Kwa wazoefu wa Ujenzi ipi Cement bora kati ya Rhino,Tembo na Twiga Cement?

Kwa wazoefu wa Ujenzi ipi Cement bora kati ya Rhino,Tembo na Twiga Cement?

Master Legendary

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
576
Reaction score
876
Wadau naomba Msaada pls nataka kuanza ujenzi wa Msingi(Foundation)Mafundi wananichanganya sana,ipi Cement bora kati ya Rhino ya Dar,Tembo Cement ya Mbeya Na Twiga Cement ya Tanga?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Tumia cement inayotoka pakistani,au cement ya Lucky,izo ni cement nzuri mkuu,
 
Wadau naomba Msaada pls nataka kuanza ujenzi wa Msingi(Foundation)Mafundi wananichanganya sana,ipi Cement bora kati ya Rhino ya Dar,Tembo Cement ya Mbeya Na Twiga Cement ya Tanga?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums


zote ni nzuri kwa kujengea,
Kwa plaster Twiga ni best, Rhino inasumbua
 
Kuna nyingine ambayo inatangazwa sana sasa hivi ITV, inaitwa NYATI!
 
Nashukuru wakuu mwenye ujuzi zaidi aendelee kunipa ushauri.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Twiga ndiyo bora.

Cement za nje ni nzuri huko kwao, zinaposafirishwa kwa njia ya bahari unyevu nyevu ndani ya bahari ni mkubwa na hupunguza sana ubora wa cement.
 
Linapokuja suala la bidhaa za nje Vs za ndani, mara nyingi napendelea za ndani lakini ktk cement uzoefu wangu ni kuwa za pakstan zimekuwa nzuri kwangu. Nyingine nzuri ni rhino, simba bora (siyo simba imara) Mkuu tumia hizo kwa matokeo makubwa
 
Wadau naomba Msaada pls nataka kuanza ujenzi wa Msingi(Foundation)Mafundi wananichanganya sana,ipi Cement bora kati ya Rhino ya Dar,Tembo Cement ya Mbeya Na Twiga Cement ya Tanga?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

kwa ajili ya msingi tafuta cement yenye hizi namba kwenye mfuko :42.5 N au 42.5R. Plaster ni Namba 32.5N au 32.5R
 
kweli jamii forum ni zaidi niijuavyo yaani kila swali liulizwalo jibu halikosekani.
 
Twiga cement iko vizuri so far twiga ordinary 42'5 au twiga extra kwa kweli ziko njema.
Shida nilizowahi kukumbana nazo ni wizi katika hii mifuko Yao. Utakuta mfuko una upungufu wa 5 -7kg. Yaani expected 50kg utakuta jamaa wamepoga bomba zimesalia 45kg or less. Za Pakistani nzr na zinakauka mapema compared to others na so far wizi si ki vile! So kama mafundi watazingatia ratio vzr zote zinafaa. But if u ask me will go for twiga
 
Ukipata Simba Cement ni bora kuliko zote lakini kwa Dar siioni madukani. Twiga inafaa ingawa wauzaji wanapoga bomba na mifuko hsifiki Kg. 50. Kuwa mwangalifu na saruji za kutoka nje, zinakauka haraka lakini uimara wake ni mashaka.
 
cement pekee kwenye market ya tanzania yenye sifa hiyo ni NYATI CEMENT ambayo inakauka haraka na hudumu zaidi yaani quick setting time with high strength au kuna mtu anabisha kwenye hili
 
Wadau naomba Msaada pls nataka kuanza ujenzi wa Msingi(Foundation)Mafundi wananichanganya sana,ipi Cement bora kati ya Rhino ya Dar,Tembo Cement ya Mbeya Na Twiga Cement ya Tanga?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

hakuna twiga ya tanga mkuu,
 
Back
Top Bottom