Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
- Thread starter
-
- #21
Nautetea na nitaendelea kuutetea na naupenda sana Muungano wetu na nasema Muungano na Udumu Zaidi. Lakini pia napenda kukwambia ya kuwa Suala la muungano siyo sawa na soda ya cocacola kwamba lazima iwe sawa Dunia nzima.Kama ni ndogo kwanini unaendelea kuutetetea muungano? Yaani unaweza kutupa faida mbili za muungano...
Zanzibar ina wapiga kua chini ya laki 6, lakina ina wawakilishi zaidi ya 70 kwenye bunge. Jibu ni kwanin?Alleni embu niambie ni nani ndani ya CHADEMA unayeweza mfananisha au mweye Uwezo kama alionao Mheshimiwa Kafulila?
Mwisho japo siyo kwa umuhimu nijibu swali hili ambalo huwa unakimbia. Wewe ndiye yule Alleni wa kwenye kile kipindi cha Ebon Fm kilichokuwa kinakuwa kila siku ya jumamosi kukichambua masuala mbalimbali na kuongozwa na mtangazaji Neema Msafiri a.k.a Mama John?
tatizo si kutetea, tatizo unatetea kitu ambacho huwezi kukitetea na hujawahi kukielewa , sasa unasema kafulila wakati hata wewe huwezi kujibu alichouliza Tundulisu?!Nautetea na nitaendelea kuutetea na naupenda sana Muungano wetu na nasema Muungano na Udumu Zaidi. Lakini pia napenda kukwambia ya kuwa Suala la muungano siyo sawa na soda ya cocacola kwamba lazima iwe sawa Dunia nzima.
Kitendo tu cha kuandika kwa herufi kubwa inaonyesha aina ya akili yako ilivyo ndogo. Unaandika utafikiri unawandikia watu wenye matatizo ya kuona?UKIWA NAYE CHUMBANI NDO HUWA ANAKUAMBIA HIVYO? MUWE MNACHUJA MANENO SERIOUS NA YALE YA KUKUPANGA KUKUWEKA SAWA.
achana naye huyo😂Ubarikiwe sana kwa mtizamo wako.
Narudia kusema tena kuwa Lissu hana hoja kabisa zenye kustahili kujibiwa .ndio maana unaona Anaendelea kupuuzwa tu na watanzaniatatizo si kutetea, tatizo unatetea kitu ambacho huwezi kukitetea na hujawahi kukielewa , sasa unasema kafulila wakati hata wewe huwezi kujibu alichouliza Tundulisu?!
Embu tupe faida mbili za huu muungano?🤣🤣
Mimi ni Mzalendo na hupenda kuwaunga mkono watu wazalendo na wachapa kazi aina ya David Kafulila bure kabisa pasipo malipo ya aina yoyote ile.Sio bure na Kafulila wako, unavyomuanzishia nyuzi kila siku huenda dada yetu mbunge wa covid 19 wewe! Mwanaume hawezi kumsifia mwanaume mwenzie kila siku namna hii kama hamna maslahi anapata!
Nimeamua kumsamehe tu maana wengine unakuta wanaingia humu jukwaani wakiwa na msongo wa mawazo na wanatafuta kwa kutolea hasira zao. Ndio maana unaweza kuta mtu anakutukana matusi bila breki bila sababu ya msingi.kwa hiyo usipokuwa na akili unaweza jikuta umenaswa kwenye mtego wake.achana naye huyo😂
basi jaribu kujibu wewe🤣🤣 maana mlimsingiza mara anatetea ushoga lakini mama samia yeye alisema fanyianeni wakubwa kwa wakubwa mbona hatukusikia mkikemea😂🤣🤣??Narudia kusema tena kuwa Lissu hana hoja kabisa zenye kustahili kujibiwa .ndio maana unaona Anaendelea kupuuzwa tu na watanzania
Mbona watanganyika hawafanyi kazi ZANZIBAR wala kuruhusiwa kumiliki ardhi? Nani ni mbaguzi mbobezi hapo?Kwani wewe huonagi anaanza kuuliza kwanini huyu anafanya kazi huku watu ni Mzanzibari? Hukuona na kusikia alichosema na kuzungumza alipokuwa Morogoro? Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere amewahi kusema kuwa dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana na ni sawa na kula Nyama ya Mtu ambapo huwezi kuacha. Lissu ni mtu Mwenye ubaguzi,chuki na roho mbaya sana.
kwanba muungano wa tanganyika na zanzibar una matatizo ni uzushi na ubaguzi? nani anambagua mwenzie kati ya tanganyika na zanzibar?Tundu Lissu hana hoja za kustahili kujibiwa .Maana Lissu hoja zake ni za uzushi ,uongo na ubaguzi tu. Mheshimiwa Kafulila sizani kama anaweza kuwa na muda huo mchafu wa kujibu hoja zisizo na mashiko wala maslahi kwa Taifa letu.
