Kwanini hakuna timu ya mpira K'njaro wala wachezaji wenye majina ya huko?

Makaura

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
892
Reaction score
295
Sijawahi kusikia timu wala mchezaji mwenye jina kama Mangi, Mbowe,Kweka, Mushi, Kileo,Ngowi, Kimambo wala Akyoo, labda Joseph Kaniki tu!
 
Joseph Kaniki ni Msambaa na sio mchaga. Na Akyoo ni ukoo Wa kabila la Meru na sio wachagga.
Yupo mchezaji wa Yanga ambaye ni goal keeper anaitwa Deo Mushi 'Dida'. Na pia Rais zamani Wa TFF Mr. Leodgar Tenga ni Mchagga.
Nadhani Wachaga wengi uenda wakawa ni si wapenzi wa Moira wa miguu kulinganisha na makabila mengine,na hata timu zinazotoka mkoa Wa Kilimanjaro nyingi zitakuwa na wachezaji ambao sio wazawa wa kule.
 
Sidhani kama Leodgar Tenga ni mchaga.
 
Sijawahi kusikia timu wala mchezaji mwenye jina kama Mangi, Mbowe,kweka, Mushi, Kileo,Ngowi, Kimambo wala Akyoo, labda Joseph Kaniki tu!
Deogratius Munishi a.k.a Dida goalkeeper wa timu yanga na tanzania one kwa sasa.....
 
wameru na wachagga hawana tofaut kivilee kimeru kinashabiana na machame wote ni sawa tu. Ni kama mndengereko mzaramo mndingo ama wamatumbi wote ni ki1 waswahili
 
Bar na maduka asimamie nani? acha wacheze wengine mangi bana.
 
Kweli umejib kama GT, hongera kwa majibu mazuri, na kwanini timu ya mpira haipo?
 
miss_changa tupo buyz na hela au mnataka tuchukue vyote
 
Last edited by a moderator:
Kuna kipindi cha nyuma kulikuwa na ushirika fc...kulikuwa na wachaga wengi kama kina john, kiango, etc

Pia pongezi kwa mohamed babu kipindi akiwa RC k'njaro alijitahidi kuinua soka na akafanikisha ujenzi wa uwanja wa George memorial moshi mjini ila ndo vile tena mafisadi wamegeuza uwanja wa mpira kuwa soko la mitumba!

Kuna timu zinawika kwa msimu kama ligi daraja la ii kama machava Fc, na sasa Panone Fc, tatizo vijana wengi wa moshi wanapenda ku invest kwenye high return na mpira haulipi kivile! Mtu unakuwa na biashara mpira unacheza for fun! Unateguka mguu mambo yako yanasimama!

Mpira utakapo kuwa kwenye level ya pro na ukalipa mbona kina mangi watajaa tu huko! Tatizo fedha hakuna huko

Sent from my WhiteBerry using JamiiForums
 
Kuna mido flani matata sana ipo Stand United "chama la wana" anaitwa Jacob Massawe.
 
Kuna mido flani matata sana ipo Stand United "chama la wana" anaitwa Jacob Massawe.
Kumbe kila Masawe inatoka Moshi eeeti!!!! basi kama ndivyo hivyo hata huku chama la Ndanda fc kuna masawe mwingine, but sijui kama huyu nae anatoka huko huko Uchagani...
 
hawa jamaa wengi wao ni wafanya biashara kwnye mikoa mingine, na wale waliobaki nyumbani huwa wana deal na upandaji wa mlima kilimanjaro huku waki make dolar so michezo kwa wao ni kama kupoteza muda wao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…