Kwanini Congo DRC?

Maelezo mengi lakini hauja jibu nilicho uliza ,zaidi umekwenda mbali kwa kuonesha wanufaika wa Mali ya DRC.

South Africa Kuna mali mbona kumetulia,shida ya Congo iko kwa Wacongomani wenyewe.
 
Japo hatuifikii Congo, lakini hata sisi utajiri tulio nao si haba! Lakini mbona sisi tuna "amani"?

Huoni kama na Wacongo nao wamechangia hayo yanayoendelea nchini kwao?
Hatufiki hata asilimia 1 ya Congo Madini yao na rasilimali zao, unailinganisha sisimizi na Nyangumi mkuu.

Estimation ya Madini ya Congo ni $24 trillion, sijui hata nikuelezeje ila it's a lot of money. Kama hayo Madini yanauzwa kwa haki kwa pamoja basi Immediately Congo inakua Nchi ya pili Tajiri zaidi Duniani na GDP per capita inakuwa ya kwanza Duniani.

Na Madini yao sio tu urembo kama ya kwetu bali ni Madini ambayo yameshikilia Dunia, Cobalt inatumika na kifaa Chochote cha Electronic iwe Simu, laptop, gari Na mengineyo. Soko lake kwa Dunia linafika hadi $30B ila Congo wanapata tu visenti.

Congo imara ina maana watakaza, wao ni monopoly wanazalisha zaidi ya Asilimia 70 ya Cobalt hivyo wanaweza ku regulate bei, so ili watu wasifike huko inabidi nchi iwe undermined watu waendelee kuiba.
 
Maelezo mengi lakini hauja jibu nilicho uliza ,zaidi umekwenda mbali kwa kuonesha wanufaika wa Mali ya DRC.

South Africa Kuna mali mbona kumetulia,shida ya Congo iko kwa Wacongomani wenyewe.

..Na mimi nimeuliza mbona mpaka wa Congo na South Sudan, Afrika ya Kati, Tanzania, Zambia, Angola, hakuna shida?

..kwanini eneo lisilo na amani ni lile linalopakana na Rwanda, na Uganda, wakati mipaka mingine iko shwari?
 

..mbona Tanzania kuna amani lakini madini yanatoka?

..amani ikiwepo madini yatatoka kwasababu Congo inahitaji mapato kutokana na madini hayo, na zaidi hawana teknolojia ya kuyachimba.
 
Na huu ndo ukweli ambao wengi hatutaki kuukubali kama viongozi wa Congo hawajali kuhusu raia wao nani atajali ? Mfano raia wa Canada awe na uchungu na raia Wa'congo ambao viongozi wao hawajali kuhusu raia wao ni maajabu ya karne.
Viongozi wa Congo ni mafisadi wa kutupwa .
 
Mkuu comment yako ingemake sense kama Western powers ndio wanunuaji pekee wa hayo Madini.

Cobalt is hot product, kila nchi duniani inaimezea mate, so Congo ikiwa na amani ina maana kutakuwa na bidding wars baina ya Nchi, atakaetoa kiasi kikubwa cha pesa ndio atapata Bidhaa, hichi ndio hao watu wa magharibi hawakitaki,

Sasa hivi China ananunua asilimia 80 ya Cobalt ya Congo (inayouzwa Ki halali) At same time Rwanda ana deal na EU na west kwa Ujumla kuwauzia Madini, it's open secret hayo Madini yanayokuwa smuggled yanakweda zaidi west

Nikukumbushe tu mkuu Che Guevara alipo kuja kukomboa Kongo, nchi za Magharibi ziliogopa sana na ku stock cobalt kwa wingi, Na kwa njia yoyote ile waliitaka tena Cobalt ambayo wakati huo wa cold war ilienda USSR, ndio wakamuweka Dikteta wao Mobutu.
 
..mbona Tanzania kuna amani lakini madini yanatoka?

