Kwanini Mabenki hayarudishi pesa wanazokata kama " Bima ya mkopo pindi deni la mhusika linapoisha

Kwanini Mabenki hayarudishi pesa wanazokata kama " Bima ya mkopo pindi deni la mhusika linapoisha

Ninachofahamu mimi ni kuwa dhamana haitachukuliwa endapo mkopaji kashindwa kurejesha mkopo kutokana na sababu zilizoainishwa labda kifo, ulemavu wa kudumu nk. Hapo ndo bima inachukua nafasi ya kulipia deni. Yaani mfano mtu kafariki, kaweka nyumba kama dhamana, hiyo nyumba haitachukuliwa na kuuzwa na taasisi ya fedha kisa marehemu hakumaliza kulipa mkopo wake.
Mkuu Kuna nyumba imetangazwa karibu mara ya sita sasa na mkopaji no marehemu imekaaje hii. Jamaa ni mtoto kwenye hiyo familia wazazi wake wamefariki wote, ndugu zake kaka na dada wamefariki kabaki yeye na wajukuu wa hiyo familia. Yeye ndio mtoto pekee wa marehemu akaenda kukopa 70M . Baada ya Kama mwaka amefariki mbona nyumba inapigwa mnada Kama marehemu hadaiwi.
 
Sikilizeni watanzania,

Bima ya mkopo ni sheria ya Bank kuu kwa taasisi za kifedha zote zilizochini yake.

Bima ya mkopo uliyokatwa wakati wa mkopo inapelekwa kwenye shirika la Bima ,

Bima ya mkopo ina cover, Kifo na ulemavu wa kudumu

Endapo Mnufaika wa mkopo atapokufa au kupata ulemavu wa kudumu basi,shirika la bima litalipa deni la benki lote,ndugu wala mali zake marehemu hazitaguswa

Bima yoyote huwa hairudishwi(fatilia vizuri huko kenya pengine ulirudishiwa makato ya ziada uliyokatwa kimakosa) bima sio Bondi..

Sheria inataka kila mkopo ulipiwe bima sababu ya kiuchumi, akifa mdaiwa mmoja basi wale wengine pesa zao zitalipa deni lake.

Shirika la bima halipati hasara kulipa sababu ni michango ya watu wengine.

Unapo saini fomu ya mkopo unakuwa umekubali hayo yote..na kama ukikataa kusaini hutapata mkopo.

Kama unamalalamiko ni vizuri ukaenda shirika la Bima la taifa.

Akifa mfaidika,basi ni kupeleka cheti cha kifo tu au hati ya mazishi na deni litalipwa(kwa michango ya wengine). Nyumba ya marehemu itapona kwaajilibya familia yake.

""Bima ni kama kamariii...Ufe ilibuifaidi maana yake imekuraaa au usife ili uliweee maana yake umeliwaaa""

Case closed mkuu,i hope umenielewa.
Well said. Umemaliza mkuu
CASE CLOSED kama kuna mbishi aende darasani kusoma kuhusu bima.
Ila watanzania wengi sana wana uelewa mdogo mtu anashindwa hata kujua bima inafanyaje kazi anakuja kusema alikopa Kenya alivyomaliza akarudishiwa bima, hamna kitu kama hicho ELIMU ELIMU ELIMU. Tujifunze kuhusu vitu kama security, bond, insurance, collateral n.k ni mambo ya finance, uchumi na hata sharia za mikataba. Tutumie mitandao vizuri haya mambo yamejaa humu tena bureee. Tunashinda insta tu kupigana vijembe wakati internet ina kila kitu cha kukukomboa kiakili na kukutoa kwenye ujinga
 
Mkuu Kuna nyumba imetangazwa karibu mara ya sita sasa na mkopaji no marehemu imekaaje hii. Jamaa ni mtoto kwenye hiyo familia wazazi wake wamefariki wote, ndugu zake kaka na dada wamefariki kabaki yeye na wajukuu wa hiyo familia. Yeye ndio mtoto pekee wa marehemu akaenda kukopa 70M . Baada ya Kama mwaka amefariki mbona nyumba inapigwa mnada Kama marehemu hadaiwi.
Kwenye mikopo kuna option tofauti tofauti kutokana na makubaliano. Mikopo mingine unaweka bima kama ukifa au kupata ulemavu ambao hautaweza kufanya kazi tena basi bima inafidia na kuna mingine ambayo mtu anaweka dhamana kitu/mali kama nyumba shamba n.k kwa hiyo option ya pili ukifa wanachukua dhamana kufidia mkopo.

