Kwanini derby ya Yanga na Simba haikuchezwa?

Kwanini derby ya Yanga na Simba haikuchezwa?

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Wengi tumejikita kwenye habari za kanuni na mabaunsa ila ngoja nipanue kidogo mjadala wa kwa nini derby ya Simba na Yanga haikuchezwa tarehe 08/03/2025.

Msichukulie huu uzi serious sanaaana ila unaweza kusaidia kupanua mawazo kidogo wakati huo huo ukitoa burudani ya hapa na pale. Tujadili bila makasiriko.

Labda ya 1: Samia Cup.
Tukumbuke ligi ya wanawake ikiwa inaelekea kuchezwa mechi ya derby ya Simba na Yanga ya wanawake, ghafla iliahirishwa ili kupisha Samia Cup kule Arusha.

Simba huwa inapata ugumu sana kujiingiza moja kwa moja kwenye siasa za uchawa. Ingekuwa ngumu sana kukubali kuahirisha derby ya wanaume kwa sababu hii na ukizingatia ina ratiba ngumu ya CAF na viporo siyo vizuri katika hatua hii. Kwa Simba kutotoa ushirikiano, wakapewa ugumu waliokutana nao. Kwa lugha nyingine, derby ikaahirishwa kwa lazima. Sasa hivi focus ipo Samia Cup.

Labda ya 2: Kifo cha Prof. Sarungi.
Hii utahitaji D mbili na walau C moja kuweza kulinyambua hili. Ngoja nipime kama kuna majiniasi watusaidie kulidadavua hili.

Halafu, hivi mbona Simba hawakuvaa vitambaa vyeusi walipocheza na TMA kwenye CRDB Confederation Cup?

Labda ya 3: Majeruhi ya Che Malone na Camara.
Simba waliona bila wachezaji hao wawili na wakati huo huo striker tegemeo Ateba akionekana kusuasua kipindi hiki, kuna dhahma ilikuwa inakuja mbele. Ukasukwa mpango mkakati.

Labda ya 4: Vita ya Kisaikolojia.
Ni wazi Simba ilikuwa inaingia kama underdog katika mechi hii. Kwa kuona ugumu wa mechi hii na umuhimu wa ushindi katika mbio za ubingwa, walichofanya Simba ni kuwashtukiza Yanga kwa kwenda kufanya mazoezi. Taarifa ilitolewa mapema ila hakuna aliyedhani Simba kweli ingeenda kufanya mazoezi. Hata kama kanuni inaruhusu, kawaida hizi timu hazikanyagi uwanja wa mechi kufanya mazoezi siku moja kabla. Huo utamaduni umekuwepo na hata uwepo wa mabausa kulinda uwanja ni sehemu ya utamaduni huo. Kuna video zilisambaa siku kadhaa hata kabla ya tukio zikionyesha mabaunsa wakilinda uwanja. Wanaowakana mabaunsa wa Yanga wameanza kushabikia mpira juzi juzi.

Wataalamu wa Simba walijua kuna mojawapo kati ya mambo mawili yangeweza kutokea ambayo yote yangekuwa faida kwa Simba.

Kwanza, Simba ingekubaliwa kufanya mazoezi baada ya mabishano na mvutano mkubwa pale getini. Kwa sababu ya element ya surprise waliyofanya Simba, kesho yake Yanga ingeingia kinyonge na hiyo kidogo ingeifaidisha Simba. Kumbuka, watu wa Yanga wasingeruhusiwa kuingia uwanjani wakati Simba inafanya mazoezi. Hata kama Simba ingeruhusiwa kufanya mazoezi, lazima vurugu zingetokea kubwa zaidi ya zile tulizoshuhudia, ama wakati wapo bado ndani au wakati wanaondoka baada ya mazoezi. Kiufupi, Yanga wangekataa kuingia kwenye mechi hii kinyonge. Hizi vurugu za wakati au baada ya mazoezi bado zingeweza kusababisha mechi kutochezeka.

