Kwanini kama Taifa Corona ni tishio kubwa?

Kwanini kama Taifa Corona ni tishio kubwa?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Maadui wakubwa wa taifa hili wamekuwa siku zote ni ujinga, maradhi na umasikini.

Miaka 60 ya uhuru leo tungali humo humo.

Hali halisi tishio jipya la corona

Leo hii pamoja na tahadhari zote za wataalamu wabobezi, ujinga ungali umetughubika vilivyo.

Kwa maana halisi, ujinga ni kudhani wajua kumbe hujui, ni kutokuelewa, au kutokufahamu. Ujinga si tusi. Elimu huondoa ujinga.

Tulipo leo bado tuna wanaodhani wataalamu ndiyo wajinga na kuwa eti kutokea vijiweni wao ndiyo werevu. Hiyo ni shughuli pevu.

Leo hii tunakabiliwa na gonjwa la hatari zaidi linaloua ghafla ghafla, ndani ya mengine mengi ambayo nayo bado ni kizungumkuti.

Umasikini wetu nao uko pale pale. Zaidi sana hata wabunge wetu nao ndiyo wanazidi kulia njaa. Huku mitaani na vijijini kutakuwa je?

Tunaponea wapi kama taifa bila ya kuwa na mkakati sahihi kutokea juu?

Hii bila ya suluhu kutokea kwake Mama Samia, zikiwamo busara zake, tusipoangalia tutaangamia wengi.
 
Tunajivunia hao maadui zetu wa asili, Mungu alituasa tuwapende adui zetu…. hivyo tuishi nao tu kiroho safi.[emoji276]
 
Tunajivunia hao maadui zetu wa asili, Mungu alituasa tuwapende adui zetu…. hivyo tuishi nao tu kiroho safi.[emoji276]

Mkuu nimekuelewa sana. Kwa hakika haiwezi kuwa tofauti. No wonder tumerithi mengi ya maana sana tokea awamu ya tano:


Hasa hasa tokea kwa engine zilizokuwa zikipeleka agenda za awamu ile mbere!
 
Maadui wakubwa wa taifa hili wamekuwa siku zote ni ujinga, maradhi na umasikini.

Miaka 60 ya uhuru leo tungali humo humo.


Leo hii pamoja na tahadhari zote za wataalamu wabobezi, ujinga ungali umetughubika vilivyo.

Kwa maana halisi, ujinga ni kudhani wajua kumbe hujui, ni kutokuelewa, au kutokufahamu. Ujinga si tusi. Elimu huondoa ujinga.

Tulipo leo bado tuna wanaodhani wataalamu ndiyo wajinga na kuwa eti kutokea vijiweni wao ndiyo werevu. Hiyo ni shughuli pevu.

Leo hii tunakabiliwa na gonjwa la hatari zaidi linaloua ghafla ghafla, ndani ya mengine mengi ambayo nayo bado ni kizungumkuti.

Umasikini wetu nao uko pale pale. Zaidi sana hata wabunge wetu nao ndiyo wanazidi kulia njaa. Huku mitaani na vijijini kutakuwa je?

Tunaponea wapi kama taifa bila ya kuwa na mkakati sahihi kutokea juu?

Hii bila ya suluhu kutokea kwake Mama Samia, zikiwamo busara zake, tusipoangalia tutaangamia wengi.
Unalalamika nini? Je unaumwa corona? Au unataka tu ushabiki wa vitu ambavyo waliovifanya havijawaokoa na corona? Ulikuwa wapi wakati watanzania wanapigana vita na corona? Inaelekea hukushiriki vita hii na ndio maana hata ushindi ulipopatikana hukuwa na habari! Nikukumbushe: Corona ilipoingia nchini mwetu Rais wetu wa wakati huo aliitisha maombi ya kitaifa kwa kufunga kwa muda wa siku tatu.? Wote walioshiriki kikamilifu wanajua kinachoendelea na kinachotafutwa sasa!! Mungu alijibu maombi yetu na shule na vyuo vikafunguliwa. Rais wetu wa awamu ya tano akaitisha tena maombi ya shukrani kwa Mungu kwa siku tatu tukiwa tumefunga!! Shule na vyuo hazikufungwa na hazitakuja kufungwa tena!! Watu wasiomjua Mungu walitubeza sana watanzania! Lakini watu hao hawana ubavu wa kubeza matokeo na hali ya Tanzania kuhusu corona wakijilinganisha na nchi zao!! Hatuhitaji takwimu kulijua hilo maana athari ya corona inaonekàna kweupe kwenyè jamiii!! Linalodaiwa ni wimbi la tatu linaitamani sana Tanzania lakini tumezungushiwa wigo na Mungu na corona haina ubavu wa kutugusa!! Ila yule anayeishabikia na kuamini kuwa ipo, atakuwa anaikaribisha nyumbani mwake na haitamwacha salama!
 
