Kwanini bunge La Kenya wanaongea English?

Kwanini bunge La Kenya wanaongea English?

Hivi kabla havijaletwa vyombo vya habari vyenye uwezo wa kupeperusha majadiliano moja kwa moja, wabunge wenu walikua wanatumia mbinu gani kuwalenga hao wananchi. Mbona unakua mgumu kuelewa issue ndogo hivi. Wabunge huchaguliwa kuwawakilisha wananchi ili wakajadili wao kwa wao na kutunga sheria kwa ajili ya nchi, pamoja na hoja zingine.

Ni majuzi tu tumepata vyombo vinavyotuwezesha kufuatilia. Mwananchi hata akifuatilia, hana uwezo wa kuhusika na nabaki tu kuangalia yanayoendelea.
tanzania imekuwa na broadcasting companies labla hata ya uhuru
 
Unaelewa umuhimu wa debate wewe, wabunge hawafanyi debate wakiwalenga wananchi, ila hujadili wao kwa wao kwa ajili ya wananchi na nchi. Hivyo umuhimu wa lugha humo ndani huwa ni kuelewana wakati wanapojadili. Inaonekana wabunge wa Tanzania huwa yao ni kuongea bungeni ili wawapendeze wananchi wanaowatazama.

Zaidi ni kwamba nchi yetu tuko huru kutumia lugha ya Kingereza na Kiswahili, na hata zetu za asili ambazo huwa tamu sana, ila Kiswahili kiofisi hakitumiki sana maana kina mapungufu mengi, hakijakomaa vizuri.

Wewe ni mwenyeji wa Kenya maeneo ya pwani au? Kwa kuandika tu, inaonyesha kiswahili unakijua vizuri sana maana wakenya wengi wasio wa pwani, Kiswahili ni kama janga ingawa huwa mnaelewana. Nimeuliza kiudadisi tu!
 
Kiswahili hakijasambaa vizuri Kenya, kuna baadhi ya maeneo kwao lugha ya Kiswahili ni tatizo, inawapa shida kuielewa, ndio maana wanatumia Kiingereza.
Hata hivyo kuna baadhi ya Wabunge huzungumza Kiswahili kwa mchanganyiko na Kiingereza. Ila kwa Kiingereza inasaidia karibu nchi yao nzima kuelewa kinachozungumzwa Bungeni.
Ova
 
Hivi kabla havijaletwa vyombo vya habari vyenye uwezo wa kupeperusha majadiliano moja kwa moja, wabunge wenu walikua wanatumia mbinu gani kuwalenga hao wananchi. Mbona unakua mgumu kuelewa issue ndogo hivi. Wabunge huchaguliwa kuwawakilisha wananchi ili wakajadili wao kwa wao na kutunga sheria kwa ajili ya nchi, pamoja na hoja zingine.

Ni majuzi tu tumepata vyombo vinavyotuwezesha kufuatilia. Mwananchi hata akifuatilia, hana uwezo wa kuhusika na nabaki tu kuangalia yanayoendelea.
tanzania imekuwa na broadcasting companies kabla hata ya uhuru
 
Lakini kwenye kampeni hakuna eneo lolote ndani ya kenya ambapo mgombea anatumia lugha tofauti na kiswahili kuombea kura.

Wanaongea na kiswahili pia ,jana nimeona mbunge akichangia mswaada wa usalama kwa kiswahili.Moja ya masharti ya kuwa mbunge Kenya ni kujua kusoma na kuandika Kiingereza na Kiswahili
 
Nilikuwa napenda kujua ni kwanini Bunge la Jamhuri ya nchi ya Kenya wanatumia Kiingereza kwenye dibeti zao?

Mkuu, umeuliza swali nzuri sana. Kwa muda mrefu nimetamaani kuleta mjadala kuhusu tofauti ya mchango wa Kenya na ule wa Tanzania katika ukuzaji wa Kiswahili, lakini mi hutatizwa sana wakati mjadala unageuka na kuwa ule wa "dudu langu ndefu kushinda lako."

Jambo la kwanza ambalo lafaa ujue ni kuwa kumekuwa na sera tofauti ya lugha, elimu, na siasa kwa hizi miaka ambazo zimepita. Tofauti na vile lawmaina78 anavyosema, Kiswahili kilikuwa lugha rasmi (official language) hata kabla ya katiba mpya kupitishwa. Ktika miaka ya sitini na sabini, hata Kiswahili kuchukuliwa kama lugha ya taifa ilikuwa vigumu sana. Mtu ambaye alikuwa ni kana kwamba anawaabudu wazungu - Charles Nonjo, alipinga sana. Lakini Mwaka wa 1974, Kenyatta mara moja akaamua na kusema Kiswahili kiwe lugha rasmi ya Bunge. Hii ilikuja ikatolewa baadaye na mchezo mwingi ukafanywa. Hivi leo, Lugha Rasmi ya High Court, Court of Appeal na Supreme Court, ni Kiingereza tu.