Pili, Simba kukataliwa kufanya mazoezi na hata kufanyiwa fujo na hivyo kukataa kucheza mechi na kudai pwenti 3. Hili ndiyo lililotokea.

Ongezea labda nyingine ambazo sijazitaja.
 
Wengi tumejikita kwenye habari za kanuni na mabaunsa ila ngoja nipanue kidogo mjadala wa kwa nini derby ya Simba na Yanga haikuchezwa tarehe 08/03/2025.

Msichukulie huu uzi serious sanaaana ila unaweza kusaidia kupanua mawazo kidogo wakati huo huo ukitoa burudani ya hapa na pale. Tujadili bila makasiriko.

Labda ya 1: Samia Cup.
Tukumbuke ligi ya wanawake ikiwa inaelekea kuchezwa mechi ya derby ya Simba na Yanga ya wanawake, ghafla iliahirishwa ili kupisha Samia Cup kule Arusha.

Simba huwa inapata ugumu sana kujiingiza moja kwa moja kwenye siasa za uchawa. Ingekuwa ngumu sana kukubali kuahirisha derby ya wanaume kwa sababu hii na ukizingatia ina ratiba ngumu ya CAF na viporo siyo vizuri katika hatua hii. Kwa Simba kutotoa ushirikiano, wakapewa ugumu waliokutana nao. Kwa lugha nyingine, derby ikaahirishwa kwa lazima. Sasa hivi focus ipo Samia Cup.

Labda ya 2: Kifo cha Prof. Sarungi.
Hii utahitaji D mbili na walau C moja kuweza kulinyambua hili. Ngoja nipime kama kuna majiniasi watusaidie kulidadavua hili.

Halafu, hivi mbona Simba hawakuvaa vitambaa vyeusi walipocheza na TMA kwenye CRDB Confederation Cup?

Labda ya 3: Majeruhi ya Che Malone na Camara.
Simba waliona bila wachezaji hao wawili na wakati huo huo striker tegemeo Ateba akionekana kusuasua kipindi hiki, kuna dhahma ilikuwa inakuja mbele. Ukasukwa mpango mkakati.

Labda ya 4: Vita ya Kisaikolojia.
Ni wazi Simba ilikuwa inaingia kama underdog katika mechi hii. Kwa kuona ugumu wa mechi hii na umuhimu wa ushindi katika mbio za ubingwa, walichofanya Simba ni kuwashtukiza Yanga kwa kwenda kufanya mazoezi. Taarifa ilitolewa mapema ila hakuna aliyedhani Simba kweli ingeenda kufanya mazoezi. Hata kama kanuni inaruhusu, kawaida hizi timu hazikanyagi uwanja wa mechi kufanya mazoezi siku moja kabla. Huo utamaduni umekuwepo na hata uwepo wa mabausa kulinda uwanja ni sehemu ya utamaduni huo. Kuna video zilisambaa siku kadhaa hata kabla ya tukio zikionyesha mabaunsa wakilinda uwanja. Wanaowakana mabaunsa wa Yanga wameanza kushabikia mpira juzi juzi.

Wataalamu wa Simba walijua kuna mojawapo kati ya mambo mawili yangeweza kutokea ambayo yote yangekuwa faida kwa Simba.

Kwanza, Simba ingekubaliwa kufanya mazoezi baada ya mabishano na mvutano mkubwa pale getini. Kwa sababu ya element ya surprise waliyofanya Simba, kesho yake Yanga ingeingia kinyonge na hiyo kidogo ingeifaidisha Simba. Kumbuka, watu wa Yanga wasingeruhusiwa kuingia uwanjani wakati Simba inafanya mazoezi. Hata kama Simba ingeruhusiwa kufanya mazoezi, lazima vurugu zingetokea kubwa zaidi ya zile tulizoshuhudia, ama wakati wapo bado ndani au wakati wanaondoka baada ya mazoezi. Kiufupi, Yanga wangekataa kuingia kwenye mechi hii kinyonge.

