Kwani hospitali ya Mlonganzila ipo wilaya gani pamoja na ile hospitali ya Palestina?

Kwani hospitali ya Mlonganzila ipo wilaya gani pamoja na ile hospitali ya Palestina?

Haijalishi ni umbali kiasi gani upo Kati ya ofisi za manispaa ya Ubungo na Hospital ya Mloganzila,kwa ufupi upande ule tu wa barabara ni wilaya ya Kisarawe na upande mwingine ni Ubungo, kwahyo hospital iko Kisarawe
Mie Niko upande wa hospital maeneo ya kibamba .tangu lini kibamba ikawa kisarawe
 
Ilala, Temeke na Mwananyamala ni hospitali xa rufaa.

Magomeni na Palestina ni za wilaya!
Nijuavyo na ndivyo ilivyo Magomeni na Sinza Palestina ni vituo vya afya yaani health centres na siyo hospitali. Moja ya changamoto zinazosababisha zisiwe elevated hadi kuwa hospitali ni ufinyu wa maeneo yake kwa sababu kuwa hospitali lazima kuwepo na huduma zingine za ziada ambazo zitahitaji nafasi ya kutosha ili kujenga jengo au majengo yatakayotumika kutoa huduma hizo.
 
Mloganzila ni ni tawi la Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. (Muhimbili National referral hospital)-
Inahudumia Wagonjwa wote Tanzania ingawa ipo kwenye Premises za Wilaya ya Ubungo.
Hospitali za Wilaya ni kwa ajili ya kuhudumia Wagonjwa wa Wilaya husika.
Kwa nini unasema Mloganzila ipo katika "premises" za wilaya ya Ubungo?
 
Palestina+ Mburahati ni Vituo vya Afya. Health centre.
Health centre ni Tofauti na Hospitali za Wilaya!! Kama Ilala, Temeke, Mwananyamala!!
Sijaelewa tofauti iliyopo kati ya hospitali ya wilaya na hospitali ya rufaa. Lakini pia hospitali ya Mwananyamala kwa sasa inajulikana kama hospitali ya rufaa na iko chini ya wizara ya afya tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo ilikuwa chini ya manispaa ya Kinondoni. Pia kwa taarifa niliyopata hivi karibuni kwa sasa manispaa hiyo ya Kinondoni wanajenga hospitali yao kubwa ya wilaya nadhani maeneo ya Mabwepande.
 
Palestina+ Mburahati ni Vituo vya Afya. Health centre.
Health centre ni Tofauti na Hospitali za Wilaya!! Kama Ilala, Temeke, Mwananyamala!!
Palestina ni DDH. Kinondoni. Ubungo ndio hamna.
 
Mheshimiwa. Mloganzila iko wilaya ya Kisarawe halafu sio hospitali ya wanyonge kama palestina au Mnyamala. Ukijipendekeza kumpeleka ndugu yako jiandae kuikimbia maiti. Kitanda kwa siku pale ni kuanzia Tsh 52, 000 per day. Ni zaidi ya gesti zote za Manzese. Hapo bado dawa na kuonwa na Dr. Unaruhusiwa kuchagua nesi atakayekuhudumia wewe tu usiku mzima. Kumbuka pale kila mgonjwa ana chumba chake full kipupwe.
 
Mimi Ni mndewa/mwenyeji pande hizo na Nina ardhi pande hizo toka 2005 na tano mauziano kila kitu yalifanyika na mihuri ya serikali ya huko inasoma kisarawe so usishangae mpaka hapo na ubungo Ni katikati ya barabara nielewe hivyo au check na traffic police wakupe ABC
Kisarawe[emoji15][emoji15][emoji15][emoji23][emoji23] we unaishi duni ya wap? Nadhan hata haujui Mloganzila ni nin ndg[emoji23][emoji23][emoji23] unajua ni umbali gan kutoka ofisi za manispaa ya ubungo kwenda Mloganzila?
 
Mheshimiwa. Mloganzila iko wilaya ya Kisarawe halafu sio hospitali ya wanyonge kama palestina au Mnyamala. Ukijipendekeza kumpeleka ndugu yako jiandae kuikimbia maiti. Kitanda kwa siku pale ni kuanzia Tsh 52, 000 per day. Ni zaidi ya gesti zote za Manzese. Hapo bado dawa na kuonwa na Dr. Unaruhusiwa kuchagua nesi atakayekuhudumia wewe tu usiku mzima. Kumbuka pale kila mgonjwa ana chumba chake full kipupwe.
Aga Khan kitanda laki mbili na nusu......hapo Mloganzila pana afadhali kumbe!
 
Back
Top Bottom