Kwanini ELIMU yetu inaendelea kushuka thamani kila kukicha?

Kwanini ELIMU yetu inaendelea kushuka thamani kila kukicha?

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
KATUNI(725).jpgKATUNI(725).jpgKATUNI(725).jpg


Kuwalaumu wanafunzi au waalimu pekee ni kutafuta majibu mepesi kwenye maswali mazito. Lengo la elimu ni kukulainishia maisha lakini kama ukiwa nayo na yule asiyenayo nyote mnarundikwa kundi moja basi motisha wa kuwa na elimu hupotea.

Wanafunzi wengi wanaona jinsi jamii na hususani serikali yao inavyodharau wasomi wake na hivyo kujenga mitazamo ya kuwa maisha yao hayana uhusiano wowote ule na elimu hiyo. Hivyo kutokazana kujifunza na matokeo yake ni kutofanya vizuri mashuleni.

Motisha ulioporwa na serikali ni katika maeneo yafuatayo:-

1) SERIKALI INAABUDU WANASIASA!



Kama mshahara wa Raisi siku hizi ni siri yake na wakati wa Nyerere mshahara wa Raisi ulikuwa Tshs 5, 000/= tu kwa mwezi. Unapoona usiri katika shughuli za umma ujue ni ujambazi wa uporaji tu ndiyo unaoendelea hapo. Serikali inaona aibu jinsi ambavyo imeuinua mshahara wa Raisi na hata kutuficha sisi waajiri wa huyo Raisi!

Bunge kazi kubwa ni kuongezeana mishahara na posho bila kuwepo chombo ambacho kinachoratibu mishahara na mafao ya watumishi wote wa umma ili kujenga misingi ya haki na kuheshimiana. Bungeni hupigia ukelele khali duni za watumishi wa umma lakini hutasikia khoja binafsi ya kuboresha masilahi ya watumishi wa ngazi za chini wa serikali ambako wengi ndipo wamo.

Aidha kinyume na matakwa ya kikatiba, Serikali imewabagua watumishi wote wa Umma na kuja na sheria ya mafao ya viongozi wa kitaifa ya mwaka 1999 na kuiboresha mwaka 2005. Huu ni ubaguzi wa kutisha na katiba inakataza tusibaguane kabisa. Serikali ikielewa ya kuwa ukokotoaji wa mafao ya kustaafu hakuzingatii khali halisi ya mfumuko wa bei na mapato wao kazi yao ni moja ni ya kuwalinda walaji wakuu serikalini wakaja na formular za 80% ya mshahara wa sasa ambao tayari umerekebishwa kumudu mfumuko wa bei huku walalahoi wanaachwa kwenye formulars ambazo hazina uhusiano wowote ule na mshahara wa sasa!

Mwanafunzi aliyepo shuleni hivi leo anaona hii dhuluma na kuvunjika moyo kukazana shuleni kwani haoni elimu hiyo itamsaidiaje kwenye maisha yake ya kiutu uzima.

2) Soko la ajira ni finyu.


Mimi huwa nacheka mpaka mbavu zinaniuma pale ambapo naona na kusikia "waajiriwa" viongozi wa serikalini wanapowahimiza vijana wajiajiri wakati wao "waajiriwa" ukifikia muda wa kustaafu huchukua mikataba kujiongezea utumishi haramu serikalini. Pia viongozi hao huhubiri "kujiajiri" wakati wao kamwe hawajawahi kujiajiri na kuelewa ugumu katika hiyo sekta ya ujasiriamali.

Mwanafunzi aliyepo darasani leo anajiuliza hivi kweli hii elimu itanipeleka wapi, maana hana mtaji hususani uzoefu wa kujiajiri na serikalini wazee wanashikilia ajira hadi kufa..............

3) Wasomi wageni ndiyo kipenzi cha serikali.

