Kwanini asisifiwe Mwananchi anayelipa kodi inayotekeleza miradi ya kitaifa?

Kwanini asisifiwe Mwananchi anayelipa kodi inayotekeleza miradi ya kitaifa?

Umejengwa utamaduni wa ajabu kwa kutoa Sifa kwa viongozi wa kisiasa wanaposimamia utekelezwaji wa miradi ya kitaifa, na kusahaulika Mwananchi ambaye ndiye aliyemwaga jasho kutafuta pesa na kuipa kodi kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.

Sifa hizo kwa sasa zimeenda mbali zaidi kusifia hata pale ambapo wanasiasa hao hawajahusika hata katika usimamizi jambo lolote ila sifa hupelekwa kwao kuwa wamefanya jambo hilo kutokea.

Huo ni utamaduni usiofaa kwani ni mbinu ya kuwalazimisha watu kuona mazuri hata yasioyokuwepo na kuwafanya watu wasione udhaifu wa viongozi hao kisiasa.

Mbaya zaidi kumezuka hata tabia ya kuweka sherehe za kuwapongeza viongozi eti kwa kutekeleza miradi, katika sherehe hizo hutumia tena pesa za walipa kodi japo sherehe nyingi hufichwa kwenye jina la uzinduzi ambapo unakuta gharama ya uzinduzi inaweza kukaribia gharama ya mdari husika!
Duh
 
Sawa unalazimishwa na haubembelezwi.

Mantiki ya mtoa hoja hapa ni nani anayezistahili kupewa sifa za pesa zilizopatikana kwa nja ya kodi?

Kwani mtu akitimiza kazi zake vizuri iwe kwaku tumwa ama kujituma, hastahili pongezi?

Je pongezi zinastahili kupewa watu wenye sifa zipi?
Shida hapa ni elimu ya kodi,kodi ni ya serikali .Utapogezwa kwa lipi wakati kitu sio chako,neno kodi mmiliki ni serikali ndio maana inapongezwa kwa kutumia pesa zake vizuri.Wewe ukitumia pesa zako vizuri tutakupongeza ,chanzo chako cha mapato ni mjadala mwingine ,ukijenga nyumba sifa ni kwa taasisi iliyokulipa au tunakusifia wewe?Hakuna mwananchi mmiliki wa kodi .Mwananchi ni chanzo kimoja kati ya vingi vya kodi ,serikali ianze kupongeza vyanzo vyote vya kodi zikiwemo taasisi zake maana zinalipa kodi ndio mnataka tuende kwa mfumo huu.Yaani wewe ukilipa ada ya watoto wako tunaipongeza biashara yako au kazi yako iliyokuletea kipato.Elimu ya kodi bado sana nchi hii.
 
Binafsi naunga Mkono kuwa fedha hizo ni Kodi za wananchi lakini kumpongeza kiongozi kwa kusimamia fedha hizo na kufanikisha miradi yenye ubora tarajiwa ni jambo zuri pia ilimradi haligharimu sana, ikumbukwe viongozi hao wanauwezo wa kutotekeleza kwa ufasaha kazi zao na kusababisha huduma mbovu kwa wananchi. Hivyo kiwapongeza kunawaongezea moyo wa kuona wanaotutumikia tunathamini kazi zao ikumbukwe wao pia wanalipa Kodi na ni wananchi pia.
 
Kitu unacholalamikia ni ujinga.Vitani Huwa hawasifiwi askari woote Bali Kiongozi wao tena Kwa jina,Je Huwa Yuko stari wa mbele wa vita? Jibu ni hapana.

So ukielewa scenario hiyo basi huwezi shangaa Rais kusifiwa.Jielimishe badala ya kuandika maelezo mengi yasiyo na msingi.
Hilo la kusifia Rais ni issue nyingine ambayo tungeifikia mwisho wake bila shida na kilichokuwa kinatafutwa ni point ya kumhalalishia sifa hizo.

Shida iliyopo katika hoja yangu kwako ni ile tabia yako ya kutumia naneno ovu katika mjadala.

