Kwanini ELIMU yetu inaendelea kushuka thamani kila kukicha?

Kwanini ELIMU yetu inaendelea kushuka thamani kila kukicha?

Nimeandika makala haya kwenye gazeti la Kiongozi toleo la jana Ijumaa. Ninaamini litaongeza chachu ya mjadala huu kuhusu elimu.

Makala iliyopita nilimaliza kwa kusema kwamba leo tutaona namna ya kufanya ili kuokoa maisha ya watoto waliofeli. Itakumbukwa kwamba tulizungumzia kuhusu dhana ya nchi kufaidika na uwepo wa vijana wengi (demograpic dividend) ama kupata hasara iwapo Taifa halikuandaa nguvu kazi hiyo kuzalisha mali na kuendeleza nchi (demographic bomb). Nimeona leo niandike tufanye nini kuhusu Elimu yetu.

Napenda kuwajulisha wasomaji wangu kwamba Jimbo langu la Uchaguzi ni moja ya majimbo ambayo yamefanya vibaya sana katika matokeo ya kidato cha nne. Nimekuwa nina msongo mkubwa sana wa mawazo baada ya matokeo hayo. Katika watoto 1329 wa Jimbo la Kigoma Kaskazini waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012, hakuna aliyepata daraja la kwanza, 5 walipata daraja la pili, 14 walipata daraja la tatu na waliosalia walipata daraja la nne na sifuri. Asilimia 98.6 ya watoto wote walipata alama hizo za mwisho. Hayo ndio matokeo kutoka katika shule 14 za kata katika Jimbo ambalo mbunge kama mimi ninayezungumzwa nchi nzima natokea. Aibu kubwa sana.

Lawama za matokeo haya ni kwa Watanzania wote lakini uwajibikaji ni wa wasimamizi wa Elimu maana wazazi, asasi za kiraia na hata wabunge wamekuwa kila wakati wakisema kuwa ni lazima tuboreshe elimu yetu. Serikali imekuwa ikificha kichwa chini ya mchanga ikiamini kuwa kiwiliwili hakionekani, madhara yake ndio haya tunaona hivi sasa kuhusu suala la Elimu na matokeo ya kidato cha nne.

Waziri wa Elimu ndugu Shukuru Kawambwa (nashangaa sana kwanini bado ni Waziri mpaka hivi sasa) alisema kwamba tatizo kubwa ni kwamba hakuna walimu wa kutosha. Kinyume chake kabisa hivi sasa kuna walimu wengi sana nchini kiasi cha kuvuka malengo ya mkukuta ya mwalimu 1 kwa kila wanafunzi 40 (1:40). Takwimu zinaonyesha kuwa hivi sasa nchini kuna walimu wa kumwaga kiasi cha baadhi ya mikoa kuwa na uwiano wa mwalimu 1 kwa kila wanafunzi 21. Wastani wa sasa kitaifa ni 1:35. Tatizo ni nini sasa? Moja walimu wamegawanywa kwa mikoa kadhaa na maeneo ya mijini ihali maeneo ya vijijni hayana walimu. Ndio maana shule za vijijini zimefelisha zaidi kuliko shule za mijini. Pili walimu hawa hawana motisha ya kufundisha na hivyo kiukweli hawatoi elimu kabisa kwa watoto.

Waziri anasema sababu za watoto kufeli sana ni kutokuwa na maabara za kutosha. Hili ni kweli kwa masomo ya sayansi lakini sio kwa kweli kwa masomo kama kiswahili, hesabu, kiingereza, historia nk. Watoto asilimia 60 wameshindwa masomo haya pia ambayo hayana mahusiano yeyote na uwepo wa maabara. Kwa hiyo kuna tatizo la ziada kuhusu elimu na ufundishaji. Sasa kama sababu zote za kufeli hazina maana nini kifanyike?

Kuna sababu ambayo imesemwa sana wachambuzi wa mambo, kwamba Bajeti ya Elimu ni ndogo na hivyo ndio maana matokeo yanakuwa mabaya sana. Inawezekana ikawa hivyo kama tunaangalia kwa undani sana bajeti ya elimu. Lakini hebu tuone Bajeti ya Elimu kwa miaka kadhaa ya nyuma na kulinganisha na matokeo ya kidato cha elimu. Mwaka 2008/09 Bajeti ya Elimu ilikuwa asilimia 20 ya Bajeti yote ya nchi na hivi sasa ni asilimia 17. Bajeti ya Elimu ya Sekondari imeongezeka kutoka shilingi 137 bilioni mpaka 509 bilioni kati ya mwaka 2008/09 mpaka 2012/13. Hata hivyo matokeo yameporomoka kwa asilimia 34. Yaani kuna mahusiano hasi kati ya kuongezeka bajeti ya Elimu na matokeo ya watoto wetu. Sasa kama bajeti inaongezeka, walimu wapo na masomo ya historia nk hayahitaji maabara nini kimefelisha watoto wetu? Mazingira ya kufundishia na kujifunza na usimamizi wa Elimu ndio chanzo cha watoto kufeli mitihani. Nitaeleza kidogo na kisha kutoa majawabu.

Walimu wengi wanaopangwa shule za vijijini hawaendi kwa sababu ya ugumu wa maisha huko. Hii ni pamoja na kuwa mwalimu wa mjini na wa kijijini wote wanalipwa mshahara sawa licha ya mazingira magumu ya mwalimu wa kijijini. Hivyo Mwalimu anakuwa hana motisha kabisa ya kufundisha na wakati mwingine wala hahudhurii darasani. Mazingira ya walimu kufundishia ni mabaya na bajeti kubwa ya elimu haielekezwi katika eneo hili. Ukitazama Bajeti ya Tanzania utaona kuwa sehemu kubw ya Bajeti inaelekezwa kwenye matumizi ya kawaida kuliko matumizi ya maendeleo. Mwaka 2011/12 kwa mfano, asilimia 10.2% ya bajeti ndio ilikuwa ya maendeleo. Katika mazingira kama haya ni vigumu sana kuweka mazingira mazuri ya walimu kufundisha. Hali hii pia haitoi motisha kwa wanafunzi kusoma maana wanahitaji mazingira bora ikiwemo uwepo wa vitabu na vifaa vinginw vya kusomea.

Mjadala wa mishahara ya walimu ni mjadala usioisha. Kiukweli kama tunataka kuboresha elimu ni lazima tutoe upendeleo wa kipekee wa kada ya walimu katika mishahara. Hivi sasa Mwalimu mwenye cheti anayeanza kufundisha analipwa tshs 240,000 kwa mwezi, wa diploma analipwa tshs 375,000 na mwenye shahada tshs 469,000. Kwanza ni vema tuanze mpango maalumu wa kuhakikisha kuwa walimu wote nchini waanzie diploma na kuendelea. Pili mishahara ya walimu ipandishwe kwa asilimia 50 na tuwape motisha nyingine kama posho za nyumba na posho maalumu kwa kuwa Walimu ili kudhibiti ugumu maisha. Vile vile tuwe na mfumo tofauti wa kodi ya mapato kwa walimu ambapo tuseme kuwa kodi PAYE kwa walimu iwe ni asilimia 5 ya mshahara. Walimu wenye elimu kubwa zaidi na wenye ujuzi maalumu wafutiwe kodi kabisa ili kutoa motisha kwa watu wenye ufaulu mzuri kuingia kufundisha badala ya sasa ambapo ualimu unaonekana kama fani ya waliofeli.

Ni maoni yangu kwamba hivi sasa taifa lijielekeze kwenye kuimarisha hadhi ya mwalimu kwa kumlipa vizuri, kumwekea mazingira mazuri ya kufundisha na kumpa vifaa vya kutosha na hasa vitabu. Mipango yote ya elimu imweke mwalimu na mwanafunzi katikati.
 
Mkiweza kupata Hotuba ya Mwalimu Nyerere aliyoitoa katika Chuo cha Ualimu Morogoro muisome. 'The Power of Teachers' - Nyerere, Morogoro Teachers' College 27th August 1966

"...... teachers can make or ruin our society....."
 