Kampuni za kigeni ndizo hupewa mnofu na hii serikali yetu kwa visingizio lukuki vikiwemo wanauzoefu na kampuni za kizawa kuambulia mifupa. Sasa unategemea kweli kwenye mazingira ya namna hii divisheni ziro zisiongezeke? Lazima kuwepo uhusiano wa moja kwa moja kati ya kiwango cha elimu na upatikanaji wa mkate vinginevyo elimu hiyo haina maana...........

4) Ajira za kujuana.

Hivi utamwelezaje mwanafunzi wa leo anapoona ajira kila mahali ni kujuana na wala siyo sifa? Sasa akazane ili iwe nini kama anachotakiwa kufanya siyo kusoma bali kumfahamu mwajiri wake tu kupitia soko la kufahamiana na kufahamishiana? Wengine wanaliita soko tajwa kuwa ni soko la kuwezeshana........

5) Wasomi kutopewa mitaji ya kuanza kujiajiri.

Wahubiri wa "mkajiajiri" kwa vile wao hawajawahi "kujiajiri" wanakosa ufahamu wa changamoto za ujasiriamali na mojawapo ya changamoto hizo ni ukosefu wa mitaji. Jitihada za kuwakopesha huishia
shs elfu hamsini ambayo ukimwuliza yule anayezitoa anatarajia mkopeshwaji atazifanyia nini hawezi kukujibu zaidi ya kujitetea uwezo wake ndipo ulipoishia. Kama hela hazitoshi kwanini hata unatoa mikopo feki hivyo kama siyo kupotezea watu muda na matumizi mabaya ya rasilimali?

6) Ukosefu wa sera ya soko la ajira binafsi!

Kama kweli tupo makini katika kuliinua soko la ajira binafsi sera zake ziko wapi? Na ni nani aliyezibuni? Tusitegemee "waajiriwa" serikalini watuandalie sera za tasnia ambayo wao wenyewe hawana uzoefu nayo.

7) Migogoro ya ajira haitatuliwi kwa haraka!

Maeneo mengi ya kazi, nguvukazi inazuiwa kufanyakazi kwa sababu ya migogoro ambayo ni mingi na hatujaweza kuweka mfumo wa kuitatua kwa haraka ili kuruhusu nguvukazi iweze kuchangia kwenye pato la taifa. Taratibu za kisheria zilizopo zinakwamisha juhudi za kuwatumia wataalamu wetu vilivyo.

Mwanafunzi anapoyaona haya unafikiri hamu ya kusoma atakuwa nayo kweli?

8) Mitaala kutumika kuua vipaji vya wanafunzi!

Elimu lazima itoe mwanya wa kukuza vipaji vya wanafunzi badala ya sera zilizopo za kuwalazimisha wanafunzi wote kusoma aina moja ya masomo. Yule mwenye ujuzi wa michezo aendelezwe kulingana na vipaji vyake siyo alazimishwe kuacha michezo na kuzama kwenye hisabati, fizikia na kemia ambayo hana kipaji nacho. Yule ambaye amejaaliwa kwenye fani ya muziki, uigizaji, mapishi na elimu nyinginezo ambazo hazifundishwi mashuleni sasa ziingizwe kwenye mitaala na kuendeleza vipaji hivyo.

9) Mitaala iwe na uhusiano na maisha ya kila siku.

Sehemu kubwa ya mambo yanayofundishwa mashuleni hayana uhusiano na changamoto tunazokutana nazo na hivyo kuwa elimu hiyo haimsaidii mhitimu kuweza kumudu maisha na hivyo kumchanganya kabisa. Kwanini mwanafunzi ahangaike na elimu ambayo haimtatulii kero zake za kila siku?

10) Kusisitiza elimu ya juu badala ya elimu ya msingi na ya kati!