Pili, Simba kukataliwa kufanya mazoezi na hata kufanyiwa fujo na hivyo kukataa kucheza mechi na kudai pwenti 3. Hili ndiyo lililotokea.

Ongezea labda nyingine ambazo sijazitaja.
Haikuchezwa kwasababu
1. Kamati ya Ligi ni sanamu
2. Simba walikimbia mechi, (underdog),

Simba SC kwavile ni underdog kwa yanga sc baada ya kugundua kwamba bodi ya Ligi ni mazezeta, (dhaifu), ama uwezo wao wa kufikiri ni mdogo walibuni mbinu ya kuahirisha mechi, (derby), je kuna mazingira ya rushwa na kama hakuna rushwa kwanini hawakufwata kanuni za ligi kuu ya Tanzania,

Bodi i ya Ligi ni wazembe huwa hawaendi eneo la tukio, (uwanjani), wanategemea taarifa toka meneja wa uwanja na kamishina wa mchezo, na Ndiyo maana hawakuweza kutatua changamoto iliyo kuwepo ndani ya saa 1
 
Sababu zitatajwa mia ila ukweli mchungu usemwe, kwa quality ya wachezaji wa Yanga kwasasa Simba ni underdog na hawako tayari kabisa kucheza derby na kukandwa mara khamsa ili kuleta uwiano na zile goli tano, hii ina maana kila derby itakapofika Simba watakimbia mechi hadi pale wataona sasa wanaimudu Yanga baada ya kuuzwa Maxi, Ki Aziz, Pacome, Dube, Mzize , Aucho na Mudathir.

Kukimbia derby ni mpango mkakati halali wa viongozi wa kolowizard kuendelea kusalia ofisini kwa miongo kadhaa ijayo maana wanakalia kuti kavu na kipigo cha tano ambacho hakiepukiki hakitabakisha mtu ofisini.
 
Yanga haina timu ya kuitisha Simba
Timu imejaa propaganda na kwa sbb akili zao finyu na wao wanapropagandika....
Yanga ya sasa ni makopo....inabebwa na mdhamini wao kudhamini timu lukuki na wachambuzi uchwara....
Napita...
 
Utahira tu.... Labda simba waliogopa kipenyo chao kupekenyuliwa
 
Sababu zitatajwa mia ila ukweli mchungu usemwe, kwa quality ya wachezaji wa Yanga kwasasa Simba ni underdog na hawako tayari kabisa kucheza derby na kukandwa mara khamsa ili kuleta uwiano na zile goli tano, hii ina maana kila derby itakapofika Simba watakimbia mechi hadi pale wataona sasa wanaimudu Yanga baada ya kuuzwa Maxi, Ki Aziz, Pacome, Dube, Mzize , Aucho na Mudathir.

Kukimbia derby ni mpango mkakati halali wa viongozi wa kolowizard kuendelea kusalia ofisini kwa miongo kadhaa ijayo maana wanakalia kuti kavu na kipigo cha tano ambacho hakiepukiki hakitabakisha mtu ofisini.
Hizi ndio akili za ajabu,Yaani timu inashindwa kuikanda Tabora,JKT,Coastal,Singida,Fountain Gate,Dodoma goli 5 ndio ije iifunge 5 Simba?Timu iliyoshindwa kupata sare nyumbani na MC Algers.mnaringia goli 5-1 mnasahau bado hamjalipa bado goli 5-0 na vipigo vingine vikubwa mlivyopigwa na Simba.Mbona mnaogopa kuleta timu kwenye mechi itakayopangwa kama si uoga wa kichapo ni nini?
 
Underdog fc walichungulia wakaona kuna hatari ya kupokea kipigo yakinifu wakaona bora nusu shari kuliko shari kamili...........nduki :Applecatrun:
 
Back
Top Bottom