maufoungph
Member
- Oct 16, 2018
- 73
- 164
Tatizo wazazi wa kiAfrika wengi akianza kuona unataka kuwa karibu na biashara yake/zake hata kama kujifunza tu mbinu mbalimbali, anaanza kuhisi unatafuta slope ya maisha ya kuusakaa urithi mapema, hivyo wanatukata stimu sana.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni shida sana kwakweli.Naunga mkono hoja hili Jambo lipo kwenye familia yetu
Habari ya wakati huu?
Naomba kwenda kwenye mada moja kwa moja.
Kwanini biashara nyingi za watanzania zinayumba hadi kufa pindi baba au kiongozi wa familia anapofariki?
Mambo ni tofauti kwa upande wa wafanyabiashara wenye asili ya Asia. Anakufa baba au kiongozi wa familia, mtu mwingine anarithi usimamizi wa biashara na mambo yanakua kama zamani au mambo yanakua bora zaidi ya zamani.
Nashindwa kuelewa ni kwanini sie tunashindwa kuendeleza biashara wakati wenzetu mambo yanaenda kama kawaida.
Mfano kampuni nyingi za Asia utakuta "Since 1960" hadi muda huu unakuta kampuni inadunda.
Nakaribisha mjadala ili tujue ni wapi tunakwama.
Hii nmeishuhudia kwenye biashara za familia kadhaa.Kwanini biashara zinakufa moja ya sababu kukuu ni ukosefu wa elimu ya biashara,kama kampuni ipo chini ya sheria na ina strong managemnt basi haitaki nguvu kubwa kuendesha biashara hiyo maana amekufa mtu na sio kampuni.
Ila kuna sababu ndogo ndgo znapelekea kufa kwa biashara ni pale ndugu wanapoitaji mirathi wanakuwa tayari kuthaminsha mali za kampuni na hata pesa yakuendeshea biashara iyo..
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli kabisa mkuu. Familia zetu nyingi kila mtu anajifikiria yeye binafsi na sio familia.Watoto wengi hawaandaliwi kuongoza biashara za familia. Labda ni ukosefu wa kuaminiana kwenye familia.
Ni muhimu sana kuwaandaa watoto kwenye biashara za familia. Wazazi wanatakiwa wajue siku itafika umri utakataa kuendana na pirika za kuendesha biashara. Kwahio ni muhimu kuwapa muongozo mapema hili wakikosea warekebishwe kuliko kuwaachia peke yao hapo mbeleni bila maandalizi.
Hivi kibongo bongo hili linawezekana kweli?Ishu kubwa niliyoiona ni kuwa wenzetu ni wafanyabiashara na wanafuata principle za kibiashara mtoto anazaliwa ktk biashara, anaishi ktk biashara, anarithi biashara na kuendeleza biashara. Wahindi huwarithisha watoto biashara mapema na kunakuwa na uwazi yaani inakuwa biashara ya kifamilia.
Tofauti na kwetu sisi biashara ni ya mtu mmoja tu wengine kazi yao ni kula kile wasichojua kinatoka wapi ni nadra sana kwa ngozi nyeusi biashara yake kuwa wazi kwa familia nzima na kuendeshwa kifamilia. Wenzetu utakuta baba ni mkurugenzi au cheo chochote cha u-CEO theni chini yake ni mwanae au ndugu mwingine wa damu.
Kifupi wenzetu biashara ni ya familia nzima na pia kwao ndo urithi kama ambavyo sisi hurithishana uganga, mashamba, uchawi nk na anayerithi huendeleza basi wao biashara ndo tunguli zao za kurithishana.
Sent using Jamii Forums mobile app
...Labda awe amekushirikisha katika kujua namna ya hata alivyoupata...Kuzika Kondoo...kulala juu ya Kaburi Usiku kucha...nk! ...ukimrithisha na haya, biashara inaweza ikadumu hata Wewe Mwenyewe Ukitangulia Kufa!![emoji16][emoji16][emoji16]Marehemu huondoka na MALI ZAKE..
Mzee mwenyewe ndo anajua siri za utajiri wake ni ngumu kuuendeleza utajiri aliokuachia mtu.
Wachache wanaweza.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hata uangalizi wa maboma magari msimamo wa familia n.k.Habari ya wakati huu?
Naomba kwenda kwenye mada moja kwa moja.
Kwanini biashara nyingi za watanzania zinayumba hadi kufa pindi baba au kiongozi wa familia anapofariki?
Mambo ni tofauti kwa upande wa wafanyabiashara wenye asili ya Asia. Anakufa baba au kiongozi wa familia, mtu mwingine anarithi usimamizi wa biashara na mambo yanakua kama zamani au mambo yanakua bora zaidi ya zamani.
Nashindwa kuelewa ni kwanini sie tunashindwa kuendeleza biashara wakati wenzetu mambo yanaenda kama kawaida.
Mfano kampuni nyingi za Asia utakuta "Since 1960" hadi muda huu unakuta kampuni inadunda.
Nakaribisha mjadala ili tujue ni wapi tunakwama.
Wazazi wa kiswahili waache kukumbatia biashara kana kwamba wataishi nayo milele, wawashirikishe watoto wao
Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa ndipo tunapokosea sana kama wazazi. The least ni kuwaandaa kupata elimu ya biashara kuweza ku-add value katika biashara ya familia.Biashara zinakufa kwa sababu baba ama vichwa vya familia nyingi za africa haziwaandai watoto wao kusimamia mali zao bali wanawaandaa watoto na elimu ya darasani baadae mtoto aajiriwe.
Wakati baba yuko bize kusaka maisha na kufanya biashara basi huku mtoto yuko bize na kitabu tu.
Sent using Jamii Forums mobile app