Vyuo vingi vya kati vimegeuzwa kuwa vyuo vikuu kama vile kazi nyingi hufanywa na wenye elimu ya chuo kikuu jambo ambalo silo kweli. Sehemu kubwa ya ajira ipo kwenye elimu ya kati badala ya kuongeza vyuo vikuu na bajeti yake msisitizo uwe kwenye elimu ya mikono (Vocational skills) kupitia vyuo vya VETA ambako wahitimu wakitoka wana ujuzi wa kuingia soko la ajira bila ya kuhitaji mafunzo ya ziada.

Kwa kurekebisha haya, utakuta wanafunzi wakijituma kwa sababu motisha wa kufanya vizuri unakuwa uko wazi na kwa kila mtu kuona, wapi anatoka, yuko wapi na anaelekea wapi......................na hakuna kubaguliwa ndiyo misingi ya utu na isipokuwepo wachache sana watakuwa na dhima ya kufanya vizuri na hivyo kukazana...........
 
kuna haja ya kufumua mfumo mzima wa elimu tuanze moja,
vinginevyo wizara ya elimu ifutwe iwe nchi ya kwanza dunia kutokuwa na shule wala vyuo maana.
ni nchi gani duniani wanafunzi wanafundishwa na wanafunzi waliofeli(walimu waliofeli)?????
 
kuna haja ya kufumua mfumo mzima wa elimu tuanze moja,
vinginevyo wizara ya elimu ifutwe iwe nchi ya kwanza dunia kutokuwa na shule wala vyuo maana.
ni nchi gani duniani wanafunzi wanafundishwa na wanafunzi waliofeli(walimu waliofeli)?????

zumbemkuu kipaumbele cha nchi yetu ni siasa sasa tusitegemee kuvuna elimu wakati tumepanda siasa...........ukimlipa mwalimu leo mshahara wa mbunge waalimu safi watapatikana tena kwa kupigania ajira ya ualimu na wako wengi. Lakini sisi tunalea soko la ajira za wanasiasa kwa hiyo tusilalamike kwa kuvuna tulichopanda wenyewe......
 
zumbemkuu kipaumbele cha nchi yetu ni siasa sasa tusitegemee kuvuna elimu wakati tumepanda siasa...........ukimlipa mwalimu leo mshahara wa mbunge waalimu safi watapatikana tena kwa kupigania ajira ya ualimu na wako wengi. Lakini sisi tunalea soko la ajira za wanasiasa kwa hiyo tusilalamike kwa kuvuna tulichopanda wenyewe......
basi kama ni hivyo mashule yote ya msingi, sekondari na vyuo vyte vibadilishwe viwe vyuo vya siasa au kama vipi yale majengo yabadilishwe ziwe nyumba za ibada labda Mungu atatusikia na kukidhi haja zetu..
 
basi kama ni hivyo mashule yote ya msingi, sekondari na vyuo vyte vibadilishwe viwe vyuo vya siasa au kama vipi yale majengo yabadilishwe ziwe nyumba za ibada labda Mungu atatusikia na kukidhi haja zetu..

zumbemkuu kasi ya kushuka elimu itapanda kwa mithili ya pressure...................siasa siyo uzalishaji wa moja kwa moja...............nchi ya namna hiyo huisihia kufilisika kabisa..................
 
kuna haja ya kufumua mfumo mzima wa elimu tuanze moja,
vinginevyo wizara ya elimu ifutwe iwe nchi ya kwanza dunia kutokuwa na shule wala vyuo maana.
ni nchi gani duniani wanafunzi wanafundishwa na wanafunzi waliofeli(walimu waliofeli)?????
Unfortunately siyo rahisi hivyo; mafanikio katika mfumo wa elimu huendana sambamba kabisa na matunda yake. Tulipoanza kuwaheshimu akina dokta fulani walionunua digirii mtandaoni au madokta fulani walioletewa digrii kutoka marekani na watu wawili ambao huko kwao hawatambuliki kabisa ndipo hapo tulipoamua kupeleka elimu yetu pale makaburini kinondoni.