Mara nyingi mikopo ya kukata kwenye mishahara ndio uwa inawekewa bima au mingine mafao yako na mikopo mingi ya biashara dhamana uwa ni mali/vitu

Huyo ambaye amefariki na nyumba yake inauzwa atakuwa aliweka hiyo nyumba kama dhamana ya kukopea na kwenye mkataba inaandikwa kabisa ukishindwa kulipa kwa sababu zozote ikiwemo kifo dhamana itatumika kufidia deni
 
Nimefurahi mada ni nzuri ila Cha kusikitisha ni kwamba watu wanambishia mtoa mada bila kuwa na sababu za kubisha. Mimi nimewahi kukopa lakini sikusaini sehemu yoyote inayoonesha kuingia kwangu mkataba na bima, kwa maoni yangu tusome zile fomu kwa umakini na tuje na majibu hapa kwa wadau au piga picha hiyo page inayoelezea bima ya mkopo.mimi naamini bima hii haiwezi kufanana na bima ya magari au nyumbani, hebu tukubali kupokea mawazo mapya na tuyachunguze kama yana ukweli au la tusiwe na mawazo mgando. Nimefurahi jamaa kaleta challenge kubwa japo inaonekana simple kwa wale simple mind.
 
Kuna vitu viwili hapa naanza kuwa na mashaka :-
(A)loan insurance
(B)loan security
Vipi wadau hivyo vitu vinafanana nafikiri kule bank wanatumia neno mojawapo Kati ya hayo
 
hivi mkuu nikiweka bond simu kwako ukanipa 120K kwa makubaliano nikilipa deni lako na riba uliyonipa unirudishie simu yangu, nikimaliza deni utakatalia simu yangu?
Yani Unaongea Vitu viwili tofauti mzee baba... Kaa ukijua Riba pale sip Bank kwamba umeweka hela wakutunzie Riba wanachukua hela yako kwamba Likitokea tatizo wao wahusike kulisolve mfano wewe unaweka Riba laki 2 lakini kwa Riba hio hio wai likitokea tatizo la Mil 2 watalisolve. BIMA means pesa zinachangwa kusaidia kutatua matatizo ya watu kwa urahisi yatakapotokea so kama wewe halijakupata tatizo kuna wenzako wamepatwa na majanga na pesa yako Obvious itatumika kusolve lile tatizo kama vile ambavyo pesa yao itatumika kusolve tatizo lako likutokea. HUWEZI DAI PESA YA BIMA KAMA NHIF ETI KISA HUJAUMWA NOOO[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] BIMA SIO BANK PALE UKITAKA HIVYO PELEKA HELA YAKO BANK IKAE.
 
  • Thanks
Reactions: Ctr
Ingekuwa unachosema ni sahihi basi makampuni ya Bima yasingestawi. Hela unayochajiwa Kw ajili ya bima ndio faida ya makampuni ya Bima pindi inapotokea umemaliza salama mkopo wako,

Ukipata hasara pesa hiyo ndio inachanganywa na nyingine za wenzako ku compesate majanga, ni kama kwenye magari tu
 
Nimefurahi mada ni nzuri ila Cha kusikitisha ni kwamba watu wanambishia mtoa mada bila kuwa na sababu za kubisha. Mimi nimewahi kukopa lakini sikusaini sehemu yoyote inayoonesha kuingia kwangu mkataba na bima, kwa maoni yangu tusome zile fomu kwa umakini na tuje na majibu hapa kwa wadau au piga picha hiyo page inayoelezea bima ya mkopo.mimi naamini bima hii haiwezi kufanana na bima ya magari au nyumbani, hebu tukubali kupokea mawazo mapya na tuyachunguze kama yana ukweli au la tusiwe na mawazo mgando. Nimefurahi jamaa kaleta challenge kubwa japo inaonekana simple kwa wale simple mind.
Tatizo la kifedha ni tatizo kama matatizo mengine tuu maana hata Kwenye bima zingine kinachotoka ni fedha...!!
 