Mr lucas una hoja nyepesi mno kulinganisha na uzito wa mambo ya kitaifa , sio kwa ubaya lakini 😊Ni uteuzi mzuri sana uliogusa mioyo ya watu wengi sana. Lakini ambao umeendelea kuiwasha na kuonyesha namna Mheshimiwa Kihongosi alivyo na Nyota kali kama ile iliowaongoza Mama Jusi kwenda alipofichwa Mtoto yesu kristo
Ulifanya utafiti gani,lini na wapi na njia gani ya utafiti ulitumia hadi kuja na hitimisho hili? After all Chadema wanahusiana nini na Kafulila and what is so special about Kafulila hadi unamuwaza hivyo? Lucas Mwashambwa una dalili zote za mtu aliyechanganyikiwa akili. Hizi mada zako mfu hazikusaidii wewe wala CCM sijui kwa nini unajibebesha mzigo wote huu usiokuwa na tija. Wewe ni kichaa sijui hili zigo lako unaenda kulitua wapi na lini.Ndugu zangu Watanzania,
Nimefuatulia mijadala mbalimbali ya kisiasa inapokuwa ikifanyika katika maeneo mbalimbali,iwe ni mitaani au kwenye mitandao ya kijamii. Nimekuja kugundua kuwa CHADEMA na wana CHADEMA wanamuogopa Sana Mheshimiwa David Kafulila linapokuja Suala la kushindanisha na kujenga hoja juu ya masuala mbalimbali hususani ya kiuchumi.
Hoja za Mheshimiwa Kafulila zimekuwa zikiwatoa sana Jasho na kuwakimbiza kama Mwenge wa Uhuru na hakuna anayeweza wala kufanikiwa kupangua hoja zake kwa hoja na akaweza kueleweka kwa watu. Mfano mdogo ni juu ya hoja nzito ambazo Mheshimiwa David Kafulila amekuwa akieleza na kuitetea serikali juu ya ukopaji na uchukuaji wa mikopo kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo imekuwa na matokeo chanya kwa uchumi wetu .
Ambapo Mheshimiwa Kafulila ametoa Elimu pana sana kuanzia masuala ya marshall Plan ya Mmarekani ilivyozisaidia nchi za Ulaya, na namna nchi mbalimbali hata zilizoendelea kama vile Japan ambavyo zina madeni makubwa tu.akaenda mbali zaidi kuelezea kwa hoja na ushahidi kuwa Tanzania siyo miongoni mwa nchi zenye madeni makubwa.na kwamba Uchumi wa Tanzania umekuwa kwa kiwango kikubwa sana ndani ya muda mfupi wa Uongozi wa Rais Samia kutoka takribani Dolla Billion 66 mpaka zaidi ya Dolla Billion 85.akaelezea pia ongezeko la watalii ambalo limefikia zaidi ya watalii Million 1.8.ambapo imepelekea kuongezeka kwa mapato mabilioni kwa mabilioni.
Mheshimiwa Kafulila akaelezea pia maana ya ujenzi wa huduma za kijamii kiuchumi zilizojengwa awamu hii ya Rais Samia.akaelezea mfano kwa kipindi hiki kumekuwa na mapinduzi makubwa sana katika Secta ya Afya ,ambapo sasa wananchi wanapata huduma za afya karibu kabisa na maeneo yao.ambapo sasa badala ya mtu huyu kutumia nauli kubwa kwenda umbali mrefu kupata huduma za afya ,sasa anaokoa pesa ya nauli na kuitumia kwa mahitaji yake mengine.
Mheshimiwa Kafulila ameweza na kufanikiwa kwa uhodari na umahili mkubwa sana na kwa takwimu kuelezea Mwenendo wa kiuchumi wa Dunia na hali ya mikopo na madeni kwa Nchi mbalimbali Duniani. Jambo ambalo limewapa Elimu na ufahamu Mkubwa sana wananchi.hali hii imewaacha CHADEMA hoi bin taabani hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa wao huongea kiujumla jumla tu pasipo kuwa na takwimu za aina yoyote ile.hali inayotokana na kukosa uelewa na watu wenye uelewa na Elimu ya masuala ya Uchumi na namna uchumi wa Dunia unavyokwenda.
