Mfiaukweli
JF-Expert Member
- Aug 30, 2018
- 5,636
- 8,777
UTANGULIZI
Wakuu; hivi karibuni Waziri wa Fedha Dr Mpango alialika watu kutoa maoni yao kuhusu mambo wanayoyaona kuwa ni kikwazo (au vikwazo) kwao katika kufanya biashara na akaahidi kuwa serikali itayafanyia kazi maoni hayo. Ni kwa sababu ya wito huo (najua watu wa serikali hupitia hapa) natoa maoni yangu na kuomba wadau wengine nao watoe maoni yao.
Angalizo: Naomba tutoe maoni kuhusu vikwazo vilivyopo kwenye kufanya biashara (kama kuna mtu anaeona kila kitu kinaenda sawa HANA SABABU ya kutoa hizo "sifa" zake kwenye uzi huu tafadhali). For once let's be serious.
MAONI
Baada ya utangulizi huo, naomba nitoe maoni yangu kama ifuatavyo:
1. Jambo kubwa kuliko yote ambalo limekuwa KIKWAZO kikubwa katika kufanya biashara (hasa tangu serikali hii iingie madarakani) ni kufanya maamuzi bila kuzingatia sheria. Mhe.Waziri, HAKUNA kitu wawekezaji wanakiangalia (kabla ya kuwekeza) kama certainty (uhakika) kwenye kanuni zilizopo nchini. Mnapotoa matamko yanayofuta sheria na taratibu zilizokuwepo instantly zinamfanya mfanyabiashara asijue atarajie nini kesho (maana alichopanga kukifanya leo kinaweza kukatazwa kesho na hatafidiwa hasara atakayoipata).
Kitu cha pili kinachohusiana na utawala wa sheria ni hii tabia/dhana iliyojengeka sasa hivi kuwa serikali inaweza kumuonea mtu lakini yenyewe ikawa na kinga ya kushtakiwa (na hata ikishtakiwa na ikashindwa hailazimiki kuwajibika kumfidia muathirika). LAZIMA turudishe na kuimarisha investors' confidence kwa nchi hii (ambayo kwa sasa hivi naamimi hata wewe mwenyewe Mh. Waziri unajua kuwa haipo).
2. TRA wafanye kazi zao kwa haki. Sasa hivi imezuka tabia ya kubambikia madai ya kodi (huku maafisa wa TRA wakijua fika kuwa HAKUNA hata chembe ya ukweli kwenye hayo madai) ili tu mfanyabiashara alazimishwe kulipa jspo theluthi ya madai hayo bandia (maana sheria inamtaka mlipa kodi kulipa theluthi moja ya kile alichodaiwa - hata pale kunapokuwa na ushahidi dhahiri kuwa madai si sahihi ili objection yake isikilizwe). Sheria hii inakuwa abused sana hivi sasa na maafisa wa TRA wanafanya hivyo with impunity wakijua hawawezi kuchukuliwa hatua kutokana na kufanya uonevu huo. Mh. Waziri; fanya uchunguzi kidogo tu na utajionea mwenyewe ni wafanyabiashara wangapi wameacha kufanya biashara nchi hii kipindi cha miaka mitatu iliyopita na kati yao ni wangapi ambao hawakuguswa na kadhia hii ya kulazimishwa kufanya objection kwa kulipa theluthi moja ya incorrect and unrealistic tax demands.
3. Nchi hii sasa hivi inakabiliwa na uhaba mkubwa wa skilled labour hasa kwenye kazi zinazohusiana na masuala ya business na financial management, IT na hata kwenye elimu. Mh. Waziri, wahitimu wa vyuo vyetu hawana competence inayohitajika na labour market. Ruhusuni sekta binafsi kuajiri watu inaoona ni competent mahali popote (japo utaratibu mzuri uwekwe ili kuzuia watu wasiostahili kupewa vibali). Hatua hii itawezesha skills transfer kuja nchini.
Mh. Waziri, maoni yangu yamelenga kusaidia sekta binafsi ambayo ni mdau muhimu kwa maendeleo ya nchi hii.
