Kwanini kujiua ni kosa kisheria?

Kwanini kujiua ni kosa kisheria?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Leo tarehe 10/10 ni siku ya Afya ya akili duniani. Moja ya sababu kubwa ya watu kujiua ni matatizo ya Afya ya akili. Na mgonjwa wa akili hatendi kosa zaidi ni anahitaji msaada wa matibabu.

Sasa nini kilipelekea Tanzania kuunda sheria kuwa kujiua(Kujaribu kujiua) ni kosa kisheria?

Hii sheria ina shida mbili.
Kwanza inamfanya anayejiua ahakikishe anakufa kabisa. Maana akipona atashtakiwa.

Pili inamfanya anayesakamwa na mawazo ya kujiua ashindwe kuomba msaada. Maana tayari anachowaza kimeshanyanyapaliwa kuwa ni kosa kisheria.

Nafikiri kuna haja ya kubadili hiyo sheria na pia kuna haja ya mamlaka husika kutoa msaada kwa wenye mawazo ya kujiua, kama kuanzisha namba ya msaada.
 
Kuniua haiwezi kuwa kosa,kwani maiti inasjitakiwa?
Labda ukikaribu kuniua na ikashindikana ndiyo kosa,maana utashitakiwa.
 
Here is the matter of Jurisprudence, Kuna theory nyingi Sana zinazoelezea hili suala..... Leo hii ukiondoa hii sheria wapo watakao uawa kwenye ndoa au familia na kutengenezwa kuwa kajiua then nothing will be investigated, maana tunapeleleza palipo na kosa na si vinginevyo.
 
Back
Top Bottom