Nimeandika makala haya kwenye gazeti la Kiongozi toleo la jana Ijumaa. Ninaamini litaongeza chachu ya mjadala huu kuhusu elimu.

Makala iliyopita nilimaliza kwa kusema kwamba leo tutaona namna ya kufanya ili kuokoa maisha ya watoto waliofeli. Itakumbukwa kwamba tulizungumzia kuhusu dhana ya nchi kufaidika na uwepo wa vijana wengi (demograpic dividend) ama kupata hasara iwapo Taifa halikuandaa nguvu kazi hiyo kuzalisha mali na kuendeleza nchi (demographic bomb). Nimeona leo niandike tufanye nini kuhusu Elimu yetu.

Napenda kuwajulisha wasomaji wangu kwamba Jimbo langu la Uchaguzi ni moja ya majimbo ambayo yamefanya vibaya sana katika matokeo ya kidato cha nne. Nimekuwa nina msongo mkubwa sana wa mawazo baada ya matokeo hayo. Katika watoto 1329 wa Jimbo la Kigoma Kaskazini waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012, hakuna aliyepata daraja la kwanza, 5 walipata daraja la pili, 14 walipata daraja la tatu na waliosalia walipata daraja la nne na sifuri. Asilimia 98.6 ya watoto wote walipata alama hizo za mwisho. Hayo ndio matokeo kutoka katika shule 14 za kata katika Jimbo ambalo mbunge kama mimi ninayezungumzwa nchi nzima natokea. Aibu kubwa sana.

Lawama za matokeo haya ni kwa Watanzania wote lakini uwajibikaji ni wa wasimamizi wa Elimu maana wazazi, asasi za kiraia na hata wabunge wamekuwa kila wakati wakisema kuwa ni lazima tuboreshe elimu yetu. Serikali imekuwa ikificha kichwa chini ya mchanga ikiamini kuwa kiwiliwili hakionekani, madhara yake ndio haya tunaona hivi sasa kuhusu suala la Elimu na matokeo ya kidato cha nne.

Waziri wa Elimu ndugu Shukuru Kawambwa (nashangaa sana kwanini bado ni Waziri mpaka hivi sasa) alisema kwamba tatizo kubwa ni kwamba hakuna walimu wa kutosha. Kinyume chake kabisa hivi sasa kuna walimu wengi sana nchini kiasi cha kuvuka malengo ya mkukuta ya mwalimu 1 kwa kila wanafunzi 40 (1:40). Takwimu zinaonyesha kuwa hivi sasa nchini kuna walimu wa kumwaga kiasi cha baadhi ya mikoa kuwa na uwiano wa mwalimu 1 kwa kila wanafunzi 21. Wastani wa sasa kitaifa ni 1:35. Tatizo ni nini sasa? Moja walimu wamegawanywa kwa mikoa kadhaa na maeneo ya mijini ihali maeneo ya vijijni hayana walimu. Ndio maana shule za vijijini zimefelisha zaidi kuliko shule za mijini. Pili walimu hawa hawana motisha ya kufundisha na hivyo kiukweli hawatoi elimu kabisa kwa watoto.

Waziri anasema sababu za watoto kufeli sana ni kutokuwa na maabara za kutosha. Hili ni kweli kwa masomo ya sayansi lakini sio kwa kweli kwa masomo kama kiswahili, hesabu, kiingereza, historia nk. Watoto asilimia 60 wameshindwa masomo haya pia ambayo hayana mahusiano yeyote na uwepo wa maabara. Kwa hiyo kuna tatizo la ziada kuhusu elimu na ufundishaji. Sasa kama sababu zote za kufeli hazina maana nini kifanyike?

