Kwanini Mabenki bado yanakata Tozo za Miamala zilizofutwa na Serikali?

Kwanini Mabenki bado yanakata Tozo za Miamala zilizofutwa na Serikali?

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Hivi wakuu mmegundua wizi unaofanywa na Mabenki kwenye makato ya miamala? Licha ya Serikali kufuta Tozo za Miamala ya uhamishaji fedha ndani ya Benki, kwenda kwenye Simu pande zote, kutoka Benki moja kwenda nyingine tangu Okt. 1, 2022 lakini bado kuna Benki zimeendelea kukata tozo hizo bila maelezo yoyote.

Suala lingine ni kimya wa Serikali unanitia mashaka kwenye hili jambo kwamba je haitambui au inashiriki kwenye huu wizi wazi wazi? Na kama Benki zimeongeza gharama mbona hazijatoa taarifa kwa mteja kuhusu mabadiliko hayo?.

Serikali ichukue hatua za haraka kudhibiti wizi wa wazi unaofanywa na Mabenki katika suala la Tozo za Miamala pia Benki zitoe taarifa fedha zinazokatwa nani anafaidika nazo. Vinginevyo tutaamini kuwa ilituhadaa kuwa imefuta lakini hakuna kilichofanyika.
1669007487259.png
 
Hivi wakuu mmegundua wizi unaofanywa na Mabenki kwenye makato ya miamala? Licha ya Serikali kufuta Tozo za Miamala ya uhamishaji fedha ndani ya Benki, kwenda kwenye Simu pande zote, kutoka Benki moja kwenda nyingine tangu Okt. 1, 2022 lakini bado kuna Benki zimeendelea kukata tozo hizo bila maelezo yoyote.

Suala lingine ni kimya wa Serikali unanitia mashaka kwenye hili jambo kwamba je haitambui au inashiriki kwenye huu wizi wazi wazi? Na kama Benki zimeongeza gharama mbona hazijatoa taarifa kwa mteja kuhusu mabadiliko hayo?.

Serikali ichukue hatua za haraka kudhibiti wizi wa wazi unaofanywa na Mabenki katika suala la Tozo za Miamala pia Benki zitoe taarifa fedha zinazokatwa nani anafaidika nazo. Vinginevyo tutaamini kuwa ilituhadaa kuwa imefuta lakini hakuna kilichofanyika.
Njoo na ushahidi hata kapicha
 
Taasisi huwa zinafanya kazi kwa nyaraka rasmi, kama tamko lilitolewa kwenye majukwaa ya kisiasa bila walengwa kupelekewa waraka wa serikali HAWALITAMBUI
 
Back
Top Bottom