Kwanini Ali Kiba hapati offer za matangazo ya makampuni makubwa kama Diamond Platnumz?

mtotomtamuu

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2016
Posts
602
Reaction score
1,459
Nnje ya mziki biashara ya matangazo kwa makampuni makubwa imekuwa inalipa wasanii wengi na hivi majuzi Diamond amevuta mkwanja wa Billioni 1 kukitangaza kinywaji cha ufaransa cha Bllaire

Lakini king kiba hapati offer za matangazo makubwa kwa nini?

Hana mvuto au hana management nzuri inayomuunganisha na makampuni?

Na kama hataki pesa ndogo kutoka kwa makampuni kwa nini bado anapiga show za bei raisi za fiesta na zile za vichochoroni za club za ulaya?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
diamond maisha yake kama movie... ni brand tayari... hapo anambeba zari, tiffa na nilan kwenye tangazo... so wanaempa tangazo wanajua hela itarudi tu
 
mbona anapiga matangazo sana tuu,kama ni muangaliaji mzuri wa TV jaribu kuangalia clouds anaonekana sana kwenye matangazo ya fiesta,kuna moja wameenda kweny shule flan ya wasichana Arusha.
Dah jf kwel nikiboko
 
Duuh huwezi kujua labda ni uamuzi wake na management yake
 
Show off ndizo zinazompa matangazo (DSTV, COCA, UBBER, REDGOLD TOMATO, VODA) na watu wa marketing ndio wanapenda hizo show off, kwani ndizo zinatangaza bidhaa. We angalia diamond karanga zinavyolika, mtaani vipaketi vyake vishakuwa kama uchafu kwani zinanunulika sana. Mwisho mondi anajua Branding na hamna msanii anayemkaribia hata robo upande wa branding.
 
Kwani wanamuziki hala tz ni diamond na kingkiba tu. Hebu jiongeze wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…