Kuna sababu ambayo imesemwa sana wachambuzi wa mambo, kwamba Bajeti ya Elimu ni ndogo na hivyo ndio maana matokeo yanakuwa mabaya sana. Inawezekana ikawa hivyo kama tunaangalia kwa undani sana bajeti ya elimu. Lakini hebu tuone Bajeti ya Elimu kwa miaka kadhaa ya nyuma na kulinganisha na matokeo ya kidato cha elimu. Mwaka 2008/09 Bajeti ya Elimu ilikuwa asilimia 20 ya Bajeti yote ya nchi na hivi sasa ni asilimia 17. Bajeti ya Elimu ya Sekondari imeongezeka kutoka shilingi 137 bilioni mpaka 509 bilioni kati ya mwaka 2008/09 mpaka 2012/13. Hata hivyo matokeo yameporomoka kwa asilimia 34. Yaani kuna mahusiano hasi kati ya kuongezeka bajeti ya Elimu na matokeo ya watoto wetu. Sasa kama bajeti inaongezeka, walimu wapo na masomo ya historia nk hayahitaji maabara nini kimefelisha watoto wetu? Mazingira ya kufundishia na kujifunza na usimamizi wa Elimu ndio chanzo cha watoto kufeli mitihani. Nitaeleza kidogo na kisha kutoa majawabu.

Walimu wengi wanaopangwa shule za vijijini hawaendi kwa sababu ya ugumu wa maisha huko. Hii ni pamoja na kuwa mwalimu wa mjini na wa kijijini wote wanalipwa mshahara sawa licha ya mazingira magumu ya mwalimu wa kijijini. Hivyo Mwalimu anakuwa hana motisha kabisa ya kufundisha na wakati mwingine wala hahudhurii darasani. Mazingira ya walimu kufundishia ni mabaya na bajeti kubwa ya elimu haielekezwi katika eneo hili. Ukitazama Bajeti ya Tanzania utaona kuwa sehemu kubw ya Bajeti inaelekezwa kwenye matumizi ya kawaida kuliko matumizi ya maendeleo. Mwaka 2011/12 kwa mfano, asilimia 10.2% ya bajeti ndio ilikuwa ya maendeleo. Katika mazingira kama haya ni vigumu sana kuweka mazingira mazuri ya walimu kufundisha. Hali hii pia haitoi motisha kwa wanafunzi kusoma maana wanahitaji mazingira bora ikiwemo uwepo wa vitabu na vifaa vinginw vya kusomea.

Mjadala wa mishahara ya walimu ni mjadala usioisha. Kiukweli kama tunataka kuboresha elimu ni lazima tutoe upendeleo wa kipekee wa kada ya walimu katika mishahara. Hivi sasa Mwalimu mwenye cheti anayeanza kufundisha analipwa tshs 240,000 kwa mwezi, wa diploma analipwa tshs 375,000 na mwenye shahada tshs 469,000. Kwanza ni vema tuanze mpango maalumu wa kuhakikisha kuwa walimu wote nchini waanzie diploma na kuendelea. Pili mishahara ya walimu ipandishwe kwa asilimia 50 na tuwape motisha nyingine kama posho za nyumba na posho maalumu kwa kuwa Walimu ili kudhibiti ugumu maisha. Vile vile tuwe na mfumo tofauti wa kodi ya mapato kwa walimu ambapo tuseme kuwa kodi PAYE kwa walimu iwe ni asilimia 5 ya mshahara. Walimu wenye elimu kubwa zaidi na wenye ujuzi maalumu wafutiwe kodi kabisa ili kutoa motisha kwa watu wenye ufaulu mzuri kuingia kufundisha badala ya sasa ambapo ualimu unaonekana kama fani ya waliofeli.

Ni maoni yangu kwamba hivi sasa taifa lijielekeze kwenye kuimarisha hadhi ya mwalimu kwa kumlipa vizuri, kumwekea mazingira mazuri ya kufundisha na kumpa vifaa vya kutosha na hasa vitabu. Mipango yote ya elimu imweke mwalimu na mwanafunzi katika
Zitto,
Rejea maoni ya umoja wa walimu Mkoa Mpya wa Katavi naungana na sababu walizotoa wao. Mtazamo wangu katika elimu nchini licha ya kutoa mada kadhaa hapa JF ni kama ifuatavyo:

Walimu
Migogoro ya walimu na serikali isiyo isha na wanaoshinda vivulini kama wabunge na watumishi wengine wa serikali kuzidi kujineemesha kwa kutajirishwa hata kwa kukigeuza kiti aangalie upande mwingine analipwa wakati mwalimu matumizi ya kikazi anayatoa mfukoni na mshahara wake ni sawa na kifuta jasho badala ya kujikimu kimaisha.