Hauwezi mwambia mtu usiyemfahamu kuwa ni 'mjinga', 'mwivu' sijui 'mpumbafu' katikati ya mjadala, wakati ukielewa wazi kuwa maneno hayo ni matusi.

Kwani tunayojadili humu tunalipwa ama kulazimishwa na mtu?

Mi nadhani ni kwa ajili ya kutupatia furaha na kupatuana mawazo!
Sasa yote hayo utayapata kati kati ya matusi!
 
Hi

Hilo la kusifia Rais ni issue nyingine ambayo tungeifikia mwisho wake bila shida na kilichokuwa kinatafutwa ni point ya kumhalalishia sifa hizo.

Shida iliyopo katika hoja yangu kwako ni ile tabia yako ya kutumia naneno ovu katika mjadala.

Hauwezi mwambia mtu usiyemfahamu kuwa ni 'mjinga', 'mwivu' sijui 'mpumbafu' katikati ya mjadala, wakati ukielewa wazi kuwa maneno hayo ni matusi.

Kwani tunayojadili humu tunalipwa ama kulazimishwa na mtu?

Mi nadhani ni kwa ajili ya kutupatia furaha na kupatuana mawazo!
Sasa yote hayo utayapata kati kati ya matusi!
Ulienda shule wewe kweli? Ili mtu awe mjinga inahitaji kumfahamu au tunaangalia unachoandika ndio tuna draw conclusion? Ujinga ni kutokuwa na ufahamu wa jambo
 
Inapendeza ikiwa ... jengo hili ni kwa Hisani ya Kodi za Wananchi wa JMT
 
Shida hapa ni elimu ya kodi,kodi ni ya serikali .Utapogezwa kwa lipi wakati kitu sio chako,neno kodi mmiliki ni serikali ndio maana inapongezwa kwa kutumia pesa zake vizuri.Wewe ukitumia pesa zako vizuri tutakupongeza ,chanzo chako cha mapato ni mjadala mwingine ,ukijenga nyumba sifa ni kwa taasisi iliyokulipa au tunakusifia wewe?Hakuna mwananchi mmiliki wa kodi .Mwananchi ni chanzo kimoja kati ya vingi vya kodi ,serikali ianze kupongeza vyanzo vyote vya kodi zikiwemo taasisi zake maana zinalipa kodi ndio mnataka tuende kwa mfumo huu.Yaani wewe ukilipa ada ya watoto wako tunaipongeza biashara yako au kazi yako iliyokuletea kipato.Elimu ya kodi bado sana nchi hii.
Mkuu mi nimefurahishwa sana na andiko lako.

Sisi tangu Magufuli tuliipenda kasi ya ufanyaji wa Serikali hasa kwa nyanja za kimaendeleo.

Ila hapa kuna hoja ya msingi hasa linapokuja suala la upindishaji wa lugha sahihi inayopotoshwa kwa makusudi.
Hivi kusema 'mheshimiwa Rais katoa pesa', tena kwa kutaja jina lake halisi, yaani majina yake yote kana kwamba kuna raia asiyemfahamu, unaiona ni sahihi kweli?

Embu tumalizane na hili kwanza nikitumaini uliyoyaongea mengine yapo sahihi.
 
Mkuu mi nimefurahishwa sana na andiko lako.

Sisi tangu Magufuli tuliipenda kasi ya ufanyaji wa Serikali hasa kwa nyanja za kimaendeleo.

Ila hapa kuna hoja ya msingi hasa linapokuja suala la upindishaji wa lugha sahihi inayopotoshwa kwa makusudi.
Hivi kusema 'mheshimiwa Rais katoa pesa', tena kwa kutaja jina lake halisi, yaani majina yake yote kana kwamba kuna raia asiyemfahamu, unaiona ni sahihi kweli?