Ingekuwa unachosema ni sahihi basi makampuni ya Bima yasingestawi. Hela unayochajiwa Kw ajili ya bima ndio faida ya makampuni ya Bima pindi inapotokea umemaliza salama mkopo wako,

Ukipata hasara pesa hiyo ndio inachanganywa na nyingine za wenzako ku compesate majanga, ni kama kwenye magari tu
Yani Hakuna utofauti hata Nukta hapa...!! Bima ya Mkopo sijui bodaboda...nyumba zote ni sawaa
 
Wakirudisha hiyo hela huo mfuko utakuaje sasa ili kesho uweze kumsaidia atakaepata hayo majanga? Ww hujapata ila pengine mwenzako kapata hiyo shida, hela yako na ya wengine imetumika kumlipia aliyepata shida. Bima huwa hairudishwi mkuu.. kwan kwa mfano ww hapo umetoa laki 2, alaf umekopa mil 50, ukapata shida wakat bado unadaiwa mil 40, unadhan hizo hela za kulipia hilo deni lako zinatoka wapi?
 
Mi nimemaliza mkopo iwaje nilipe fidia ya wengine bado jibu halijakaa sawa
Ww usingemaliza hiyo laki 2 inatosha kulipa mill 20? Jiulize hilo, hizo pesa ambazo ningejaziwa mm kama ningepata shida zinatoka wapi? Heb jiulize hayo maswali
 
mkuu madhumuni ya bima ya afya ni tofauti na bima ya mkopo... hii mikopo pamoja na kwamba wanakata bima pia kuna dhamana... mbna stanbic kenya walinirudishia, why hizi bank zetu za ndani hazirudishi?
Hiyo bima ndio itakuja kuzuia nyumba yako kuja kuuzwa kama ndio uliweka dhamana. Hiyo stanbik kenye labda ni trik yao tu ya kutafuta wateja ila mfuko hauwez kikua hapo uweze kukusaidia kesho ukipata shida.
 
Nimefurahi mada ni nzuri ila Cha kusikitisha ni kwamba watu wanambishia mtoa mada bila kuwa na sababu za kubisha. Mimi nimewahi kukopa lakini sikusaini sehemu yoyote inayoonesha kuingia kwangu mkataba na bima, kwa maoni yangu tusome zile fomu kwa umakini na tuje na majibu hapa kwa wadau au piga picha hiyo page inayoelezea bima ya mkopo.mimi naamini bima hii haiwezi kufanana na bima ya magari au nyumbani, hebu tukubali kupokea mawazo mapya na tuyachunguze kama yana ukweli au la tusiwe na mawazo mgando. Nimefurahi jamaa kaleta challenge kubwa japo inaonekana simple kwa wale simple mind.
Kanuni ya bima ni moja ingawa kuna bima za aina tofauti. Alicholeta mtoa mada ni mortgage insurance au loan insurance. Unapoingia mkataba na benki wao ndio wanaingia mkataba na kampuni ya bima na sio wewe. Mteja wa mkopo anachofanya ni kulipia premium ambayo benki inaipeleka kwenye kampuni ya bima na kama ikitokea mteja amekufa basi benki italipwa na kampuni ya bima.

Hapa mteja wa mkopo anakuwa kama third party kwani haingii moja kwa moja mkataba na shirika la bima bali benki ndio inaingia mkataka na bima ili kama ikitokea tatizo iweze ku-recover loss. Na pia hapa mteja wa mkopo hawezi kupewa insurance policy document kwani huo ni mkataba wa benki na bima.

Kuweka bima mkopo kuna manufaa sana maana ikitokea maafa basi mteja aliyepoteza uhai familia yake haitopata shida kwani bima itafidia deni tofauti na kuweka dhamana ya mafao au nyumba
 
mkuu roho ipi ya kwa nini? hiyo 200K sio ndogo ingekuwa ndogo wasingechukua..., stanbic bank branch ya kenya wao mbona walinirudishia mkuu...na kumbuka hao wanaoweka bond nyumba lakini pia wanakatwa hii bima kwenye mikopo wanayochukua sasa why wasirudishiwe pesa yao wanapomaliza deni lao
Huyu jamaa amekataa kuelewa
 
