Kwamba kuapishwa kwa wabunge 19 viti maalumu CHADEMA, chama hakijashiriki kufanya uteuzi sawasawa na sheria zinavyotaka. Nini maana yake hasa?

The Beautyful Ones Are Not Yet Born
- Ayi Kwei Armah

Naendelea kusoma novel yangu sina haraka πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Ok!,na ili mtuhumiwa atoke gerezani si lazima mahakama ishiriki kwenye maamuzi?Usiku huo Judge alikaa?

Hilo ni wazi kabisa kwamba sheria za nchi zimewekwa pembeni na dola halafu utasikia wakiapa wanasema ewe mwenyezi Mungu nisaidie. Kwa Haya wanayofanya na wamekula kiapo hakuna tofauti na majambazi wanaiba usiku
 
Wananchi wanachosubiri kwa sasa kuona hao viti maalumu wanafukuzwa ili ukirudishia imani
 
Hilo ni wazi kabisa kwamba sheria za nchi zimewekwa pembeni na dola halafu utasikia wakiapa wanasema ewe mwenyezi Mungu nisaidie. Kwa Haya wanayofanya na wamekula kiapo hakuna tofauti na majambazi wanaiba usiku
😁 😁 😁 😁 😁 😁
 
Mkuu naona unataja nguvu ya fedha bila kushangaa hizo pesa zinatoka wapi na zinatumika kwa mipangilio ipi? Huoni kwamba ni habari fikirishi zaidi kwamba Rais wa Tanzania ana uwezo wa kujichukulia kiasi chochote cha pesa toka hazina ya taifa na kuzitumia atakavyo? Anaweza kujigawia na kugawa mabilioni kwa watu binafsi bila kubanwa na sheria za ufisadi au uhujumu uchumi? Tuna nchi hapo kweli?

Hicho ndicho cha kuogopesha zaidi kuliko hao "wapinzani wanaonunuliwa" kwa pesa ambayo ingetumika kulipa madeni na stahiki za kisheria za wananchi pamoja na kuchochea shughuli za kiuchumi kwa ujumla. Bila shaka matokeo ya ufujaji wa aina hii yatatufundisha umuhimu wa kuwa makini na masuala ya kisiasa nchini. Na wanaoshabikia wanasiasa "kuula" kwa hizi dili za kifisadi wataelewa watakapoendelea kushuhudia ajira zikizidi kupotea, kodi zikikaba na wanunuzi wa bidhaa za kimachinga wakizidi kufifia.
 
Hivi hao jamaa hawanaga akili? Hawakuwaza hilo kabisa? Au ndio maovu yanawalewesha
 
Washafukwa uana chama, ama bado?
Kama bado, wana ngoja nini?
 
we are in big trouble as nation....!
We better accept the reality that yes, we are in big trouble!
Hawana kisisi tena mkuu, hata kuuwa raia wameuwa bila soni! chochote kinaweza kutokea. Muhimu wao wanalazimisha matakwa yao na tuliobaki sote ni tutaburuzwa kufanikisha malengo yao! Hakuna alie salama kwa kweli Taifa limevurugwa kila upande!
CCM ya Magufuli iko very desperate and strategic kutekeleza mission hii hatari kabisa ya kishetani....
Na sasa naiona hatari ya tunakopelekwa. Ilikuwaje CCM wakatuletea janga hili?
Anachofanya Magufuli na ambayo ndiyo silaha kuu ndilo anayojivunia kutekeleza adhma yake hii ovu ni kutengeneza njaa ya uhitaji ama njaa ya fedha..
Hapa sasa ndio nawaelewa akina Mayala. Muhimu tujitahidi tusigawanyike au kuchukiana kwa uamuzi wa watu kama kina Mdee. Kwa kweli walijitahidi lakini kila mmoja wetu anaijuwa hali halisi ilivyo. Kuwachukia na kuwatenga kina Mdee ni kufanikisha lengo la 'system'! Kuwafukuza si solution nzuri kwani kuna wengi wengine watatupiwa chambo kama hizi. Tukiamua kufukuza kila mtu wa aina hii chama kitasambaratika vibaya mno! Kwa kuwa hii ndio formula na ni endelevu.
 
