Juzi kupitia taarifa ya habari ya usiku Meneja wa TARURA Wilaya ya Urambo alipoulizwa na Baraza la Madiwani kuhusu hali mbaya ya barabara katika Wilaya hiyo bila kuogopa alitamka wazi kuwa ni muda mrefu umepita Wilaya yake haijapokea fedha toka Serikalini.
Siyo tu kwa wilaya ya Urambo bali karibu nchi nzima wanapitia tatizo hili. Juzi kwenye kikao cha Bunge la Jamhuri kule Dodoma, Mbunge wa Singida Mashariki wakati akichangia kwenye mjadala alisema kuwa Wakandarasi wengi hawajalipwa madai yao licha ya kuwasilisha certificate kwa mamlaka husika kwa ajili ya malipo.
Tunajiuliza kunanini na kwanini wakandarasi hawalipwi madai yao ili waendelee na kazi?. Hii ni tofauti kabisa na awamu ya tano pale mkandarasi alipomaliza kazi yake na kuwasilisha cerificate na kukaguliwa alikuwa analipwa mara moja.
Siyo tu kwa wilaya ya Urambo bali karibu nchi nzima wanapitia tatizo hili. Juzi kwenye kikao cha Bunge la Jamhuri kule Dodoma, Mbunge wa Singida Mashariki wakati akichangia kwenye mjadala alisema kuwa Wakandarasi wengi hawajalipwa madai yao licha ya kuwasilisha certificate kwa mamlaka husika kwa ajili ya malipo.
Tunajiuliza kunanini na kwanini wakandarasi hawalipwi madai yao ili waendelee na kazi?. Hii ni tofauti kabisa na awamu ya tano pale mkandarasi alipomaliza kazi yake na kuwasilisha cerificate na kukaguliwa alikuwa analipwa mara moja.