Elimu ni juhudi za mwanafunzi na mwalimu; it is a rewarding effort kwa mwanafunzi na consoling effort kwa mwalimu. Mwaliimu hufarijika sana anapoona mwanafunzi wake kafanikiwa, na mwanafunzi hutumia muda na juhudi nyingi sana kufanikiwa kieleimu kusudi baadaye juhudi zake hizo zithaminiwe na jamii yake. Ingawa mwalimu Nyerere alijua sana maana ya elimu kwa jamii, mwishoni mwa utawala wake kuanzia mwaka 1982 wakati wa msukosuko wa uchumi thamani ya elimu ilianza kushuka sana baada ya kutokuwa rewarding effort kwa wanafunzi, na matokeo yake hata waalimu wakakosa moyo baada ya kugundua kuwa wanafunzi wao walikuwa hawafanikiwi.

Ninashangaa sana kuwa ile kauli mbiu ya elimu ni ufunguo wa mwaisha ilipotea kabisa na Nyerere.

Leo hii elimu halisi hailipi kabisa hapa kwetu kwani ukinunua digrii hata ya udakatri wa kupasua moyo utaula tu; bali ujanja ujanja umeua ndio unaolipa, kwa hiyo sishangai iwapo vijana wetu wakiamua kuwa wajanja wajanja wa kuchora vikatuni kwa vile wanajua huko ndiko kweye maisha. They have one life, and they have to flow with the wind!

Muungano wa Jumuia ya Afrika ya Mashariki utaunda matabaka mazuri sana ya walioandaliwa kuula kutoke sehemu nyingine na wale wa Tanzania waliondaliwa kutumikiwa ndani ya nchi yao.
 
Kuporomoka kwa elimu nchini kwetu, kuna changiwa na vitu vitatu.
1. Serikali
2. Wazazi
3. Mwanafunzi
1. Ninapo sema serikali, nina maanisha mitaala ya ufundishaji na mfumo wa ufundisha sio mzuri, si mfumo wa kufanya mwanafunzi aelewe na afaulu, pili Serikali ime shindwa kutengeza mahusiano mazuri kati yake na walimu.
2. Ninapo sema wazazi, tumejikuta wazazi wengi hawana ukaribu na watoto na hata kujua maendeleo ya watoto wao huko mashuleni pia hata malezi pia ya sasa ivi ni mabovu ambayo yanasabisha hata watoto kua wajinga na wavivu
 
Matokeo yake kwa elimu ya juu ni:

a. Kufungwa kwa vyuo vikuu kwani kutakuwa hakuna wanafunzi wa kuingia chuo kikuu. Pool ya wanafunzi wa kuingia vyuo vikuu itakuwa ndogo sana, hivyo kupelekea vyuo vingi kukosa wateja.

b. Kuchukuwa wanafunzi wasiostahili, wasio na sifa za kuingia vyuo vikuu. Hii ni hatari kuliko maelezo. Ni heri vyuo vifungwe tu kuliko kupokea wanafunzi wasiostahili.

c. Vyuo vikuu kuanza kutoa elimu ya viwango vya cheti na diploma kwa wingi. Nafahamu kuna vyuo vikuu vinatoa elimu kwa viwango hivyo. Lakini matokeo ya aina hii, yatavifanya vyuo vikuu viongeze huduma za elimu za cheti na diploma. Pengine kila idara itabidi itoe elimu za cheti na diploma. Vinginevyo, vyuo vitafungwa na maelfu ya wanataaluma kuwa jobless!!

Ni hatari na balaa!

Hili jambo linahitaji kuundwa kwa tume ya wataalamu (technocrats committee) na si tume ya wanasiasa. Wataalamu wapewe jukumu la kuchambua mfumo mzima wa elimu yetu. Haswa ya msingi na sekondari; mambo yakiwa mazuri huko chini, huku juu kwenye vyuo vikuu, mambo nayo yanakuwa mazuri.

