Kwani Wakulima waliikosea nini Serikali ya CCM?

Kwani Wakulima waliikosea nini Serikali ya CCM?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Nilimsikia waziri wa fedha akisema, kwa ajili ya kukuza kilimo cha umwagiliaji vikundi vya skimu za umwagiliaji, vitatozwa ada ya kuendeleza miradi ya umwagiliaji.

Hivi ni kweli kwamba serikali imeshindwa kubuni mbinu za kuwatafutia ruzuku wakulima wetu hata kwa kukopa toka mabenki mbalimbali?

Ni nani kwenye nchi hii asiyejua madhira wanayopata wakulima wetu ikiwemo kukosa uhakika wa masoko ya mazao yao, achilia mbali uzalishaji wenye tija ndogo.

Kwa maoni yangu nilidhani kilimo ni sekta inayohitaji kulelewa na serikali ili izidi kutoa ajira kwa wananchi kuliko kuwaongezea kongwa la ada za kuendeleza skimu za umwagiliaji.
 
Halafu mnashangaa kwanini machinga wamezagaa kila mahali hadi juu ya mitaro ya maji taka mijini? Kwa sera hizi nani atabaki vijijini? Labda vikongwe; ila vijana sahau!

Tutaijaza miji na itajaa kweli kweli; tutaziba mabarabara na mitaa kwa kila linalowezekana - machinga, bodaboda, bajaj, etc. Kwa ufupi, sera za CCM zimefeli!
 
Waziri wa fedha amesoma bajeti na tunaendelea kuichambua kipengele kimoja baada ya kingine. Kwa ufupi ni kwamba wanasiasa wameshindwa kutatua changamoto zetu.

Wakati taifa likiwa katika mtanzuko mkubwa wa ajira na kuhimiza vijana wetu waegemee zaidi kilimo hasa cha umwagiliaji, Serikali imeamua kuwavunja moyo kwa kuongeza kodi katika uanzishwaji wa vikundi vya umwagiliaji. Je, tuendelee kuwaamini hawa akili ndogo katika kutuongoza?

cc Mwigulu Nchemba
 
Kwa hili la umwagiliaji mama amekwenda kinyume na dhamira ya jpm ya kuinua kilimo cha umwagiliaji
Yule katili hata usimtaje unachafua hali ya hewa.

Kwanza wameweka hiyo tozo Ili kufanya scheme zijiendeshe kama mamlaka za maji
 
Hivi jpm ni nani nchi ifuate aliyokuwa anataka yeye jpm alifanya yake mwacheni mama afanye jpm jpm mnatuchosha na jpm wenu huyo si mmufuate huko aliko.
Natambua kuna mabaya na mazuri ya jpm. Katika mazuri hili ni mojawapo kama wewe ni mkulima wa umwagiliaji utakuwa umenielewa, kipindi cha nyuma ilikuwa unakutana na vikwazo lukuki kupata kibali wakati bodi ipo wizara ya maji.

Niliandika comment ndefu kufafanua transformation yote bahati mbaya imejirefresh na kufutika
 
CCM inawabamiza wakulima kama punching bag yaani.
giphy.gif


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom