Kwanini hoteli kubwa zenye hadhi ya 5 stars huwa na bendera za mataifa mbalimbali kwa nje? Siri iko hapa!

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Najua nitakuwa sipo peke yangu, lakini mara nyingi huwa nikienda kwenye hizi hoteli kubwa the likes of Serena, Kilimanjaro Hyatt, huwa nakutana na bendera za nchi mbalimbali.

Zamani nilikuwa sijui maana ya bendera hizi na nilikuwa nadhani kwamba pengine bendera huwakilisha aina ya wageni ambao wako kwenye hoteli fulani.

Lakini ukweli ni kwamba hoteli nyingi husimamisha bendera kuonesha heshima kwa nchi nyingine na kuwafanya wageni wa nchi husika kujihisi wako nyumbani.

Ni jambo la kisaikolojia zaidi.

Imagine unapita katikati ya New York alafu unamuona mtu aliyevaa T shirt ya Taifa Stars anapigwa huku akiomba msaada kwa kiswahili.



It's more likely unaweza ukaenda kumsaidia kwa sababu umeona kwamba ana utanzania fulani na ni watu mliotoka eneo moja

It's the same way kwenye hoteli.

Bendera zinawekwa ili kujihisi na kukuvutia wewe uhisi uko nyumbani.



Kama kuna hoteli mbili zenye hadhi sawa, it's more likely utaenda kwenyee hoteli yenyr bendera ya nchi yako.

Nadhani kwa watu ambao wanasafiri sana watakuwa wameshanielewa!

Nawasilisha!
 
kuna bendera ya Tanzania, Afrika mashariki na Afrika picha ya juu nyingine ni Mataifa ambayo inaonyesha raia wake wengi hutembelea hoteli hiyo au hizo. Hii ndiyo maana halisi ya hoteli ya Kimataifa . Ukisikia five star hotel hata chakula kinachopatikana hapo utashangaa maana kuna vyakula vingine vilivyopo huko nchi za wenzetu vinapatikana pia.
 
Mbona huku Zanzibar Hotel ya nyota 5 aina bendera ya Tanzania
 

Attachments

  • IMG_20241102_134425_953.jpg
    1.3 MB · Views: 12
  • IMG_20241102_134421_826.jpg
    1.7 MB · Views: 11
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…