Maadui wakubwa wa taifa hili wamekuwa siku zote ni ujinga, maradhi na umasikini.

Miaka 60 ya uhuru leo tungali humo humo.


Leo hii pamoja na tahadhari zote za wataalamu wabobezi, ujinga ungali umetughubika vilivyo.

Kwa maana halisi, ujinga ni kudhani wajua kumbe hujui, ni kutokuelewa, au kutokufahamu. Ujinga si tusi. Elimu huondoa ujinga.

Tulipo leo bado tuna wanaodhani wataalamu ndiyo wajinga na kuwa eti kutokea vijiweni wao ndiyo werevu. Hiyo ni shughuli pevu.

Leo hii tunakabiliwa na gonjwa la hatari zaidi linaloua ghafla ghafla, ndani ya mengine mengi ambayo nayo bado ni kizungumkuti.

Umasikini wetu nao uko pale pale. Zaidi sana hata wabunge wetu nao ndiyo wanazidi kulia njaa. Huku mitaani na vijijini kutakuwa je?

Tunaponea wapi kama taifa bila ya kuwa na mkakati sahihi kutokea juu?

Hii bila ya suluhu kutokea kwake Mama Samia, zikiwamo busara zake, tusipoangalia tutaangamia wengi.
Upuuzi....
 
Upuuzi....

Ninakazia:

IMG_20210624_132438_541.jpg
 
Unalalamika nini? Je unaumwa corona? Au unataka tu ushabiki wa vitu ambavyo waliovifanya havijawaokoa na corona? Ulikuwa wapi wakati watanzania wanapigana vita na corona? Inaelekea hukushiriki vita hii na ndio maana hata ushindi ulipopatikana hukuwa na habari! Nikukumbushe: Corona ilipoingia nchini mwetu Rais wetu wa wakati huo aliitisha maombi ya kitaifa kwa kufunga kwa muda wa siku tatu.? Wote walioshiriki kikamilifu wanajua kinachoendelea na kinachotafutwa sasa!! Mungu alijibu maombi yetu na shule na vyuo vikafunguliwa. Rais wetu wa awamu ya tano akaitisha tena maombi ya shukrani kwa Mungu kwa siku tatu tukiwa tumefunga!! Shule na vyuo hazikufungwa na hazitakuja kufungwa tena!! Watu wasiomjua Mungu walitubeza sana watanzania! Lakini watu hao hawana ubavu wa kubeza matokeo na hali ya Tanzania kuhusu corona wakijilinganisha na nchi zao!! Hatuhitaji takwimu kulijua hilo maana athari ya corona inaonekàna kweupe kwenyè jamiii!! Linalodaiwa ni wimbi la tatu linaitamani sana Tanzania lakini tumezungushiwa wigo na Mungu na corona haina ubavu wa kutugusa!! Ila yule anayeishabikia na kuamini kuwa ipo, atakuwa anaikaribisha nyumbani mwake na haitamwacha salama!

Wapi umeona malalamiko? Kabila gani wewe ambako huko kiswahili bado ki hivyo?

Unafahamu kuwa huu ugonjwa unakwenda kama mawimbi? Unafahamu nini maana ya wimbi #1, #2, na sasa hivi tunatahadharishwa wimbi #3?

Hii nchi iliokoka lini kufungamanishwa na maombi za maombi? Hao maaskofu wafufua wafu waliopotelea wapi wakati muda wao wa kuhitajika kweli kweli ulipowadia?

Acheni kulitaja jina la bwana bure kwa maslahi yenu uchwara kama inavyoandikwa kwenye misahafu.

Nisiache kukazia:

IMG_20210624_132438_541.jpg


kwani bila hivyo nitakuwa sijakutendea haki.
 
Pole pole tunaendelea kusogea:


IMG_20210625_121904_739.jpg


Barakoa si hiari tena.
 
Back
Top Bottom