Wanataaluma hawapewi haki, heshima na malipo stahiki na matokeo yake wanakimbilia kwenye siasa kwenye malipo mazuri. Hii hufanya walimu wawe na
inferiority complex isiyokoma
kiutendaji katika julumu lao la kulielimisha taifa la kesho, serikali inazidi kuwakandamiza na kuwapa vitisho wanapodai haki zao za msingi, matokeo ndio sasa tunayaona. Hili jambo hatuwezi kuwanyooshea vidole walimu moja kwa moja, tunakuja kuona shule binafsi zinafanya vizuri kwa sababu waajiri wao wanawajali wanataaluma hawa.

Bajeti ya Wizara ya Elimu
Nisingependa kukubaliana na hoja hii kwa maana kwamba wizara inaendelea vizuri na watumishi kulipwa mishahara. Mbaya zaidi makongamano na semina haziishi ndiko zinakoishia pesa za bajeti. Mfano Taasisi ya Elimu Mwenge kumekuwa na semina nyingi sananashangaa semina hizo zilikuwa za nini kama vitaala mashuleni ni taabu.

Taasisi ya Elimu ina majengo yake pale Mikocheni na Mwenge na ukumbi mkubwa pale Mwenge, lakini utaona wanaondoka pale na kwenda kuishi mahotelini kwa wiki kadhaa au mwezi kufanya semina na mikutano waka wajumbe wote ni wote ni wale watumishi wanatoka Mikocheni na Mwenge makao makuu Dar, huko ni kula pesa za umma.

Mkurugenzi wa Taasisi ya elimu inasemekana amekuwa mlaji mzuri sana wa pesa za Taasisi. Mwenyewe nimewahi kukutana naye pale ofisini na kumwuliza maswali kadhaa kuhusu uduni wa mitaala mashuleni na mabadiliko ya mara kwa mara yanayo athiri msingi endelevu wa mfumo wa elimu nchini, alicho nijibu ni kwamba hata yeye hana ubavu maana walio juu yake hakuna anayeonekana ana uchungu na Taasisi anayoiendesha, Jibu kama hilo linaonyesha hali halisi ya uongozi na wala si pajeti.​

Mfumo wa utunzi mitihani wa kumkomoa mwanafunzi
Kumkomoa mwanafunzi kutungiwa mtihani kuulizwa maswali kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne, wakati alishafanya mtihani kidato cha pili na akapita. Wanafunzi wahitimu O'leve wanatakiwa kutungiwa mitihani ya kuhitimu O'Level kwa miaka miwili ya mwisho yaani kidato cha tatu na cha nne, maana kidato kwa kwanza na cha pili walishafanya mitihani inayotambuliwa kitaifa na baraza la mitihani. Kwa maneno mengine ni kuwatahini mara mbili kwa kurudia kuwapa maswali ya kitado cha kwanza na cha pili ni kupanua wigo wa ukubwa wa mitihani usio muhimu na kuwaongezea mzigo mzito mno kwa kuwafanya wawe na uwanja mkubwa mno wa kujiandaa kwa mitihani. Ndivyo mfumo wa mitihani kwa mataifa makubwa duniani wanavyofanya, labda sina hakika sana na mfumo wa Uingereza ambao labda tunauiga.​

Mitaala
Kubadilikabadilika kwa mfumo wa mitaala mara kwa mara huathiri wanafunzi na walimu. Uimara wa elimu ni pale mfumo unapokuwa endelevu usiobadilikabadilika. Kinachosemwa mitaala iliyopo si mitaala bali ni majarida ya majaribio ya kutengeneza mitaala kazi ambayo miaka nenda rudi haikamiliki.​

