Kwani kinachoshindikana kulipa malimbikizo ya Watumishi wa Umma ni nini? Inaumiza sana

Kwani kinachoshindikana kulipa malimbikizo ya Watumishi wa Umma ni nini? Inaumiza sana

EZJ

Member
Joined
Jun 25, 2021
Posts
49
Reaction score
48
Siku chache zilizopita, Waziri wa Utumishi na Utawala Bora akiwa mkoani Kigoma, alijinasibu kuwa kuanzia tarehe 20/12/2021 yaani siku ya Jumatatu iliyopita wataanza kulipa malimbikizo ya watumishi. Cha kushangaza wamelipwa baadhi na wengine hatujalipwa.

Hivi kweli tokea Mei, 2019 mpaka sasa takribani miaka mitatu kinachoshindikana hasa nini kulipa stahiki zetu?

Wengine wanacheka, wengine tuna huzuni kuu.

Tafadhali sana Mh Rais na Mh Waziri wa Utumishi tunaomba kuwepo na usawa katika hili la kulipa stahiki za watumishi. Maana hakuna asiye na uhitaji.

Ni kama mnatugawa pasipo sababu za msingi. Ninawaomba mrekebishe hilo, sote tuneemeke na jasho letu tulilolitoa katika utumishi wetu.
 
Mfano, wilaya ya HAI tuliopandishwa mwezi Mei, 2019 kuna ambao walilipwa Malimbikizo yao mwaka jana 2020, wakati wa likizo ya korona.Wengine wamelipwa kwenye mshahara wa mwezi huu wa December, 2021. Sisi wengine bado tunasota tu.

Ulisema tupo 18,000 na Billion 30 zimetengwa kabisa kwa ajili ya kulipa malimbikizo. Sasa mbona walengwa hatuyaoni Mh Waziri? Au kuingiza taarifa kwenye mfumo ni kazi kubwa sana ukilinganisha na msoto ambao tunaoupitia tukisubiri stahiki zetu?

Tunaamini Mh Waziri wa Utumishi na Utawala bora ni kijana na ni mchapakazi. Nikushauri tu kuwa katika mazoezi nyeti kama haya ya ulipaji wa stahiki za watumishi, ikiwezekana muwe mnaongeza nguvu. Maana lengo linaweza likawa ni zuri sana, lakini utekelezaji wake ukaleta dosari ambazo zitachafua,au zitatia doa kabisa zoezi lote.

Naamini ushauri wangu utawafikia,na dosari mtazirekebisha.Ili na sisi tunufaike na jasho la Utumishi wetu!
 
Kumbukeni tu kuwa stahiki za watumishi,ni haki zao za msingi.kuzichelewesha pasipo sababu za msingi au kutokana na uzembe wa watendaji wachache kwa kweli inakera sana sana sana.Kama kweli fedha zipo na zimeidhinishwa kwa ajili ya kutulipa,tulipeni Basi.Maana mkumbuke malimbikizo sio hisani.Ni jasho na damu ya mtu iliyopunjwa.
 
Hivi wanalipa na interest kwa muda wote huo waliokaa na fedha ya mtu?
 
Naimani taarifa hii imewafikia walengwa.Na wataitendea haki.Maana vitu vingine ni aibu.Wengine wameshasahau,sisi tunasubiri zaidi ya miaka mitatu kweli????Mh Mchengerwa ,hii wizara yako ya Utumishi na utawala bora .Hebu iongezee spidi kwa watendaji wako.Tunajua una nia na malengo mazuri sana kwa watumishi wa umma.Ila nadhani kuna watendaji wako wanakuangusha.Ukiona haya yanasemwa,yafanyie kazi.Maana sio majungu,bali ndio hali halisi ya sisi watumishi ambao tumecheleweshewa sana stahiki zetu,ambapo wengine wamelipwa.MH HAKUNA ASIE NA UHITAJI,UKIZINGATIA NI HAKI YAKE!
 
Hivi wanalipa na interest kwa muda wote huo waliokaa na fedha ya mtu?
Hakuna cha interest mkuu.Hebu fikiria kuna waliolipwa wakati wa likizo ya Corona,kuna ambao wamelipwa December hii 2021.Sisi bado ,tunasota.Na tulipandishwa pamoja.Hii haishushi ufanisi wa kazi?????
 
Back
Top Bottom