Yangu ni hayo kwa leo.
Wakuu; hivi karibuni Waziri wa Fedha Dr Mpango alialika watu kutoa maoni yao kuhusu mambo wanayoyaona kuwa ni kikwazo (au vikwazo) kwao katika kufanya biashara na akaahidi kuwa serikali itayafanyia kazi maoni hayo. Ni kwa sababu ya wito huo (najua watu wa serikali hupitia hapa) natoa maoni yangu na kuomba wadau wengine nao watoe maoni yao.
Angalizo: Naomba tutoe maoni kuhusu vikwazo vilivyopo kwenye kufanya biashara (kama kuna mtu anaeona kila kitu kinaenda sawa HANA SABABU ya kutoa hizo "sifa" zake kwenye uzi huu tafadhali). For once let's be serious.
MAONI
Baada ya utangulizi huo, naomba nitoe maoni yangu kama ifuatavyo:
1. Jambo kubwa kuliko yote ambalo limekuwa KIKWAZO kikubwa katika kufanya biashara (hasa tangu serikali hii iingie madarakani) ni kufanya maamuzi bila kuzingatia sheria. Mhe.Waziri, HAKUNA kitu wawekezaji wanakiangalia (kabla ya kuwekeza) kama certainty (uhakika) kwenye kanuni zilizopo nchini. Mnapotoa matamko yanayofuta sheria na taratibu zilizokuwepo instantly zinamfanya mfanyabiashara asijue atarajie nini kesho (maana alichopanga kukifanya leo kinaweza kukatazwa kesho na hatafidiwa hasara atakayoipata).
Kitu cha pili kinachohusiana na utawala wa sheria ni hii tabia/dhana iliyojengeka sasa hivi kuwa serikali inaweza kumuonea mtu lakini yenyewe ikawa na kinga ya kushtakiwa (na hata ikishtakiwa na ikashindwa hailazimiki kuwajibika kumfidia muathirika). LAZIMA turudishe na kuimarisha investors' confidence kwa nchi hii (ambayo kwa sasa hivi naamimi hata wewe mwenyewe Mh. Waziri unajua kuwa haipo).
2. TRA wafanye kazi zao kwa haki. Sasa hivi imezuka tabia ya kubambikia madai ya kodi (huku maafisa wa TRA wakijua fika kuwa HAKUNA hata chembe ya ukweli kwenye hayo madai) ili tu mfanyabiashara alazimishwe kulipa jspo theluthi ya madai hayo bandia (maana sheria inamtaka mlipa kodi kulipa theluthi moja ya kile alichodaiwa - hata pale kunapokuwa na ushahidi dhahiri kuwa madai si sahihi ili objection yake isikilizwe). Sheria hii inakuwa abused sana hivi sasa na maafisa wa TRA wanafanya hivyo with impunity wakijua hawawezi kuchukuliwa hatua kutokana na kufanya uonevu huo. Mh. Waziri; fanya uchunguzi kidogo tu na utajionea mwenyewe ni wafanyabiashara wangapi wameacha kufanya biashara nchi hii kipindi cha miaka mitatu iliyopita na kati yao ni wangapi ambao hawakuguswa na kadhia hii ya kulazimishwa kufanya objection kwa kulipa theluthi moja ya incorrect and unrealistic tax demands.
3. Nchi hii sasa hivi inakabiliwa na uhaba mkubwa wa skilled labour hasa kwenye kazi zinazohusiana na masuala ya business na financial management, IT na hata kwenye elimu. Mh. Waziri, wahitimu wa vyuo vyetu hawana competence inayohitajika na labour market. Ruhusuni sekta binafsi kuajiri watu inaoona ni competent mahali popote (japo utaratibu mzuri uwekwe ili kuzuia watu wasiostahili kupewa vibali). Hatua hii itawezesha skills transfer kuja nchini.
Mh. Waziri, maoni yangu yamelenga kusaidia sekta binafsi ambayo ni mdau muhimu kwa maendeleo ya nchi hii.
Yangu ni hayo kwa leo.