Uchaguzi 2020 Kwanini kampeni za mwaka huu zimepooza sana?

Hamna kampeni, kuna watu wanazunguka zunguka kupigana vijembe na kusifia vyama.

Wanainchi hawana mzuka tena na shughuli za kisiasa...... Wamewaacha wafanye wanachotaka....
 
Hiyo point namba saba umenikumbusha kuna mtu namdai....
 
Mkuu hii reply yako umenifanya nikupuuzie Sana, Yaani haiendani na Uzi hata kidogo. Punguza ushabiki. Lissu Kaingiaje hapo!?
Kaingia kwasababu ni mmoja wa wagombea. Hujaelewa.mada inauliza nn?
 
NEK ifumuliwe.Imekuwa ya Ovyo sana
 
mkuu uko sawa ila niseme tu chama dola hasa viongozi wa juu wameisha ona aina ya mchezo ulivyo mgum , japo twaongea kujifuraisha hum tu thats hata hii engua inawafeva kidogo but niseme tu ccm pamoja na viti ambavyo tiyari wanavyo vikiongezeka zaidi katika uchaguzi havitazidi 25 nakwambia , msicheze na uchaguzi mkuu , mfano jiulize kama chama dola kinafikili uchaguzi huu ni mwepesi why wanatumia gharama kubwa , kwa macho ya rohoni huu ni uchaguzi mgum kuwahi tokea tz na hivihivi kimasiara uanweza shangaa chadema inaondoka na taulo ya mtu , msemo wa gwajima
 
 
CCM wameharibu nchi sana tumekuwa kama Sudan ya Kusini.
 
Profesa Magufuli anafanya yale yote watz mnayoyataka.


Lisu oyeeeeeeeeee
 
Toka kuzinduliwa kwa kampeni yaan sehemu nyingi za dar Utadhani Hakuna uchaguzi mwaka huu... Story za simba na yanga ndio zimetapaa... SIJASIKIA POPOTE WATU WAKIJADILI CCM AU CHADEMA ETC..

Watu wamekata tamaaa mkuu
 
"dalili zote zinaonyesha Wananchi hawana hamu na kampeni".

Kwa maoni yangu nadhani si kwamba watu hawana hamu na kampeni, bali inawezekana ni kwa sababu 2.
(1) Kutokana na awamu hii ilivyokuwa watu wamesha kata tamaa na ccm, pengine wanaona hata wakifuatilia kampeni za ccm hakuna jipya kuhusu maisha yao, hasa kwa namna ccm inavyo lazimisha ushindi. Wanajua nini kitaendelea ccm itakapo jiweka madarakani baada ya uchafuzi.
(2) Kutokana na awamu hii ilivyokua pengine watu bado wana hofu na maisha yao kuhudhuria mikutano ya upande wa upinzani. Kwa sababu wanajua kwa upande huo polisi hawakawii kukinukisha.

Kwa kuwa kampeni ndio zimeanza, pengine wengi bado hawajaamini kwamba ni kweli imeruhusiwa kukusanyika ama ni mtego ili watu tuumizane? Si unajua tena kila mtu ana uelewa wake.

"ufunguzi wa kampeni za CCM, wao walinufaika zaidi na wanachama wao hai".

Ukiondoa walio na vyeo ndani ya chama/serikalini walio baki wote walishavunjwa viuno sio hai tena. Kwa mfano idadi ya walio jitokeza kuomba uteuzi kwenye nafasi za ubunge haija wahi kutokea katika historia ya nchi hii. Kipropaganda wanakwambia ni kwa sababu ya utendaji kazi wa awamu ya 5. Lakini ukweli ulio jificha ni kwamba watu wamejifunza katika muhula wa kwanza wa JPM. Na kama akiingia muhula wa pili basi hali inaweza kuwa mbaya zaidi kwa sababu anamaliza muda wake na hana cha kupoteza. Kazi ambayo haina longolongo na ni ya uhakika nikuingia mjengoni. Ukiondoa mshahara, posho ya kila kikao bora tu uwe umesaini kwamba upo bila kujali kwamba utachangia, utashangiria ama utalala tu kwenye kiti chako lakini lazima 340,000 itakuhusu. Bado kuna kiinua mgongo cha zaidi ya milioni 200 kina kusubiri ndani ya miaka mitano. Kwa nini watu wasijitokeze kwa wingi. Na pia uhai wa ccm unao onekana sio uhalisia. Kuna makundi mawili, kundi la masikini ambao kwa sasa tunaitwa wanyonge, kundi hili inapofika wakati wa kampeni kwao inakuwa ni kama sikukuu wanapata shati, flana, magauni, madera, kanga na vitenge vipya kwa sare ya chama na wanakuwa wamepata mahali pa kwenda ili siku iishe kwa shangwe. Na kundi jingine ni la wapenzi/mashabiki wa wasanii, hawa nao wanafuata shangwe na ndio hapo watu tunapo dhani kuwa ccm inajaza watu kwa maana yakupendwa/kukubalika.

"CCM ndo usiseme, wako slow kweli kweli au kwakuwa wana akiba kibindoni?"

Hawana akiba yoyote kiongozi,miaka zaidi ya 50 madarakani na hasa yaliyo fanywa na awamu hii kama yatawekwa kinamna ya hoja ili yajadiliwe basi itakuwa ngumu kwa ccm kuyatetea kwa hoja.

"WATU WENGI WANASUBIRI UTOKEE MUUJIZA LISsU ASHINDE".

Lissu kushinda sio muujiza na hata ccm wenyewe wanajua hilo, ndio maana unaona kuna sarakasi nyingi. Ki ukweli JPM hayuko vizuri katika ujengaji hoja ukimpambanisha na Lissu.
Na suala la Lissu kushinda ama kushindwa rudia kutafakari kauli za aina tatu na uangalie mambo yanavyo kwenda halafu utajua muujiza utakuwa upi? Tafakari kauli hizi:

"Nikuteue mimi, nikupe gari na mshahara nikulipe mimi halafu umtangaze mpinzani?"-JPM
"Chama kilichopo madarakani ndio kinacho nufaika na dola kubaki madarakani, kanu iliondoka madarakani kwa sababu ilishindwa kuitumia dola kubaki madarakani". - Dr Bashiru
"Uchaguzi ukiwa huru na wa haki, ccm ijiandae kukabidhi ikulu". - Polepole

Kutokana na kauli hizo ambazo hata mimi ambae si msomi lakini nimezielewa. Muujiza hapa sio Lissu kushinda, bali muujiza ni tume ya uchaguzi (tawi la ccm) kumtangaza Lissu kwamba ameshinda.
 
Kumpambanisha JPM na maguni ya viazi ndio majibu yake haya.
JPM is not a man in a campaign, IS THE ONE WITH A CAMPAIGN.




MAGUFULI4LIFE.
 
Magufuli ameharibu siasa za Tanzania yaani watu wamechoka siasa
Ile kuwalazinisha watu kujiunga nae jamaa kaharibu siasa.
Maana ile kununua wapinzani ndio maana raia wengi wanaona ni ujinga tu kupambana wanapita ila kesho wananunuliw!
 
Hawatupi wananchi hela, watoe hela tuingie front kuwafanyia kampeni, wanahubiri uzalendo, uzalendo bongoooo.
 
Ukweli utatuweka huru, uchaguzi huu umeharibiwa na gia ya angani 2015 wapinzani hawaaminiki tena. Hata hizi kelele unazosikia mitandaoni ni vijana ambao hawakupiga kura 2015 sababu ya umri.

Kingine wapinzani hawapo serious Sana kupambana na CCM huwezi kuishinda CCM bila wao kuungana km ilivyokuwa 2015. Hawana malengo, wamejaa viburi na ubinafsi.

CCM sio ile ya 2015 iliyoingia kwenye uchaguzi ikiwa ndembendembe kwa kashfa za rushwa na kutowajibika ipasavyo. Hii ya 2020 inamtaji mkubwa wa wananchi wanaoiunga mkono hasa watu wa hali ya chini. Ikumbukwe ndipo wapigakura wengi walipo.

Lissu na Membe hawana ushawishi wala mvuto kwa wananchi. Inaonekana 'bora zimwi likujualo... Aina za kampeni hasa Lissu inaonekana hakujiandaa kilicho mleta ni hasira za risasi 16. Kauli zake nyingi ni utegemezi kwa mataifa ya nje. Hii imempotezea sana hata ile imani ndogo wananchi walokuwa nayo juu yake.
 
Huku kwenye ngazi za Kata ni aibu. Hakuna mgombea awe wa CCM,CHADEMA ama ACT aliyezindua kampeni na tatizo kubwa hawana bajeti ya kukodi hata baiskeli zote pesa zote zimeshamezwa na wakubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…