Oh! Lakini kwa upande mwingine, mbona taasisi nyingi sana (HakiElimu, Twaweza n.k.) zimefanya tafiti na kuja na mapendekezo mengi mno na mazuri sana ya kuboresha mfumo wa elimu yetu?

Oh yes! Kumbe tatizo siyo kutokuwepo kwa ushauri wa kitaalamu. Tatizo ni ubichwa ngumu wa serikali ya CCM.

Suluhisho kumbe ni kuipumzisha serikali hii; serikali hii ndiyo imesababishwa ubovu kwenye mfumo wetu wa elimu. Na hakika serikali hii hii haiwwzi kuwa na majibu na masuluhisho.

Ni hayo tu.
 
Very simple, "elimu yetu" inazidi kushuka thamani na itaendelea kushuka thamani kwa sababu hii tunayoiita elimu is not our product, hatujui maana ya Elimu na haisadifu mazingira na wakati wetu na kikubwa zaidi inakinzana na tamaduni zetu.

Kwa upuuzi tu tunaweza kusema kwamba kushuka au kupanda kwa kiwango cha elimu ni kuangalia matokeo ya shule ya msingi, kidato cha nne na cha sita. Lakini hichi sio kipimo sahihi neither is kuangalia upatikanaji wa ajira na vitu vinavyohusiana na hilo kwa wahitimu wa viwango mbalimbali vya elimu, kwani lengo la elimu ni kumpatia mtu ajira? Kama unafikiria hivyo then bado hujaELIMIKA.

Kuna ulazima wa kuwa na mjadala wa ELIMU ni nini, manufaa na kazi za ELIMU ni yapi or else tutakua tunajadili kitu tusichokua na uhakika nacho au mbaya zaidi kutokijua kabisa.

Na naomba kuacha swali hapa, Elimu ni nini? Manufaa yake ni nini?
 
Unfortunately siyo rahisi hivyo; mafanikio katika mfumo wa elimu huendana sambamba kabisa na matunda yake. Tulipoanza kuwaheshimu akina dokta fulani walionunua digirii mtandaoni au madokta fulani walioletewa digrii kutoka marekani na watu wawili ambao huko kwao hawatambuliki kabisa ndipo hapo tulipoamua kupeleka elimu yetu pale makaburini kinondoni.

Elimu ni juhudi za mwanafunzi na mwalimu; it is a rewarding effort kwa mwanafunzi na consoling effort kwa mwalimu. Mwaliimu hufarijika sana anapoona mwanafunzi wake kafanikiwa, na mwanafunzi hutumia muda na juhudi nyingi sana kufanikiwa kieleimu kusudi baadaye juhudi zake hizo zithaminiwe na jamii yake. Ingawa mwalimu Nyerere alijua sana maana ya elimu kwa jamii, mwishoni mwa utawala wake kuanzia mwaka 1982 wakati wa msukosuko wa uchumi thamani ya elimu ilianza kushuka sana baada ya kutokuwa rewarding effort kwa wanafunzi, na matokeo yake hata waalimu wakakosa moyo baada ya kugundua kuwa wanafunzi wao walikuwa hawafanikiwi.

Ninashangaa sana kuwa ile kauli mbiu ya elimu ni ufunguo wa mwaisha ilipotea kabisa na Nyerere.

Leo hii elimu halisi hailipi kabisa hapa kwetu kwani ukinunua digrii hata ya udakatri wa kupasua moyo utaula tu; bali ujanja ujanja umeua ndio unaolipa, kwa hiyo sishangai iwapo vijana wetu wakiamua kuwa wajanja wajanja wa kuchora vikatuni kwa vile wanajua huko ndiko kweye maisha. They have one life, and they have to flow with the wind!

Muungano wa Jumuia ya Afrika ya Mashariki utaunda matabaka mazuri sana ya walioandaliwa kuula kutoke sehemu nyingine na wale wa Tanzania waliondaliwa kutumikiwa ndani ya nchi yao.

