Uchaguzi 2020 Kwanini kampeni za mwaka huu zimepooza sana?

Magu alifungia siasa kwa miaka mitano, akawasomesha namba wananchi.

Akafungia bunge, wananchi wakanyimwa ushiriki wao kwa shughuli za serikali.

Wakazuia taasisi za kiraia ambazo hutoa elimu ya uraia na ushiriki wa wananchi kwenye shughuli za umma.

Akaziminya halmashauri zote zikamtegemea yeye kaamkaje hivyo wananchi wakawa hawana sauti tena hata huko serikali za mitaa.

Serikali yake ikafumbia macho utekaji, watu kupigwa risasi, vijana waliokuwa wakishiriki siasa wakatekwa, wakafunguliwa makesi.

Wanasiasa wakafunguliwa makesi, wakapigwa na mapolisi, wakafungwa na wakafilisiwa.

Vyombo vya habari vikazuiwa kutangaza habari za siasa tena wala masuala ya kijamii radio zikaamua kupiga bongo flava na singeli kwa miaka mitano wananchi wakaamua kuunga mkono bongo flava.

Tume ya uchaguzi kufanya uhuni kuchezea Sanduku la kura na uchaguzi wa serikali za mitaa.

Vyombo vya habari haturuhusiwi tena kutangaza mikutano ya vyama vingine isipokuwa ccm tu wakati haina mvuto tena kwa wananchi.

Akajitia mjuaji akaanza kununua wapinzani uchwara ambao wananchi walipoteza damu zao kuwapigania.

Wananchi wakatishwa kwa matukio ya utekaji na maiti kuokotwa kwenye viroba, na waliopigwa risasi hadharani bila hata aibu.


Nani atakuwa na hamu na uchaguzi tena ??
Magufuli katuharibia nchi sana.
 
Wengi hawataenda kwenye kampeni ila kwenye kupiga kura wataenda na wanamjua mgombea watakaempa ambaye alichokifanya kinaonekana lakini wapo wapinzani watakaobadilika siku ya kupiga kura akiingia tu kwenye chumba anawaza maendeleo hapo moja kwa moja inamjia sura ya magu.
 
Uhuru wa kujieleza na Ni haki yako kusikilizwa.
 
Huu ni ukweli au hisia tu ?
 
Inasikitisha. Vyombo vya habari vimechukua nafasi kubwa ya kugeuza kampeni na Uchaguzi kuwa na muelekeo wanaotaka. Si wananchi tumekosa picha kamili ya nini kinaendelea!
 
Kiufupi nchi hii tasnia ya habari imeingiwa na matapeli na washamba wa kisiasa
 
Mnapowashangaa waandishi wa habari na vyombo vya habari, shangaeeni na TCRA ambao kila siku wanatunga kanuni ili CHADEMA na upinzani wasisikike. Kwani ni nani anataka kufungiwa bwana?
 
Ukiona mgombea wako au chama chako hakiripotiwi sana na vyombo vya habari fahamu kuwa wanafanya kampeni zilizo kinyume na maadili ya uchaguzi. Matusi, uchochezi, vitisho, uchonganishi ndio vinatawala. Sasa vyombo vya habari haviwezi kuripoti vitu kama hivyo.
 
Mnapowashangaa waandishi wa habari na vyombo vya habari, shangaeeni na TCRA ambao kila siku wanatunga kanuni ili CHADEMA na upinzani wasisikike. Kwani ni nani anataka kufungiwa bwana?
Kwani CHADEMA wanashindwa nini kutimiza masharti ya hizo kanuni? Nini kinawazuia kucomply na hizo kanuni?
 
Ndivyo wanavyotaka.. awamu hii ilianza kutunisha mbawa zake toka bungeni hawakutaka liwe live ili wananchi wasione wawakirishi wao!..

Vyombo vya habari ilitakiwa iwe ni chemchem ya kujibu maswali kwa kuwahoji wahusika juu ya maswala mbalimbali mfano.. kukosekana kwa mikopo vyuoni,maswala ya ajira,kunatakiwa kuwe kuna mjadala juu ya elimu yetu je,inakidhi vipi ktk kutatua uhaba wa ajira..? Hayo ni baadhi ya hoja na maswali yaliyopaswa yajibiwe.. tupo tu tunasikilizishwa watu walewale wanaolalamika nchi ikinyonywa wakati huyohuyo nae amekuwepo serikallini kwa miaka 20! Tena anarudi na kuuhadaa uma!..

Vyombo vya habari vingi vinaonyesha yaliyofanywa tu hata hawaonyeshi ambayo hayajafanywa.. inatakiwa wawe chachu pia ya kuionyesha serikali matatizo,inatakiwa pia iwahoji watu ili serikali ijue watu wake wanataka Nini.. tumechoka kila siku kusema hoyeeeee..
 
Kwani Chadema wanashindwa nini kutimiza masharti ya hizo kanuni? Nini kinawazuia kucomply na hizo kanuni?
Kwendra huko. Hata huelewe unachoandika hapa. Nitapoteza muda kubishana na wewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…