Embu tumalizane na hili kwanza nikitumaini uliyoyaongea mengine yapo sahihi
Kuna miradi ipo na imepitishwa kwenye budget lakini pesa ya kutekeleza haipo ,sasa Rais anaweza kutumia mamlaka yake kulazimisha utekelezaji wa mradi huo,pesa zinatoka wapi watendaji mtaumiza vichwa .Huu ni mfano mmoja ambapo Rais anapongezwa .Mfano wa pili chadema walikataa kupokea ruzuku miaka 3 ,kila mwaka bilioni 1 ,sasa kwa mwaka wa kwanza hiyo pesa ilipangiwa matumizi mengine serikali haiwezi kuangalia pesa tu mambo ni mengi ,mwaka wa pili hivyohivyo ,mwaka wa tatu maridhiano yanafanyika chadema wanaweka masharti kulipwa ruzuku miaka mitatu,mlipaji wa serikali anasema hiyo pesa haipo ,Rais anasema walipwe mtajua itatoka wapi ,japo ni haki yako kulipwa mazingira ya kulipwa yanafanya umpogeze Rais kwa kutaja jina la babu yake.Vinginevyo ingekuwa madai ya miaka nenda rudi.
 
Hii imekuwa kawaida sana katika nchi yetu lakini lengo na madhumuni ya kumsifia kiongozi hata kama anafanya mabaya ni yeye aonekane anafanya vizuri kwa wananchi na pia watoa sifa pia wao wanaangalia promotion ya vyeo kwa nchi yetu hii imekuwa ni kama propaganda ya watu flani ili kufanikisha jambo lao.
 
Kimsingi kwa katiba mbovu ukishalipa kodi hiyo Hela siyako Bali ya rais nayeye anaamua afanyie Nini!!!
 
Kumsifia mtu ambaye hatoi hata 💯 kutoka mfukoni mwake kufanikisha hiyo miradi; nadhani ni uwendawazimu wa kiwango cha juu sana.
 
Una point konki, lakini umeuzunguka mno mbuyu.

Nikuambie tu kwamba unachokijua ama usichokijua, hii tabia ya uchawa pamoja na kujifyetua akili hata kwa watu waheshimiwa kabisa katika jamii ni ajira inayowalipa sana wao kwa kushibisha matumbo yao.

Ni ubinafsi na uzandiki kwa uzalendo wa Taifa kwa mheshimiwa kama Waziri, Rc, Dc ama Mbunge kusimama hadharani na kusema kwa mfano: ... 'Mama katoa pesa kujenga kipande cha barabara kutoka point 'A' kwenda point 'B' na maneno mengine yenye kufanana na hayo wakati wakijua kabisa kuwa ni ya uongo mtupu.

Rais ni muajiriwa wa wananchi, ni kiongozi wa utekelezaji wa maamuzi ya Taifa, analipwa kwa kazi hiyo kama mwajiriwa yeyote mwingine wa Serikali na hana pesa hata senti 5 kuweza kuitoa mfukoni mwake kutekelezea mradi wowote hata wa kujenga choo cha shimo cha shule.

Walishaona kwamba kumsifia Rais kwa maneno ya uzandiki na unafiki wa uongo ni kumuenzi na kumfurahisha yeye ili kumfubaza mawazo yake, asiweze kuziona dosari zake katika uongozi wake na asiweze kuona watu wengine wenye sifa bobezi zenye kufaa kuweza kulitumikia taifa, kwamba wao ndiyo watu bora na wapo karibu na mama.

Na kama wako mbali, basi kwa kupaza sauti zao za kusifia, wataonekana na kusogezwa.

Kwa hiyo kama kuukemea huu uozo, tuukemee bila ya kumumunya maneno.

Kwani kumsifia Rais kwa sifa za kweli zenye kuonekana katika utekelezaji wa majukumu yake kuna ubaya gani?

Basi mwenye kusifia, akae chini achambue sifa stahiki anazopaswa kumpa kiongozi husika na siyo kumtengenezea sifa za uongo wa mchana kweupe zisizomstahili kupewa.

Na huo utaratibu mbovu kwa matumizi ya fedha za Serikali, ndiyo athari za matokeo ya mambo tunayoyaongelea sasa.

