Kwani Wakulima waliikosea nini Serikali ya CCM?

Kwani Wakulima waliikosea nini Serikali ya CCM?

Natambua kuna mabaya na mazuri ya jpm. Katika mazuri hili ni mojawapo kama wewe ni mkulima wa umwagiliaji utakuwa umenielewa, kipindi cha nyuma ilikuwa unakutana na vikwazo lukuki kupata kibali wakati bodi ipo wizara ya maji, . Niliandika comment ndefu kufafanua transformation yote bahati mbaya imejirefresh na kufutika
Mkuu kwanza heshima kwako umenijibu kwa hekima sana unafaa kuwa kiongozi shukrani kwa busara uliyoinyesha kwa jibu lako
 
Nilimsikia waziri wa fedha akisema, kwa ajili ya kukuza kilimo cha umwagiliaji vikundi vya skimu za umwagiliaji, vitatozwa ada ya kuendeleza miradi ya umwagiliaji.

Hivi ni kweli kwamba serikali imeshindwa kubuni mbinu za kuwatafutia ruzuku wakulima wetu hata kwa kukopa toka mabenki mbalimbali?

Ni nani kwenye nchi hii asiyejua madhira wanayopata wakulima wetu ikiwemo kukosa uhakika wa masoko ya mazao yao, achilia mbali uzalishaji wenye tija ndogo.

Kwa maoni yangu nilidhani kilimo ni sekta inayohitaji kulelewa na serikali ili izidi kutoa ajira kwa wananchi kuliko kuwaongezea kongwa la ada za kuendeleza skimu za umwagiliaji.
CCM OYEEEEEE ... !!! Nchi zote zinazo jitambua kilimo cha umwagiliaji hupata ruzuku ili kuukomaza uti wa mgongo wa taifa hili

Lakini wenzetu wanataka viwanda basi haya toeni ruzuku ya viwanda au ndio tutashia kwenye viwanda vya kushona viatu ... yani CCM ni chama cha kizamani sana ase!
 
Waziri wa pesa ni mwigulu unategemea nini hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii wizara ilitakiwa apewe mtaalam aliyebobea kwenye masuala ya uchumi kama ilivyokuwa kwa Philipo Mpango! Ila siyo Mwigulu Nchemba mzee wa TOZO!

Huyu angepelekwa Wizara ya Muungano na mazingira akapige porojo na mwenzake Jaffo.
 
Hivi jpm ni nani nchi ifuate aliyokuwa anataka yeye jpm alifanya yake mwacheni mama afanye jpm jpm mnatuchosha na jpm wenu huyo si mmufuate huko aliko.
Huu ndo upumbavu kuleta ushabiki hata kwenye Mambo yenye maslahi kwa taifa kwaio Kama budget imembana mkulima watu wasiseme wamwache wakati wanaumia angekua nchi ni Mali yake angeachwa afanye anavyotaka.hata uyo jpm alikua anaambiwa hapa JF akienda sivyo.
 
Huu ndo upumbavu kuleta ushabiki hata kwenye Mambo yenye maslahi kwa taifa kwaio Kama budget imembana mkulima watu wasiseme wamwache wakati wanaumia angekua nchi ni Mali yake angeachwa afanye anavyotaka.hata uyo jpm alikua anaambiwa hapa JF akienda sivyo.
Huyo jpm wako alikuwa na muda kukusikiliza acha upumbavu na jpm wako
 
Budget hii ya Waziri Wa Fedha imeweka dhahiri kwamba:

1) Dk Mwigulu haiwezi hio Wizara, na anageuka kuwa mzigo kwenye serikali ya SSH.

2) Waziri Wa Kilimo na Naibu Waziri wake sasa ni maadui wakubwa wa wakulima nchini.

Moja, huwezi kuruhusu upumbavu huu kufanyika kwenye wizara yako ya kilimo wakati wakulima bado hawajajiweza wala hawajaingia kwenye kilimo cha kisasa.

Pili, wakulima hawana mtaji na hawana masoko ya mazao yao wanayolima.

Tatu, swala la kilimo cha umwagiliaji kwanza lingepewa kipaumbele ili wakulima wengi waingie kwenye sekta hio ya kilimo cha umwagiliaji.

Nne, ahadi za CCM za uchaguzi mkuu 2015 zilikua kuongeza idadi za hekta katika kilimo cha umwagiliaji (Jambo ambalo hawakuweza kufanya, hawakuongeza hata ekari 1 ya kilimo cha umwagiliaji, kwasababu walikua bussy kununua ndege na treni).

Tano, nchi haijaweza kujikwamua kwenye kilimo na haijaweza kuzalisha chakula cha kutosha na chakula cha ziada (Yaani kufikia mahitaji ya chakula kinacho hitajika).

Sita, viongozi wanaangalia matumbo yao, na kukalia upuuzi uliopitiliza kwenye kuliongoza taifa katika sekta ya kilimo.

#WAZIRI WA FEDHA, WAZIRI WA KILIMO & NAIBU WAZIRI WA KILIMO - WAENDE WAO WAKASHIKE MAJEMBE NA WAKALIME HALAFU WALIPE HIZO KODI, NDIO WAJE KUTUPA MREJESHO KAMA KUNA FAIDA WATAPATA HUKO.
 
Kwa hili la umwagiliaji mama amekwenda kinyume na dhamira ya jpm ya kuinua kilimo cha umwagiliaji
Rais anaongoza kwa dhamira yake mwenyewe haongozi wala kushawishika kuongoza kwa dhamira ya marehemu.

Acheni ujinga wenu
 
CCM ilipotwaliwa na matajiri jumla kutoka kwa wakulima kupitia mabadiliko ya katiba.
Vijana nendeni mkazurure mjini mkichuuza 'made in China', kilimo kimeonekana kama kazi ya laana.
Hata viongozi wakiwa majukwaani hujitapata kuwatetea bodaboda, machinga na mama ntilie.
 
Back
Top Bottom