Kwa yanayoendelea kwenye mitandao ya kijamii, kama ukurasa huu ni wa Serikali basi ni aibu

Kwa yanayoendelea kwenye mitandao ya kijamii, kama ukurasa huu ni wa Serikali basi ni aibu

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
Wakuu, huku tukiwa tunaendelea na shamra shamra za Uchaguzi mkuu. Kuna ukurasa unaojiita Mawaziri & Manaibu Tz. Dhumuni ya ukurasa huo ni kuonesha taarifa na habari mbali mbali za manaibu waziri wote Tanzania. Ukurasa huu umejiunga na mtandao wa Twitter mwaka 2018 na umekuwa ukituhabarisha taarifa mbali mbali muhimu kwa mustakabali wa nchi yetu.

Katika hali ya kushangaza ukurasa huo umekuwa katika majibizano kutetea serikali ya awamu ya tano dhidi ya moja wapo ya watumiaji wa mtandao huo. Majibizano hayo yanaonekana kufanywa na mtu mwenye gadhabu ambaye anaonekana wazi kabisa kuandika maudhui ambayo ni mtizamo wake binafsi na si wa serikali/mawaziri na makatibu wake.

Kuna umuhimu wa kuwapatia hawa waratibu wa akaunti hizi za zinazowakilisha serikali kwa jamii, wanaweza kuwa na nia njema ya kuitetea serikali lakini si kwa kujibizana mtandaoni. Serikali ni taasisi kubwa na inaweza kusikia mengi yanayosemwa lakini si kujibizana na kila jambo papo kwa hapo.

Screenshot_20200826-152739_Chrome.jpg
 
Makurasa mengine kama hayo ni ya kazi gani ?
Ni kutoa taarifu kiujumla zimazohusu utendaji wa Mawaziri/Manaibu waziri, lengo lake ni zuri baadala ya mtu kufuatilia kila wizara/waziri anaweza kupata taarifa muhimu kutoka ukurasa mmoja. Tatizo ni jinsi zinavyoratibiwa ndio inaweza kuzifanya zipoteze umuhimu na maana
 
We akili hauna, huo toka lini ukawa ukurasa wa serikali?
 
Back
Top Bottom