Ndio maana kuna wakati walikuwa wanapiga kelele kuwa mafuta ya petrol yanauzwa bei juu sana na kwamba hali hiyo inasababishwa na serikali ya CCM. Lakini walikuja kuishiwa nguvu na kupata aibu ya karne pale walipoona wakenya mbalimbali wanakimbilia Tanzania kununua mafuta kwa kuwa bei yetu ilikuwa ni ndogo ukilinganisha na Nchini kwao.hii ni baada ya serikali ya Rais Samia kuwa na utaratibu wa kutoa Ruzuku ya Billion Mia moja kila Mwezi katika Mafuta na hivyo kupelekea Bei ya mafuta kuwa chini ukilinganisha na Majirani zetu..
Ikumbukwe bei ilikuwa imepanda kutokana na kupanda katika soko la Dunia,kulikokuwa kumechochewa na kuchangiwa na vita vya Ukrein na Urussi.ila wao CHADEMA wakawa hawaelewi kitu chochote kile maana wao hawawezagi kuangalia na kujuwa hali ya Dunia inakwenda vipi. Na kwamba wao huona kama Tanzania ni kisiwa hapa Duniani.
Sasa Mheshimiwa Kafulila amekuwa akiwatwanga kwa hoja nzito na zenye ushahidi wa kutosha na takwimu sahihi ,jambo linalowafanya wamuogope sana na kumuona adui wao wa kuwaumbua udhaifu wao na uongo wao na upeo wao mdogo wa masuala mbalimbali hususani ya kiuchumi.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Naona umeongea vitu mchanganyiko mpaka umejichangaya Mwenyewe. Sasa Mheshimiwa Dkt Mwigulu Nchemba ameingiaje hapa? Au unachuki binafsi? Au umechaganyikiwa? Au umevurugwa akili yako?kwanba muungano wa tanganyika na zanzibar una matatizo ni uzushi na ubaguzi? nani anambagua mwenzie kati ya tanganyika na zanzibar?
kwamba mwigulu anamiliki timu nyingi za mpira hapa nchini ni uzushi?
kwamba katiba ya JMT ina matatizo ni uzushi na siyo hoja yenye mashiko
RUDI SHULE WEWE ACHA KUKARIRISHWA
Ingefaa ungesema hoja fulani ni nyepesi kwa sababu hii na hii.pia ungesema hoja hii ni nzito na sababu ni hii na hii. Hoja hujibiwa kwa hoja.Mr lucas una hoja nyepesi mno kulinganisha na uzito wa mambo ya kitaifa , sio kwa ubaya lakini 😊
Wewe huwezi ukaelewa hoja hii maana imekupita na kukuzidi kimo cha akili yako.Ulifanya utafiti gani,lini na wapi na njia gani ya utafiti ulitumia hadi kuja na hitimisho hili? After all Chadema wanahusiana nini na Kafulila and what is so special about Kafulila hadi unamuwaza hivyo? Lucas Mwashambwa una dalili zote za mtu aliyechanganyikiwa akili. Hizi mada zako mfu hazikusaidii wewe wala CCM sijui kwa nini unajibebesha mzigo wote huu usiokuwa na tija. Wewe ni kichaa sijui hili zigo lako unaenda kulitua wapi na lini.
Kumsifia mtu nako unaita hoja? Una mtindio wa ubongo wewe si bure. Wewe ulichoandikia ni kumsifia tumbili sasa hoja iko wapi au unataka na mimi nimsifie? Wewe soon tutakukuta unafakamia mauchafu majalalani.Wewe huwezi ukaelewa hoja hii maana imekupita na kukuzidi kimo cha akili yako.
Mwigulu ameingia kwasababu lisu aliibua hoja kwamba mwigulu anamiliki ihefu, singida united, majaliwa anamiliki namungo, biteko kuna timu itapanda ikiwa ni ya kwake, JPM alimiliki Gwambina FC na aliyasema haya akiwa jimboni kwa mwigulu.Naona umeongea vitu mchanganyiko mpaka umejichangaya Mwenyewe. Sasa Mheshimiwa Dkt Mwigulu Nchemba ameingiaje hapa? Au unachuki binafsi? Au umechaganyikiwa? Au umevurugwa akili yako?