Kichuguu Ni kweli elimu feki itatumaliza
 
Kuporomoka kwa elimu nchini kwetu, kuna changiwa na vitu vitatu.
1. Serikali
2. Wazazi
3. Mwanafunzi
1. Ninapo sema serikali, nina maanisha mitaala ya ufundishaji na mfumo wa ufundisha sio mzuri, si mfumo wa kufanya mwanafunzi aelewe na afaulu, pili Serikali ime shindwa kutengeza mahusiano mazuri kati yake na walimu.
2. Ninapo sema wazazi, tumejikuta wazazi wengi hawana ukaribu na watoto na hata kujua maendeleo ya watoto wao huko mashuleni pia hata malezi pia ya sasa ivi ni mabovu ambayo yanasabisha hata watoto kua wajinga na wavivu

Ishmael kwenye mazingira yaliyopo mwanafunzi lawama zake zinatokea wapi? Kumbuka hata chakula huwa hali ipasavyo
 
Matokeo yake kwa elimu ya juu ni:

a. Kufungwa kwa vyuo vikuu kwani kutakuwa hakuna wanafunzi wa kuingia chuo kikuu. Pool ya wanafunzi wa kuingia vyuo vikuu itakuwa ndogo sana, hivyo kupelekea vyuo vingi kukosa wateja.

b. Kuchukuwa wanafunzi wasiostahili, wasio na sifa za kuingia vyuo vikuu. Hii ni hatari kuliko maelezo. Ni heri vyuo vifungwe tu kuliko kupokea wanafunzi wasiostahili.

c. Vyuo vikuu kuanza kutoa elimu ya viwango vya cheti na diploma kwa wingi. Nafahamu kuna vyuo vikuu vinatoa elimu kwa viwango hivyo. Lakini matokeo ya aina hii, yatavifanya vyuo vikuu viongeze huduma za elimu za cheti na diploma. Pengine kila idara itabidi itoe elimu za cheti na diploma. Vinginevyo, vyuo vitafungwa na maelfu ya wanataaluma kuwa jobless!!

Ni hatari na balaa!

Hili jambo linahitaji kuundwa kwa tume ya wataalamu (technocrats committee) na si tume ya wanasiasa. Wataalamu wapewe jukumu la kuchambua mfumo mzima wa elimu yetu. Haswa ya msingi na sekondari; mambo yakiwa mazuri huko chini, huku juu kwenye vyuo vikuu, mambo nayo yanakuwa mazuri.

Oh! Lakini kwa upande mwingine, mbona taasisi nyingi sana (HakiElimu, Twaweza n.k.) zimefanya tafiti na kuja na mapendekezo mengi mno na mazuri sana ya kuboresha mfumo wa elimu yetu?

Oh yes! Kumbe tatizo siyo kutokuwepo kwa ushauri wa kitaalamu. Tatizo ni ubichwa ngumu wa serikali ya CCM.

Suluhisho kumbe ni kuipumzisha serikali hii; serikali hii ndiyo imesababishwa ubovu kwenye mfumo wetu wa elimu. Na hakika serikali hii hii haiwwzi kuwa na majibu na masuluhisho.

Ni hayo tu.

Nzi matokeo mabaya ya chini hayawezi kufunga vyuo vikuu ambavyo lazima vitawapasisha ili kupata mgawo wake kutoka serikalini...........kwa hiyo "garbage in, garbage out...."
 
kuna haja ya kuangalia suala hili kwa upana wake kwanza kwa mpokea elimu mwenyewe au client jee anaipokeaje?? pili kwa mtoa elimu kwa maana ya serikali na tatu kwa msimamizi wa elimu hiyo ambae pia ni serikali na mzazi.. tatizo la kushuka kwa elimu limechangiwa sana na wazazi kutozingatia malezi bora ya watoto hasa kumsimamia mtoto kwa ukaribu pili nidhamu ya watoto imekuwa mbaya sana.
 