..amani ikiwepo madini yatatoka kwasababu Congo inahitaji mapato kutokana na madini hayo, na zaidi hawana teknolojia ya kuyachimba.
Guys rudini kwenye data kucompare Tanzania na Congo kwenye Madini ni dhihaka hizi, we are talking $24 trillion worth of minerals here, tena Madini yanayorun Dunia sio Tanzanite na dhahabu.

Cobalt pekee soko la dunia inaenda hadi $30B na Congo anahusika na 70% ya hio cobalt, sisi Export yetu kwa mwaka hata $2B haifiki, mwaka uliopita ni kama $1.4B. Kama mapato yetu miaka 20 Madini yote hayafikii pato la dini moja tu la Congo kwa. Mwaka huoni ni ujinga kucompare hizi Nchi?
 
Maelezo mengi lakini hauja jibu nilicho uliza ,zaidi umekwenda mbali kwa kuonesha wanufaika wa Mali ya DRC.

South Africa Kuna mali mbona kumetulia,shida ya Congo iko kwa Wacongomani wenyewe.
South Africa reserve yao ya Madini $2.5 Trilioni, Congo $24 Trilioni. Mbinguni na Ardhi.

Hakuna Africa Hii nchi yenye Madini hata robo tu ya Congo,
 

..mataifa makubwa yatachimba vizuri zaidi kama Congo ikiwa na amani.

..hawa-invest kwenye amani ya Congo kwasababu supply madini haijakata.
 

..China anapata madini.

..Western countries zinapata madini.

..kwasababu vita haijaathiri supplies ndio maana hawajishughulishi nayo.
 
Mkuu, sidhani kama Kishansa hata wanajua kama nchi ipo vitani huko Kivu. DRC ni muunganiko wa nchi nne ndani ya ardhi moja..
 
..China anapata madini.

..Western countries zinapata madini.

..kwasababu vita haijaathiri supplies ndio maana hawajishughulishi nayo.
Vita vinasaidia supply ya Madini west kuongezeka (wanahusika na smuggling) Amani inasaidia Maslahi ya Congo kuongezeka wataweza kuuza kwa wanayemtaka.
 
Vita vinasaidia supply ya Madini west kuongezeka (wanahusika na smuggling) Amani inasaidia Maslahi ya Congo kuongezeka wataweza kuuza kwa wanayemtaka.

..amani itasaidia SERIKALI ya Congo kupata mapato makubwa zaidi, na hata kuweza ku-,negotiate bei nzuri.

..vita hii haiongezi wala kupunguza supply kwa nchi za magharibi, China, na nyinginezo.

..vita ingekuwa inaathiri upatikanaji / supply ya madini hayo muhimu kwa nchi zenye viwanda, basi ungezishuhudia zikiushughulikia mgogoro huo kwa nguvu zaidi.
 
shida ni Paul kagame na mseveni .wale jamaa siyo kabisa.sisjui kwa nini wako EAC
 
DRC ni Nchi pekee ambayo Mtutsi hawezi kuwa raia ni sawasawa na kusema Wamasai wote ni wakutoka Kenya Mmasai hawezi kuwa Mtanzania.
 
Yote ni majibu ....

Kuhusu uongozi tangu auwawe Patric Lumumba, viongozi waliofuata hasa Mobutu hakuwa mzalendo kabisa.

Rasilimali zake ilizonazo zinaiponza.
 
Wewe ndio unafikiri hivyo ila Usa na West kwa Ujumla hawafikirii hivyo. Na siongelei theory nimekupa tu mfano mzuri hapo hapo Congo, Mobutu alisaidiwa na Usa Kupindua serikali ya Congo sababu ya Cobalt, sababu tu Serikali hio iliuza Cobalt zake USSR, trust me they will never ever kukubali wasipate hio cobalt, wataanzisha hata vita vikuu vya 3 vya dunia.

Na vita haviwaathiri wao sababu wao ndio wana fund hayo makundi, so wanajua wanachofanya ni nini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…