Kwani mtoto chini ya mwezi mmoja huwa analia sana

Chukua kitunguu saumu saga kidogo sana weka na maji kidogo kisha mpake kwenye paji la uso kifuani tumboni na viganjani
Pia waweza kutumia hata chumvi kwa mbali lakini kwenye maji yake ya kuoga

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii ni dose ya siku ngapi? Au ni once for good? Imeshaleta matokeo mazuri ambayo umejiridhisha tunaweza tumia option hii kiongozi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama swali liliulizwa sababu ni nyingi na zinatofautiana Mtoto na Mtoto.
Ila kuna zile ambazo zinajulikana kwa wengi.
1. Mtoto analia sababu ana njaa
2. Mtoto analia sababu anajisikia tu kulia.[emoji6]
3. Mtoto analia sababu anahitaji kubadilishwa nepi.
4. Mtoto analia sababu hajiskii vizuri, pengine anaumwa /maumivu
5. Mtoto analia sababu amechoka anahitaji Kulala.
6. Mtoto analia sababu anataka kubebwa.
7. Mtoto analia sababu anasikia joto au baridi.

Kama yote hayo hayamuhusu basi mwache alie akichoka atalala, jinsi anavyozidi kukua atapunguza nakuacha kabisa.
 
Sababu kuu ni njaa.
Zingine ni;
kuwa uncomfortable labda dipers ziko mbichi, position aliyopo, kutokujisikia vizuri, kutaka kubeua( hapa mfano akianza kulia baada ya kunyonya).
Na pia ukimzoea mtoto wako vizuri kabla hajaannza kulia kuna viashiria tofauti anavionyesha physically ktk uso au sehemu zingine za mwili. Mfano kukunja sura, kuweka mikono mdomoni, au ukimgusa tu mdomoni anafungua mdomo,
Ila sababu kubwa ni njaa, mtoto ana tumbo dogo hivyo hata intervals zake za ulaji ni tofauti na mtu mzima!
Ushauri: mama kula vyakula sahihi ili umnyonyeshe mwanao maana maziwa yako ndo kila kitu kwa afya yake, na wababa walisheni wazazi wenzenu inavyotakiwa!
 
Spot on!
 
Gas inatoka kwa njia ya kujamba, sijaelewa ni njia ipi mbadala ya kumtowa mtoto gesi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama mtoto anamyonya maziwa ya chupa huwa anavuta ndani na hewa inayojaa tumboni, akisha kunywa maziwa haya mbeulishe ka kumuweka tumbo behani kwako alafu unampiga piga kidogo taratibu mgongoni kwake mpaka abeue, kubeua ni njia moja wapo ya kutoa gesi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…