Michezo Mashuleni
Michezo ni sehemu muhimu ya elimu kwa wanafunzi, maana husaidia si kwa afya tu, bali pia kisaikolojia na kiakili. Kufutwa kwa michezo mashuleni kumesababisha wanafunzi kuwa wadumafu katika akili zao, maana baada ya kuchoka madarasani hawana kitu cha kuwachangamsha kiakili na kimwili, matokeo ni kuishia mitandaoni kulonga mapenzi. Wanafunzi wakiwa na ratiba za michezo, baada ya masomo wakienda michezoni hurudi wamechoka ni kupumzika maana mwili umechoka. Lakini bila kuuchosha mwili kwa michezo silika huwaamsha na maungo ya mwili kuwadai ndio udhaifu wa ngono kujitokeza kitu ambacho kinawaathiri kimasomo badala ku-browse elimu wao ni ku-browse mambo ya ufuska.

Shule huwa chimbuko la wanamichezo mahiri duniani na wawapo shuleni huibua vipaji vya michezo, miziki nk. Wanamichezo waliopitia shuleni hufundishika kuliko wa mitaani wasiopitia shule. Kiwango duni cha michezo nchini kimetokana na kufutwa michezo nchini na hivyo kupata wanamichezo mitaani wasio na elimu na uwezo wa kufuata maelekezo na vielelezo wapewavyo na wataalamu na hivyo kubaki taifa kuwa kichwa cha mwendawazimu kuendelea mataifa mengine kujifunzia kunyoa.

Sekondari za kata ndio bomu lalipuka
Maandalizi duni ya uanzishwaji wa shule za kata ndio matokeo yake. Sawa na kuzaa watoto wengi wakati huna uwezo na nguvu za kumudu kuwalea. Shule hazina walimu, hakuna vitabu, hakuna maabara, na mengineyo, sasa tutegemee nini kwa watoto hawa? Kosa kubwa limefanyika kwa kufikiria jambo na kulitenda kinadharia zaidi badala ya kupima uwezo na uendeshwaji wake. Hapa serikali imefanya kufuru kubwa mno.​

Sekondari nyingi za kata zilitakiwa ziwe vyuo vya ufundi stadi
Elimu ya wanafunzi wengi wanayoipata shule za sekondari za kati si ya kiwango cha kuwafanya waishi kwa kujitegemea, bali kuna kitu kinachokosekana kuwajengea uwezo wa kujitegemea. Kuendekeza mfumo wa elimu jumla isiyowapa watu ajira wala kuwapa uwezo wa ubunifu wa kuendesha maisha ni kutokana na hizi shule za kata kuwa za utoaji elimu jumla tu. Jambo la msingi lilitakiwa shule hizo zingekuwa zaidi vyuo vya ufundi stadi, vyuo vya kilimo, vyuo vya wenye vipaji maalumu, vyuo vya uvuvi, vyuo vya ufugani, nk. Wahitimu wangekuwa na elimu ya kujiajiri, kubuni na kuendesha maisha yao. Lakini tatizo linalojitokeza wahitimu wa shule na vyuo vyetu ni kuchakaza kandambili kutembeza Resume maofisini wakati ardhi tupu imejaa ikiwasubiri ambayo ingewapa nafasi tele za kujiri na kuendesha maisha.​

Hakuna serikali duniani yenye uwezo wa kuwapa ajira vijana wote, kama kuna mwanasiasa anayewadangaya watu hivyo hivyo ni dondandugu katika jamii yetu. Kinachotakiwa kuwajengea vijana uwezo na nafsi ya kuendesha mamisha ndio elimu nzuri na tunapaswa kufanya hivyo. Mara kadhaa nimejaribu kuwapa vijana maoni namna ya kujiajiri lakini napata taabu sana kuuza sera hii, wanachodai muda wote ni mtaji.


Siri moja niianike wazi, matajiri wengi duniani wameanza na umaskini, wakajihinisha, kuweka kando starehe, na pengine wangine kutumia jembe la mkono hadi wamesimama. Sisi tunataka faida ya pao kwa papo wakati tumekaa kivulini, maisha bora hayaji hivyo.