Ngoja nijaribu kutabiri matokeo yake; Pesa hawatopata na akina Mdee watapata angalau riski zao za kuwasogeza mbele πŸ˜‚
 
Ok!,na ili mtuhumiwa atoke gerezani si lazima mahakama ishiriki kwenye maamuzi?Usiku huo Judge alikaa?
Spika anasema orodha ya wabunge wateule wa CHADEMA aliipokea kutoka NEC tangu tarehe 20 November (maana yake hao wateule walijaza fomu, kuapichwa mbele ya jaji, kusainiwa na katibu mkuu wa CHADEMA na fomu zao kufikishwa NEC kabla ya 20 November), maajabu ni kwamba Nusrat Hanje aliachiwa huru kutoka gerezani usiku wa tarehe 23 November, halafu tarehe 24 November akaapishwa na spika kuwa mbunge!!!

Yaani system ilishindwa kuwa smart kufanya usanii wake.
 
Haya mambo yanachafuwa taswira ya nchi,huyo aliyekuwa mahabusu hasa ndio anawachafua zaidi maana uteuzi wake unatia ukakasi
Kwa hiyo unataka kusema nini!!??
1. Kwamba Serikali iliamua nani awe Mbunge viti maalum!?
2. Ikaandaa Orodha
2. Ikajaza nyaraka
3. Ikawashawishi wateule wake waende kuapa,
4. Ikawasafirisha sambamba na kuwatoa waliokuwa GEREZANI...!?
5. Kwamba yote haya yamefanyika mbele ya uongozi wa CHAMA bila wao KUJUA wala KUSHIRIKI..!??

NO.. BIG NO.
Yaani, HAIWEZEKANI.

Panua akili wewe, usiishie kupanua vidole tu..
Mnyika anazungumzia nafasi yake Kikatiba kuwasailiana na Tume, anazungumzia nafasi yake kutia saini nyaraka za wateule..
Lakini hahoji ni nani alochukua nafasi hizo!?
Haulizi nani amekuwa akifanya mawasiliano na Tume badala yake,
Haulizi nani amesaini FOMU ZA UTEUZI badala yake..
Karibu Mkuu ni Ofisi..
Kama Mnyika hayupo bado ofisi itaendelea kufanya Kazi, Kuna msaidizi wake Kuna watendaji wanaweza kufanya kwa niaba..

Ndio..,
Njia pekee ya kufanikisha haya kutokea ni KIONGOZI MKUBWA ndani ya chama kushiriki kwa kufanya uteuzi Kisha akaitumia ofisi ya katibu Mkuu (Labda bila SG Mnyika kujua), Akaitumia MIHURI na nyaraka za chama, akawasilisha Orodha kwa mujibu wa SHERIA na Jina Nusrat likiwemo na hapo ndipo Serikali ika compromise kwa kumtoa huyo Nusrat..Kinyume na hapo basi CHADEMA haijawahi kuwa chama cha Upinzani Kama TAASISI hata siku moja..
Bali ni VIBAKA, WAHUNI, MTAPELI, wanaotudanganya eti CHAMA cha siasa
 
Unauliza wakati Chadema iliwahi kulazimishwa kuwa na mbunge akiwa mwanaccm!
 
"anaacha mark kwenye foot print." Kwa uandishi huu, ni wazi unakurupuka sana tu. Kuna kasoro fulani hivi, wataalamu wa afya & saikolojia wanadai ukiwaganako unatend kuwapakazia wengine --- yaani unawaona wao kwa lenzi ya mtufinyuku ulionao wewe binafsi.
 
Hawatakuelewa
 
Kwani hiyo 20 Novemba Ms Nusrat alikuwa hukooo mbali anga za juu kwenye Galaxy ya Andromeida Spiral kwamba ashindwe kufikika na kutekeleza matakwa ya kikatiba????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…