Very simple, "elimu yetu" inazidi kushuka thamani na itaendelea kushuka thamani kwa sababu hii tunayoiita elimu is not our product, hatujui maana ya Elimu na haisadifu mazingira na wakati wetu na kikubwa zaidi inakinzana na tamaduni zetu.

Kwa upuuzi tu tunaweza kusema kwamba kushuka au kupanda kwa kiwango cha elimu ni kuangalia matokeo ya shule ya msingi, kidato cha nne na cha sita. Lakini hichi sio kipimo sahihi neither is kuangalia upatikanaji wa ajira na vitu vinavyohusiana na hilo kwa wahitimu wa viwango mbalimbali vya elimu, kwani lengo la elimu ni kumpatia mtu ajira? Kama unafikiria hivyo then bado hujaELIMIKA.

Kuna ulazima wa kuwa na mjadala wa ELIMU ni nini, manufaa na kazi za ELIMU ni yapi or else tutakua tunajadili kitu tusichokua na uhakika nacho au mbaya zaidi kutokijua kabisa.

Na naomba kuacha swali hapa, Elimu ni nini? Manufaa yake ni nini?

Elimu ni nyenzo ambazo mwenye nazo humrahisishia uwezo wa kuyamudu maisha na pia kuwarahisishia jamii inayomzunguka
 
kuna haja ya kuangalia suala hili kwa upana wake kwanza kwa mpokea elimu mwenyewe au client jee anaipokeaje?? pili kwa mtoa elimu kwa maana ya serikali na tatu kwa msimamizi wa elimu hiyo ambae pia ni serikali na mzazi.. tatizo la kushuka kwa elimu limechangiwa sana na wazazi kutozingatia malezi bora ya watoto hasa kumsimamia mtoto kwa ukaribu pili nidhamu ya watoto imekuwa mbaya sana.

mtz one mzazi mwenyewe hana uwezo wa kuinjika maharagwe kwenye mafiga matatu sasa kama hayo hawezi ya mtoto atayawezea wapi? Bila kuimarika uchumi wa familia tutaendelea kuwalaumu wazazi bureeeeeeeeee
 
Unfortunately siyo rahisi hivyo; mafanikio katika mfumo wa elimu huendana sambamba kabisa na matunda yake. Tulipoanza kuwaheshimu akina dokta fulani walionunua digirii mtandaoni au madokta fulani walioletewa digrii kutoka marekani na watu wawili ambao huko kwao hawatambuliki kabisa ndipo hapo tulipoamua kupeleka elimu yetu pale makaburini kinondoni.

Elimu ni juhudi za mwanafunzi na mwalimu; it is a rewarding effort kwa mwanafunzi na consoling effort kwa mwalimu. Mwaliimu hufarijika sana anapoona mwanafunzi wake kafanikiwa, na mwanafunzi hutumia muda na juhudi nyingi sana kufanikiwa kieleimu kusudi baadaye juhudi zake hizo zithaminiwe na jamii yake. Ingawa mwalimu Nyerere alijua sana maana ya elimu kwa jamii, mwishoni mwa utawala wake kuanzia mwaka 1982 wakati wa msukosuko wa uchumi thamani ya elimu ilianza kushuka sana baada ya kutokuwa rewarding effort kwa wanafunzi, na matokeo yake hata waalimu wakakosa moyo baada ya kugundua kuwa wanafunzi wao walikuwa hawafanikiwi.

Ninashangaa sana kuwa ile kauli mbiu ya elimu ni ufunguo wa mwaisha ilipotea kabisa na Nyerere.

Leo hii elimu halisi hailipi kabisa hapa kwetu kwani ukinunua digrii hata ya udakatri wa kupasua moyo utaula tu; bali ujanja ujanja umeua ndio unaolipa, kwa hiyo sishangai iwapo vijana wetu wakiamua kuwa wajanja wajanja wa kuchora vikatuni kwa vile wanajua huko ndiko kweye maisha. They have one life, and they have to flow with the wind!

