Mzee ES,
Nasikitika sana sikuwepo ktk mkutano huo na sababu kubwa ni kwamba sisi wenyewe hapa tulikuwa na kijimkutano chetu ktk kuanzisha upya jumuiya ya Watanzania.
Aliyosema Tausi ni habari zinazovuma North America na hakika hata mimi nimejaribu sana kupata habari hizi kwa kirefu lakini imekuwa shida. Vijana wengi naofahamiana nao hawakwenda. Habari za Bush kukutana na JK, kusema kweli nimeziona tu ktk magazeti ya Bongo. Sijaona hata artical moja toka gazetini, tovuti wala radio inayosema hivyo zaidi ya Dick na C. Rice.
Tausi,
Umezungumzia kuhusu Mkapa, sijui kama umesahau kwamba ni JK akiwa kama waziri wa mambo za nje ndiye alikuwa akijibu sana maswali ya Mkapa. Mkapa mwenyewe jeuri na mara nyingi alijiepusha hasa nchi za nje.
Kusema kweli Tausi nadhani mimi nitasikitishwa sana na nyie kwa sababu hamkujiandaa.. JK hawezi kujibu maswali ambayo hayakuulizwa. Rais yupo pale kusikia wewe matatizo yako na kuyawakilisha kwa wahusika! nadhani mlitakiwa kudondosha swala la Uraia wa nchi mbili...