Habari zenu wanajamvi
Miaka sita (6) iliyopita nilichukua mkopo bank ya CRDB kwa dhamana ya utumishi na marejesho yakiwa yanakatwa moja kwa moja kwenye mshahara, moja ya masharti ya ule mkopo ilikuwa ni lazma ukatiwe bima dhidi ya kifo au ulemavu wa kudumu, maafisa mikopo wa CRDB walinielimisha vizuri sana kuhusu hii bima amabayo wanaikata kwenye kile kiasi ulichoomba mkopo, nadhani ni kama 200k+ kama sikosei.wakanielieza kwamba

Kile kiasi cha pesa kilichokatwa kwenye mkopo nilioomba kama Bima kinasimamia upotevu wa fedha,mali iliyokatiwa Bima kutokana na kutokuwepo kwa uaminifu kutoka kwa waajiri wakati wafanyakazi wakiwa kazini. Bima hii pia inasimamia usalama wamali iliyochukuliwa kama dhamana. Wakaendelea kusema,

Bima hiyo inalipia hasara ya fedha anayoipata mkopeshaji ( ambao ni wao CRDB Bank) kutokana na matatizo aliyopata mdeni kufuatia majanga ya kifo au ulemavu wa kudumu kabla hajamaliza kulipa deni. Husaidia kupunguza hasara ikilinganishwa na dhamana iliyowekwa. Kwa wakopaji wasio na dhamana za kazi Bima hii ina hakikisha familia ya mhanga haiachwi bila makazi au mzigo wa kuendelea kulipia deni linalodaiwa pale mkopaji anapofariki au kupata ulemavu wa kudumu.

HOJA YANGU
Deni langu lilikuwa la miaka mitano (5) na mwaka jana nilimalizana na hili deni, yaani hawanidai tena tangu mwaka jana, nilitegemea baada ya deni kumalizika hawa CRDB bank wanirudishie ile pesa yangu Zaidi ya 200K kwa vile mkopo wao tayari nimeurudisha wote pamoja na riba na bila usumbufu, mwanzoni mwa mwaka huu niliwatumia barua kuwakumbusha kuhusu kunirejeshea hii pesa hawajanijibu hadi leo, jana nimewatumia email kupitia kwa DG wao bado pia naona kimya.

Hii kitu imeekaaje kwa hapa bongo, au ndo bank inadhulumu wateja wao…, nakumbuka nilikopaga pesa stanbic bank nikiwa Kenya kwa mda wa mwaka mmoja na baada ya mkopo kuisha nikarejesehewa hii pesa tena wakani email kabisa kunitaarifu.

Najua wakopaji kwenye hizi taasisi za kifedha wako wengi na najua na wao hawajui kama wanatakiwa kurudishiwa hii pesa baada ya mikopo kumalizika , naombeni kujulishwa kama hapa bongo hii pesa huwa hairudi hata kama deni lao umemaliza lote?
Bima ya mkopo, maana yake ni kuwa pesa hiyo imepelekwa bima, iweje tene urudishiwe? Kama mkopo umelipwa pasipo tatizo maana yake ni kuwa bima ndiyo wamenufaika na fedha hiyo na siyo bank. Sasa iweje bank wakurejeshee pesa ya bima?

Bima za tahadhari yaani za magari, majumba, biashara, wafanyakazi nk zinazokatwa kila mwaka, je ukiisha mwaka bila kupata tatizo unarejeshewa?
 
Kanuni ya bima ni moja ingawa kuna bima za aina tofauti. Alicholeta mtoa mada ni mortgage insurance au loan insurance. Unapoingia mkataba na benki wao ndio wanaingia mkataba na kampuni ya bima na sio wewe. Mteja wa mkopo anachofanya ni kulipia premium ambayo benki inaipeleka kwenye kampuni ya bima na kama ikitokea mteja amekufa basi benki italipwa na kampuni ya bima.

Hapa mteja wa mkopo anakuwa kama third party kwani haingii moja kwa moja mkataba na shirika la bima bali benki ndio inaingia mkataka na bima ili kama ikitokea tatizo iweze ku-recover loss. Na pia hapa mteja wa mkopo hawezi kupewa insurance policy document kwani huo ni mkataba wa benki na bima.