Muungano wa Jumuia ya Afrika ya Mashariki utaunda matabaka mazuri sana ya walioandaliwa kuula kutoke sehemu nyingine na wale wa Tanzania waliondaliwa kutumikiwa ndani ya nchi yao.

Nakuunga mkono.-
Mchango wangu.

Kuporomoka kwa elimu ni moja kati ya matokeo au one of the End Results za failure as a Nation.

Elimu sio sekta pekee ambayo iko hali mbaya, kila kitu Tanzania kiko hali
Mbaya na kimeharibika. Ukitaka kujidhibitisha, wakati huu huu tunalalamika elimu imeporomoka baada ya kupata majibu ya Form 4, umoja wetu wakitaifa na amani iliyokuwa tunajjvunia nayo ipo hatiani na machafuko ya kidini kiasi mpka nchi za nje wanakuja kutusaidia kumaliza matatizo yetu wenyewe.

kuporomoka kwa kiwango cha elimu inaweza kutokana na sababu nyingi sana ambazo kila mtu anauwezo wa kuorodhesha. Lakini sababu hizi karibia zote ni minor problems ambazo hata nchi zilizoendelea wanazo. Sababu kuu kuliko (the root problem) ya kushuka kwa kiwango cha elimu wengi wetu hatuijui bado, tunahangaika huko na huko kuitafuta. Tutasema yote ili mradi kujiaminisha kuwa hili ndo tatizo lililopelekea watoto wetu kufeli.

Mimi nasema ni mmoja ya watu wachache ambao naamini tatizo la kuanguka kiwango cha elimu ni kushindwa kwetu kama Taifa.-

Sasa tutapo jitambua kama taifa ni jinsi gani tumefeli ndio hapo tutaanza kuona mabadiliko.-

Hii ni mwanzo tu, mwakani watoto watafeli tena wengi tu, kwasababu wengi wa form three wa hizi shule face matatizo yale yale ya form 4 waliopita (mfano shule ambayo haikuwa na walimu mwaka jana unafikiri wakipata mwalimu mwakani wataweza kuwafaulisha hao watoto)

Hakuwezi kuwa na mabadiliko katika mwaka mmoja. So mwakani wasipochakachua majibu watoto watafeli kama mwaka huu.
 
Sasa imefika wakati wa kuandamana ili Lazima Serkali IWEKEZE kwenye ELIMU! Kama ilivyokuwa zama zile za kilimo cha kufa na kupona!
 
Sujaona sababu ya msingi ya serikali kuunda tume. Matatizo wanayajua vizuri sana. Wakitaka majibu mazuri wakamwone mama Sitta. Anajua vizuri sana
 
I think we shouldn't blame the government at all. If education is a matter of national urgency, we, the people, should do more. Take for example this thread, it ended just a week after the results were announced with less than 20 posts. The question is if concerned citizens aren't taking the their issues very seriously, why the government should try to help them?

Anyway, we reap what we sow. It's simple as that. The education system in Tanzania was design to increase the number of enrollment not the quality. For example, in 70s, the number of primary students enrolled in primary schools increased from 35% to 90%. Today, the number of secondary school students is more than 100,000, compared to approximately 20,000 in 90s.

All of these initiatives to increase the number of students in primary and secondary schools were launched when we knew that there weren't enough teachers and other resources to empower students. So we shouldn't be surprised with the results because they are of our own making.
 
Sujaona sababu ya msingi ya serikali kuunda tume. Matatizo wanayajua vizuri sana. Wakitaka majibu mazuri wakamwone mama Sitta. Anajua vizuri sana

Everybody know what's the problem. The examinations cover what students are expected to learn during their four years of secondary education. Yet, many students aren't well prepared to attend secondary school education. What's worse, the secondary schools they attend aren't schools at all.

If we can't admit that everybody of us knows the problem, we are in state of denial.
 
Back
Top Bottom