Tatizo ni kuwa, elimu ya kale haikumlazimisha mtu kusoma Kiswahili baada ya darasa la nne. Kwa hivyo, watu wengi waliosoma enzi zile hawakukielewa kiswahili kamwe. Moi alipoingia madarakani na kuileta mfumo wa 8-4-4, alilazimisha Kiswahili kifundishwe katika shule za upili hadi Kidato cha 4. Lakini, Kizazi hiki kilikuwa kimezoe sheng. Tofauti na vile flyingcrane anavyosema, hakuna yeyote atakayekudharau ukiongea Kiswahili sanifu bungeni; sijui hili amelitoa wapi. Tofauti na hilo, watu watakushangilia sana ikiwa utaongea kwa ufasaha.

Mdakuizi Umekosea unaposema kuwa katika bunge la taifa unakubaliwa kuchanganya ndimi. Kuna kanuni zinazofuatwa kuhusu lugha. Mara nyingi utampata Mbunge wa Tanzania anasema "Hili jambo la corruption ni lazima tulitatue once and for all." Jambo kama hili halikubaliki katika bunge la Kenya. Hili ndilo linafanya wabunge wanabaki kwa kiingereza.

Saa zingine, Kiswahili hutumika kuwakejeli wengine. Kama mnavyojua, mambo mengi ya Kiswahili yana maana mbili tofauti. Kwa mfano, Kuna mbunge mmoja aliyekuwa na tatizo na Raila Odinga ambaye alikuwa waziri mkuu. Kwa hivyo, akamwita Shoga - ambalo liko na maana tofauti. Hebu tazama video hii.

 
Last edited by a moderator:
Kibera ni Slum kubwa kabisa Kenya mzima. Lakini, utapata kuna wanasiasa wanaongea kiingereza na wananchi

 
Last edited by a moderator:
Kibera ni Slum kubwa kabisa Kenya mzima. Lakini, utapata kuna wanasiasa wanaongea kiingereza na wananchi



kibera ni kwa wajaluo, hao hata mzee mkongwe anaongea kizungu.
 
Last edited by a moderator:
Lakini kwenye kampeni hakuna eneo lolote ndani ya kenya ambapo mgombea anatumia lugha tofauti na kiswahili kuombea kura.

kama nilivyosema awali...asilimia kubwa ya wananchi wa wakawaida lugha ya mawasiliano ni lugha mama(native language) ama wakichanganya kiswahili na kiingereza(swanglish)....katika hali hiyo ili waeleweke inawapasa waongee ama kilugha chao au kiswahili kilichochanganywa na maneno ya kiingereza....

hapo kwenye red unakosea...nimeishi huko NA NINA FIRST HAND EXPERIENCED...nilikuwapo kipindi cha kampeini mwaka 2002/2003...media zinakuwepo sehemu zenye mchanganyiko wa jamii za madaraja na matabaka mbalimbali,ndio maana matumizi ya kiswahili unayaona,,,,,ukiingia countryside ni native languages kwa kwenda mbele na kiswanglish kiasi...
 
Nilikuwa napenda kujua ni kwanini Bunge la Jamhuri ya nchi ya Kenya wanatumia Kiingereza kwenye dibeti zao?

Na mimi nikuulize, kwa nini bunge la EA (EALA) wanatumia kiingereza?
 
Ohh kumbe ni hivyo! basi nilikuwa sijui kumbe huko Kenya ni tofauti na kwetu, hapa kwetu Mwananchi ndiyo mlengwa, na Mbunge anamwakilisha Mwananchi wake aliyemchagua hivyo ni muhimu kwa Mwananchi kuelewa Mbunge wake anasema nini!


Unahitaji kuongeza zaidi uwezo wa kufikiri!

Sio wabunge wote huongea bungeni, wengine huchangia kwa maandishi! Je kwa notion yako hawa huwaonyeshaje wananchi wao walichokichangia?
 
Kiswahili ni majanga kwa Wakenya wengi pamoja na kujipambanua kama Taifa linalozungumza Kiswahili
 
usisahau kwamba kiswahili wanachozungumza wakenya sio sanifu vile..kifupi,lugha ya kiswahili kwa wakenya ni vigumu kujieleza wakaeleweka vyema..hivyo wanapendelea kiingereza..
 
usisahau kwamba kiswahili wanachozungumza wakenya sio sanifu vile..kifupi,lugha ya kiswahili kwa wakenya ni vigumu kujieleza wakaeleweka vyema..hivyo wanapendelea kiingereza..
Mbaya zaid kwa wasiojua kizungu wanaongea kiswahili chao hicho cha kujigonga au lugha ZAO za asili.
Khy unqona hakuna network nzuri ktk mawasiliano ya lugha SBB kuna kundi halijui kiswahili
Kuna kundi LA pili halijui kizungu na kuna kundi la tatu halijui kiswahili wala kiingereza
Lkn wawakilishi wa wananchi waongea kizungu khy waweza kuta theluthi moja AMA zaidi ya wakenya hawajui kinachoongelewa bungeni.
 
  • Thanks
Reactions: Oii
Wakenya wanatumia kingereza Kwa sababu wenye kuimiliki nchi ya Kenya awajui kiswahili Kenya isha uzwa Kwa wazungu siku nyingi
 
Back
Top Bottom