Nilibahatika nchini Marekani kutembelea makumbusho ya hayati Thomas Edson mvumbuzi wa bulb za umeme tunazotumia siku hizi pale West Orange, karibu na Newark, Essex County, New Jersey. Kitanda chake alicholalia kingali pale makumbusho, alikuwa analala pale kwenye banda lake la majaribio, na gari lake lililotumia battery lingali pale pamoja na battery zake alilokuwa anafanya majaribio ya gari linalotumia umeme, bahati mbaya mauti ilimchukua kabla hajamalizia ndoto za uvumbuzi gari la umeme, ila bulb za umeme alifanikiwa. Mafanikio si kuanza na starehe, starehe huja baada ya mafanikio.

Ukweli elimu ya msingi ya kuwaandaa vijana kimaisha inakosekana. Vijana wanafikiria kazi za maofisini badala ya kufikira namna ya kujiajiri. Vijana hawaandaliwi kwa kujengewa elimu ya kujitegemea na ubunifu, bali huandaliwa mazingira ya kuajiriwa. Tanzania tuna bahati ardhi kila mtu ni huru kuitumia tofauti na mataifa ya magharibi ardhi ni ghali mno na mlalahoi hawezi kutia pua pale ila matajiri tu.Nchi yetu haijawa industrialized, tunatakiwa kujenga msingi wa kujiajiri

Kuna sababu nyingi ambazo zimefikisha matatizo haya ya elimu, na leo pengine tunachokiona ni matawi tu na kuacha mzizi, maana matatizo yametoka mbali na mengi yamesahaulika. Kuna kazi ya ziada kuifanya hadi elimu itengamae, na itatuchukua miaka kadhaa pengine hadi mwongo mzima kuimarisha elimu nchini.

Kazi bado na hakuna kukata tamaa, mabadiliko ni lazima la sivyo tutaendelea kulalamikia kitu wakati mamlaka ya kuleta mabadiliko nchini tunayo wananchi wapiga kura kuchagua viongozi wanaofaa kuondokana na mfumo wa kuachiana nafasi za uongozi kwa kutazamana usoni kwa kujali kutazama kwanza majina ya watu waliopo madarakani na nafasi nyingine serikalini ndipo mtu apewe nafasi. Nchi katu haitaendelea kwa mwendo huu.
 
Candid Scope and Zitto;
You have touched valid points. But I think that when it comes to education in rural areas, the country isn’t addressing the issue smartly. Take for example the current model. In this model, it’s believed that once you build a school, teachers will come and students will be taught accordingly. However, for some reasons this model hasn’t worked very well, and it’s time to tweak it.

One area that needs to be tweaked is the compensation of teachers. Currently, the levels of education and experience are the only variables that determine teachers’ salaries. I believe; however, this isn’t the case be the movement and migration of teachers follow economics patterns. In order to attract talented educators to work in remote and rural areas; other temporary and permanent compensation variables should be introduced as well. For example, a teacher who has decided to work in Kigoma should be paid twice as much as one who has decided to remain in DSM even though both have the same level of education and experience.

Furthermore, we need to recognize that the fundamentals of education for rural and urban students are the same. As such, shule za kata should serve the same purpose as other secondary schools. Yes there’s a room for ufundi stadi. However, we should be aware that ufundi stadi isn’t a substitute of decent secondary school education. We either empower our students with both types of education or we stick with secondary school education.

It’s clear that this year form four results aren’t impressive. However, this shouldn’t be a reason to retreat from the mission of providing secondary school education to our people, in particular those in rural areas. Students have failed because we didn’t invest well in education. For examples, we didn’t train good and enough teachers. We don’t offer attractive incentives and many more. So instead of changing the course, we should invest wisely.

We need to invest wisely because there are many subjects for secondary schools students which don’t need laboratories and other fancy teaching aid. Take for example, mathematics, Swahili, English, history, geography etc. To teach these subjects, you need teachers, pieces of chalk, blackboards, classrooms and students. These items are within our means and there’s no need to make excuses.

Even those subjects that require laboratories experiments can be taught theoretically. As a matter of fact, the environments which students live are living laboratories. We can teach our children using what available in their surroundings. For example, we can use our environments to teach chemistry, physics and biology.
 
Back
Top Bottom