Kwako waziri wa kilimo, Hussein Bashe naomba msaada wako

Kwako waziri wa kilimo, Hussein Bashe naomba msaada wako

clinton gidioni

Senior Member
Joined
Oct 24, 2016
Posts
145
Reaction score
165
Kiukweli, unatupambania sana vijana na hakika unatutakia mema. Kijana yeyote anayejitahidi kupambana lazima ataona juhudi zako.

Mheshimiwa, nimejitahidi kadri ya uwezo wangu, lakini nimeshindwa kufanikisha mambo kupitia fani na taaluma nilizonazo. Kwa sasa, nimeamua kuanza upya maisha yangu na kuingia kwenye kilimo chenye tija. Uamuzi huu nimeufanya binafsi, bila kushauriwa na mtu yeyote.

Hata hivyo, sina chochote kama kianzio – sina ardhi wala mbegu. Mtaji pekee nilionao ni afya, akili, na nguvu za kufanya kazi. Hitaji langu kubwa ni kupata ardhi ya kulima, na endapo nitapata kupitia BBT (Building a Better Tomorrow), itakuwa vyema zaidi.

Nimepita kwenye baadhi ya mashamba ya BBT na kuona juhudi zako, Mheshimiwa. Nipo tayari kuanza kazi hata leo. Sitaki kupoteza muda zaidi. Naomba msaada wako, Mheshimiwa Hussein Bashe.
 
Kuna wengine tunalima kilimo Cha kutegemea mawingu Yani unaweza pata presha
Ikifika mwezi wa pili mvua zinasimama muda mrefu mpaka inafikia muda unaamka usiku kuangalia mawingu yapoje ,kama ni ya mvua au la
Kiukweli Kuna muda vijana tunapitia magumu mno
 
Kuna wengine tunalima kilimo Cha kutegemea mawingu Yani unaweza pata presha
Ikifika mwezi wa pili mvua zinasimama muda mrefu mpaka inafikia muda unaamka usiku kuangalia mawingu yapoje ,kama ni ya mvua au la
Kiukweli Kuna muda vijana tunapitia magumu mno
mkuu nikweli ila hana namna mdogo mdogo mwisho utaingia kwenye kilimo cha umwagiliaji
 
NDOTO YANGU NI KUPATA ENEO LANYE MAJI ILI KUFANYA KILIMO CHA MBOGA MBOGA NA MAZAO YA MDA MFUPI KAMA HOHO NYANYA CHUNGU NA PILIPILI NA UFUGAJI WA KUKU
 
Back
Top Bottom