Kwanini 90% ya Maafisa wa Vyeo vya Juu wa JWTZ Wakistaafu Ugonjwa wao mkubwa huwa ni 'Stroke: tu?

Kwanini 90% ya Maafisa wa Vyeo vya Juu wa JWTZ Wakistaafu Ugonjwa wao mkubwa huwa ni 'Stroke: tu?

Mtu yeyote asiyejali afya ( lishe Bora, mazoezi na utulivu kifikra ) hupelekea matatizo kiafya na magonjwa.

Jamani ukifika umri wa miaka 30s jidhatiti kujali afya na kuacha tabia zinahatarisha afya Yako

1. Punguza unywaji pombe
2. Fanya mazoezi
3. Zingatia lishe Bora
4. Epuka stress
5. Jishughulishe na kazi nyepesi
 
Tafadhali naomba huu Uzi uwe na Mjadala wenye Mantiki kwa Faida ya Wengi kwani kwa Utafiti wangu GENTAMYCINE nikienda Kuona Wagonjwa Lugalo Military General Hospital na hata Majumbani / Mitaani 90% ya Wagonjwa wa Kiharusi ( mliosoma mnauita Stroke ) huwa ni Wanajeshi Wastaafu ( tena waliokuwa na Vyeo Vikubwa ) kabisa.

Nini hasa hupelekea hali hii? Bujibuji Simba Nyamaume katika Mitaa yako ya Mbezi Beach ( hasa usawa wa Kona Baa ) nyuma ya Nyumba ya Marehemu Mzee Kitundu kuna. Wajeda Watatu ( Wastaafu wa Vyeo vya Juu. ) wote wana 'Stroke' na Nyumba zao ziko jirani jirani tafadhali kuanzia Saa 11 sema utakuwa wapi nikupitie ili tukawasalimu kwani Walifanya Kazi Kubwa sana katika Kumtia Adabu Nduli Idi Amini Dada.

Nichukue nafasi hii kuwapa Pole nyingi mno wale wana JamiiForums wote Wanaouguza Wazazi wenye hili tatizo la Kiharusi ( Stroke ) ambalo GENTAMYCINE naona ni kama vile limeachwa tu wakati naliona kwa sasa ndiyo limeshika Kasi na linatishia sana.

Mwenyezi Mungu awapiganie Wagonjwa wote wa Stroke ( Kiharusi ) na awatie Nguvu na awape Uvumilivu na Ujasiri wale Watu ( Wanafamilia ) wote Wanaowauguza Mahospitalini na Majumbani.
Uongo mtupu hamna kitu kama hicho
 
Back
Top Bottom