Kwanini Mabenki hayarudishi pesa wanazokata kama " Bima ya mkopo pindi deni la mhusika linapoisha

Ungeweka hati za nyumba labda ungeipata, maana ya bima unatoa sehemeu ndogo ya thamani harisi ya kitu, ili itakapo tokea janga wao bima wachange na za wengine kufidia hasara, kwa kifupi kama hakuna dharura hiyo pesa inakuwa imeliwa au imetumika kufidia wengine.
 
Sikilizeni watanzania,

Bima ya mkopo ni sheria ya Bank kuu kwa taasisi za kifedha zote zilizochini yake.

Bima ya mkopo uliyokatwa wakati wa mkopo inapelekwa kwenye shirika la Bima ,

Bima ya mkopo ina cover, Kifo na ulemavu wa kudumu

Endapo Mnufaika wa mkopo atapokufa au kupata ulemavu wa kudumu basi,shirika la bima litalipa deni la benki lote,ndugu wala mali zake marehemu hazitaguswa

Bima yoyote huwa hairudishwi(fatilia vizuri huko kenya pengine ulirudishiwa makato ya ziada uliyokatwa kimakosa) bima sio Bondi..

Sheria inataka kila mkopo ulipiwe bima sababu ya kiuchumi, akifa mdaiwa mmoja basi wale wengine pesa zao zitalipa deni lake.

Shirika la bima halipati hasara kulipa sababu ni michango ya watu wengine.

Unapo saini fomu ya mkopo unakuwa umekubali hayo yote..na kama ukikataa kusaini hutapata mkopo.

Kama unamalalamiko ni vizuri ukaenda shirika la Bima la taifa.

Akifa mfaidika,basi ni kupeleka cheti cha kifo tu au hati ya mazishi na deni litalipwa(kwa michango ya wengine). Nyumba ya marehemu itapona kwaajilibya familia yake.

""Bima ni kama kamariii...Ufe ilibuifaidi maana yake imekuraaa au usife ili uliweee maana yake umeliwaaa""

Case closed mkuu,i hope umenielewa.
 
Ngoja na mimi nijaribu kuchangia;

Jambo la kwanza; bima yoyote inakatwa kwa ajili ya event. Na kwa ajili ya bima tunalipa insurance premium ambayo ndiyo uliyokatwa. Hii premium inatengeneza sum insured ambayo ndo ule mkopo uliochukua.
Kwenye hii arrangement ya mtoa mada kama nimeelewa vizuri, alikata bima ya maisha na ulemavu wa kudumu (credit life).
Ni kweli hii italipa deni lako litakalokuwa limebaki kama utafariki au kupata ulemavu wa kudumu wakati mkopo haujamalizika.

Lakini ikitokea ukacancel mkopo wako kabla ya muda basi utapaswa kurudishiwa sehemu ya premium ambayo haija-expire bado.
Lakini deni linapoisha kulingana na muda mliokubaliana basi na bima inaisha. Yaani lapse of time or marurity of the subject. Premium haiwezi kurudishwa kama muda umepita.
Ni hayo tu kwa sasa
 
Hahaha hawa jamaa watakuwa wanapiga pesa sana kwa kutumia.
Bado wana kitu kinaitwa processing fee aisee
 
Nimekuelewa japo naona kama janja janja tu za kupiga pesa.
Hii processing fee ina haja gani kuwepo nayo wakati mimi ni mteja?
 
Benki pekee inayorudisha bima wakati ukimaliza mkopo ni Standard charterd.
Wiki iliyopita nilitoa maoni yangu kwa bank nyingine kwamba walifikirie jambo hilo.
 
Processing fee kwa upande mwingine ni gharama inayolipwa na mkopaji kwa ajili ya shughuli mbalimbali zinazohitajika kukamilisha mkopo
Kwa haraka haraka nafikiri gharama zake ni kama vile stationeries, travel here and there, kuja kufanya uhakiki ( kwa baadhi ya aina ya mikopo), na vinginevyo
 
Bima hawahesabu hasara kwao kila siku ni faida tupu, ndiyo maana hawarudishi chochote...



Cc: mahondaw
 
Benki pekee inayorudisha bima wakati ukimaliza mkopo ni Standard charterd.
Wiki iliyopita nilitoa maoni yangu kwa bank nyingine kwamba walifikirie jambo hilo.
Mkuu hata mimi stanbic bank Kenya walinirudishia japo hapa wadau wanakataa kwamba hairudishwi
 
Hivi unajua maana ya BIMA???


Bima amana inayowekwa ili yanapotokea matukio fulani ya kuleta hasara kwa kwa mlipaji basi aweze kufidiwa, ikizingatiwa kwamba matukio hayo yasipotokea, basi mlipaji hatarudishiwa pesa yake hiyo..
 
Gharama za processing fee ni wizi wa waziwazi
 
Hivi unajua maana ya BIMA???


Bima amana inayowekwa ili yanapotokea matukio fulani ya kuleta hasara kwa kwa mlipaji basi aweze kufidiwa, ikizingatiwa kwamba matukio hayo yasipotokea, basi mlipaji hatarudishiwa pesa yake hiyo..
Huu nao ni wizi hayajatokea, why nisirudishiwe?
 
Bado nataka kuamini kwamba either umelipa mkopo kabla ya muda kwa hiyo ukarudishiwa unexpired premium ama uliweka deposit ukaiita gharama ya bima.

Kumbukeni tunacholipia ni cost of insurance which is premium, to have that cover in place.

Why should we be refunded the cost while we enjoyed the benefit?
 
Mh kwani hiyo bima ni dhamana?..na je dhamana unatoa wewe mkopaji au benki?..kama unatoa wewe mbona bima imejumlishwa kwenye mkopo means hutoi wewe direct mfukoni mwako kama ilivyo hati ya nyumba....so kiutaratibu hairudishwi ila iliwekwa kumlinda mkopaji incase umetangulia mbele ya haki au umeachishwa kazi kwa sababu ambazo hukusababisha wewe basi mali yako isichukuliwe..hivyo tu...watakuja wenyewe na majibu
 
Sasa ndo sijafukuzwa na wala sijafa wanirudishie, hizi taasisi kuna sehemu hawatoi elimu vizuri ili wapate mwanya wa kutupiga
 
Dr Kimei hawezi kukuelewa una hoja dhaifu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…