Kwamba Skudu anabaki kwa ajili ya msimu mgumu ujao halafu Guede mmempa Byebye

Kwamba Skudu anabaki kwa ajili ya msimu mgumu ujao halafu Guede mmempa Byebye

JF mbambamba nyingi sana, kocha ndio anatowa report ya wachezaji wa kuachwa, uongozi unatekeleza.
 
Nimesikitika pia mwamba kuondoka, gari lilikuwa lishawaka
Screenshot_20240503-135832_1.jpg
 
Hongera kwa uongozi wangu wa Yanga kwa kazi inayoendelea mpaka sasa kiukweli kwa kiasi fulani inaridhisha kuimarisha maeneo yaliyokua yanalega lega msimu uliopita. Lakini kuna jambo naona halijakaa sawa na hapo viongozi lazima tuwaambie mlipopuyanga.

Huyu Guede ambaye gari lake limewaka na kaanza kuzoeana na wachezaji wenzake alipaswa kupewa mkataba mpya na mzuri kuendeleza kile alichoanza nacho kwa nusu msimu aliokuwepo badala yake mnamuacha anaondoka na Skudu ambaye ni injury prone player bado yupo. Kiukweli sikutegemea kwa hili kutokea na nadhani mna haja ya kufanya kweli kuhakikisha Skudu aliyebaki ana deliver tulichotegemea kukiona.

Hongereni Singida mmepata mtu nafasi ya ushambuliaji.
Skudu ni kocha wa chenga na manjonjo Kwa wachezaji mazoezini
 
Back
Top Bottom