilimali zenu mnatakiwa muonyeshe heshima na si madharau kwani kwa kufanya hivyo hatutahitaji tena ushauri wako katika hili, nenda tu ukajenge/ukaendeleze kwenu utuache na Mugumu yetu sisi wenyewe tutaweza kuifikisha mahali tunapotaka.