Hiyo syndicate ya wazandiki na mafisadi, hakuna anayeweza kuwakemea katika ubadhirifu wao huo kwa sababu mwenye uwezo wa kufungua kinywa na kukaripia ili kukomesha ndiye kapigwa nusu kaputi la usingizi wa sifa, kwa hiyo hawezi kuona madhila yoyote ambayo taifa linapitia kutokana na matumizi mabaya ya fedha za umma.
Umesema kweli mkuu hawa machawa wanafikiri kwa kutumia matumbo badala ya vichwa
 
Umejengwa utamaduni wa ajabu kwa kutoa Sifa kwa viongozi wa kisiasa wanaposimamia utekelezwaji wa miradi ya kitaifa, na kusahaulika Mwananchi ambaye ndiye aliyemwaga jasho kutafuta pesa na kuipa kodi kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.

Sifa hizo kwa sasa zimeenda mbali zaidi kusifia hata pale ambapo wanasiasa hao hawajahusika hata katika usimamizi jambo lolote ila sifa hupelekwa kwao kuwa wamefanya jambo hilo kutokea.

Huo ni utamaduni usiofaa kwani ni mbinu ya kuwalazimisha watu kuona mazuri hata yasioyokuwepo na kuwafanya watu wasione udhaifu wa viongozi hao kisiasa.

Mbaya zaidi kumezuka hata tabia ya kuweka sherehe za kuwapongeza viongozi eti kwa kutekeleza miradi, katika sherehe hizo hutumia tena pesa za walipa kodi japo sherehe nyingi hufichwa kwenye jina la uzinduzi ambapo unakuta gharama ya uzinduzi inaweza kukaribia gharama ya mdari husika!
Kiongozi anapewa sifa kutokana na jukumu alilonalo kikatiba la usimamizi wa Kodi zetu. Na inapotokea mambo yameenda vibaya wa kwanza kulaumiwa huwa ni kiongozi na huwa tunamlaumu kwa sababu ya kushindwa majukumu yake ya usimamizi wa Kodi zetu.
 
Vile anavyopewa sifa mbaya kutokana na matendo ya Wananchi wake na ndivyo anavyopewa sifa mzuri pale anaposimamia vyema fedha za Wananchi wake.
Mfano ukitokea ukame Wananchi wakashindwa kuzalisha chakula na wengi wakafa basi atalaumiwa kwa kutochukua hatua Ili kuokoa wananchi wake. Ataitwa mzembe!


Anyway mnapata shida kubadilisha asili ya uongozi na kike kinachoitwa mafanikio au utendaji kazi wa kiongozi.
 
Umejengwa utamaduni wa ajabu kwa kutoa Sifa kwa viongozi wa kisiasa wanaposimamia utekelezwaji wa miradi ya kitaifa, na kusahaulika Mwananchi ambaye ndiye aliyemwaga jasho kutafuta pesa na kuipa kodi kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.

Sifa hizo kwa sasa zimeenda mbali zaidi kusifia hata pale ambapo wanasiasa hao hawajahusika hata katika usimamizi jambo lolote ila sifa hupelekwa kwao kuwa wamefanya jambo hilo kutokea.

Huo ni utamaduni usiofaa kwani ni mbinu ya kuwalazimisha watu kuona mazuri hata yasioyokuwepo na kuwafanya watu wasione udhaifu wa viongozi hao kisiasa.

Mbaya zaidi kumezuka hata tabia ya kuweka sherehe za kuwapongeza viongozi eti kwa kutekeleza miradi, katika sherehe hizo hutumia tena pesa za walipa kodi japo sherehe nyingi hufichwa kwenye jina la uzinduzi ambapo unakuta gharama ya uzinduzi inaweza kukaribia gharama ya mdari husika!
MIMI NAKATWA 1.1 MIILLION PER MONTH SIJAWAHI SIFIWA HATA SIKU MOJA .DAAAAH
 
Kiongozi anapewa sifa kutokana na jukumu alilonalo kikatiba la usimamizi wa Kodi zetu. Na inapotokea mambo yameenda vibaya wa kwanza kulaumiwa huwa ni kiongozi na huwa tunamlaumu kwa sababu ya kushindwa majukumu yake ya usimamizi wa Kodi zetu.
Kodi zenyewe wanaiba tu.hivi hatuwezi kuwa tunawafanyia APPRAISAL viongozi wetu?
 
Back
Top Bottom