Uchaguzi wa serikali za mitaa umepita yaliyotokea tumeyaona na yametoa muelekeo mpya kuelekea uchaguzi mkuu 2025.
Kwa viongozi walionao kuanzia katibu mkuu,naibu katibu mkuu na katibu mwenezi CCM imeonyesha udhaifu mkubwa kwenye siasa za ushindani.
Ili kurudi kuwa chama cha siasa bila kuhusishwa na vyombo vya dola, chama cha mapinduzi kinahitaji watendaji wapya ambao wateleta siasa ya nguvu ya hoja na sio hoja ya nguvu.
Kwa watu walionao kwenye uongozi wa sasa itakuwa ngumu sana kuwavusha kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Tayari kwa siasa za sasa wameshapoteza mvuto kwa wananchi kwa mambo yaliyotokea kwenye uchaguzi wa serikali ya mtaa, kwa ufupi hawana ushawishi wa jukwaa.
Chama cha Mapinduzi kinatakiwa kifanye mabadiliko kurudisha nguvu iliyokuwa nayo kwenye siasa za nchi hii ili kushinda uchaguzi kwa haki.
Kwasababu mpaka leo hii hawana makamu mwenyekiti wa chama ingefaa komredi Emanuel Nchimbi achukue nafasi hiyo.
Nafasi ya Katibu mkuu apewe Humphrey Polepole, Nafasi ya katibu mwenezi apewe Makongoro Nyerere.
Nasema hivyo kwasababu zifuatazo kwanza Balozi Emanuel Nchimbi ameshakuwa katibu mkuu ameshapata uzoefu tayari wa utendaji kichama atamsaidia vizuri mwenyekiti wao kuongoza chama.
Balozi Humphrey Polepole akipewa ukatibu mkuu wa chama kwanza atasaidia kundi kubwa la vijana kurejea kuwa na imani na chama kwa sababu watakuwa wamepata kijana mwezao .
Na vile vile kwa uzoefu wake aliopata katika awamu iliyopita alivyokuwa katibu mwenezi na sasa ni balozi haitakuwa ngumu kwake kuongoza chama na watendaji waliopo chini yake watamheshimu.
Kwa upande wa Makongoro Nyerere kwanza nimzungumzaji mzuri wa jukwaa kwa ufupi ana mvuto na ushawishi wa kisiasa kumsikiliza kama baba yake.
CCM kama ikitaka kurudi kuwa chama cha siasa bila kutegemea nguvu ya nje ya chama Makongoro ni mtu pekee anayeweza kuwarudisha kwenye siasa zenye mvuto za majukwaani.
Kuelekea uchaguzi mkuu 2025 bila mabadiliko ya kiuongozi CCM itapata shida sana hawa waliopo wameshaonyesha kufeli.
Kwa viongozi walionao kuanzia katibu mkuu,naibu katibu mkuu na katibu mwenezi CCM imeonyesha udhaifu mkubwa kwenye siasa za ushindani.
Ili kurudi kuwa chama cha siasa bila kuhusishwa na vyombo vya dola, chama cha mapinduzi kinahitaji watendaji wapya ambao wateleta siasa ya nguvu ya hoja na sio hoja ya nguvu.
Kwa watu walionao kwenye uongozi wa sasa itakuwa ngumu sana kuwavusha kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Tayari kwa siasa za sasa wameshapoteza mvuto kwa wananchi kwa mambo yaliyotokea kwenye uchaguzi wa serikali ya mtaa, kwa ufupi hawana ushawishi wa jukwaa.
Chama cha Mapinduzi kinatakiwa kifanye mabadiliko kurudisha nguvu iliyokuwa nayo kwenye siasa za nchi hii ili kushinda uchaguzi kwa haki.
Kwasababu mpaka leo hii hawana makamu mwenyekiti wa chama ingefaa komredi Emanuel Nchimbi achukue nafasi hiyo.
Nafasi ya Katibu mkuu apewe Humphrey Polepole, Nafasi ya katibu mwenezi apewe Makongoro Nyerere.
Nasema hivyo kwasababu zifuatazo kwanza Balozi Emanuel Nchimbi ameshakuwa katibu mkuu ameshapata uzoefu tayari wa utendaji kichama atamsaidia vizuri mwenyekiti wao kuongoza chama.
Balozi Humphrey Polepole akipewa ukatibu mkuu wa chama kwanza atasaidia kundi kubwa la vijana kurejea kuwa na imani na chama kwa sababu watakuwa wamepata kijana mwezao .
Na vile vile kwa uzoefu wake aliopata katika awamu iliyopita alivyokuwa katibu mwenezi na sasa ni balozi haitakuwa ngumu kwake kuongoza chama na watendaji waliopo chini yake watamheshimu.
Kwa upande wa Makongoro Nyerere kwanza nimzungumzaji mzuri wa jukwaa kwa ufupi ana mvuto na ushawishi wa kisiasa kumsikiliza kama baba yake.
CCM kama ikitaka kurudi kuwa chama cha siasa bila kutegemea nguvu ya nje ya chama Makongoro ni mtu pekee anayeweza kuwarudisha kwenye siasa zenye mvuto za majukwaani.
Kuelekea uchaguzi mkuu 2025 bila mabadiliko ya kiuongozi CCM itapata shida sana hawa waliopo wameshaonyesha kufeli.