Kuweka bima mkopo kuna manufaa sana maana ikitokea maafa basi mteja aliyepoteza uhai familia yake haitopata shida kwani bima itafidia deni tofauti na kuweka dhamana ya mafao au nyumba
Mi sikuingia mkataba na bima na nimrkopa na hela wamekata wapeleke bima. Ikitokea nimekufa ni kipi kitakacholinda shamba langu lisiuzwe?. Yaani si kwamba bank watapata malipo mara mbili. Kwenye familia yangu na kwenye bima wote tutalipa. Maana hakutakuwa na vielelezo vyovyote vya familia yangu kujinasua. Aliyeingia mkataba na bima ni bank mwenyewe. Inamaana mi kwenye bima sitambuliki ila nimewalipa!!
 
Mi sikuingia mkataba na bima na nimrkopa na hela wamekata wapeleke bima. Ikitokea nimekufa ni kipi kitakacholinda shamba langu lisiuzwe?. Yaani si kwamba bank watapata malipo mara mbili. Kwenye familia yangu na kwenye bima wote tutalipa. Maana hakutakuwa na vielelezo vyovyote vya familia yangu kujinasua. Aliyeingia mkataba na bima ni bank mwenyewe. Inamaana mi kwenye bima sitambuliki ila nimewalipa!!
yes hata mimi ni hivi mkuu thats why nataka wanirudishie pesa yangu
 
Bima ya mkopo, maana yake ni kuwa pesa hiyo imepelekwa bima, iweje tene urudishiwe? Kama mkopo umelipwa pasipo tatizo maana yake ni kuwa bima ndiyo wamenufaika na fedha hiyo na siyo bank. Sasa iweje bank wakurejeshee pesa ya bima?

Bima za tahadhari yaani za magari, majumba, biashara, wafanyakazi nk zinazokatwa kila mwaka, je ukiisha mwaka bila kupata tatizo unarejeshewa?
Mi sikuingia mkataba na bima na kipindi nakopa hela wamekata bank sijui kama walipeleke bima, na sijui kama bima wananitambua mimi kama mteja wao na mimi siwafahamu wao
 
Hivi mfano umekatia BIMA Passo yako au Vits then hiyo gari haikupata ajali wakati huo,so bima ikiexpire hua tunakwenda kudai hiyo hela uliyokatia bima?,mfano huu hauna tofauti na hii ya bank
 
Habari zenu wanajamvi
Miaka sita (6) iliyopita nilichukua mkopo bank ya CRDB kwa dhamana ya utumishi na marejesho yakiwa yanakatwa moja kwa moja kwenye mshahara, moja ya masharti ya ule mkopo ilikuwa ni lazma ukatiwe bima dhidi ya kifo au ulemavu wa kudumu, maafisa mikopo wa CRDB walinielimisha vizuri sana kuhusu hii bima amabayo wanaikata kwenye kile kiasi ulichoomba mkopo, nadhani ni kama 200k+ kama sikosei.wakanielieza kwamba

Kile kiasi cha pesa kilichokatwa kwenye mkopo nilioomba kama Bima kinasimamia upotevu wa fedha,mali iliyokatiwa Bima kutokana na kutokuwepo kwa uaminifu kutoka kwa waajiri wakati wafanyakazi wakiwa kazini. Bima hii pia inasimamia usalama wamali iliyochukuliwa kama dhamana. Wakaendelea kusema,

Bima hiyo inalipia hasara ya fedha anayoipata mkopeshaji ( ambao ni wao CRDB Bank) kutokana na matatizo aliyopata mdeni kufuatia majanga ya kifo au ulemavu wa kudumu kabla hajamaliza kulipa deni. Husaidia kupunguza hasara ikilinganishwa na dhamana iliyowekwa. Kwa wakopaji wasio na dhamana za kazi Bima hii ina hakikisha familia ya mhanga haiachwi bila makazi au mzigo wa kuendelea kulipia deni linalodaiwa pale mkopaji anapofariki au kupata ulemavu wa kudumu.

HOJA YANGU
Deni langu lilikuwa la miaka mitano (5) na mwaka jana nilimalizana na hili deni, yaani hawanidai tena tangu mwaka jana, nilitegemea baada ya deni kumalizika hawa CRDB bank wanirudishie ile pesa yangu Zaidi ya 200K kwa vile mkopo wao tayari nimeurudisha wote pamoja na riba na bila usumbufu, mwanzoni mwa mwaka huu niliwatumia barua kuwakumbusha kuhusu kunirejeshea hii pesa hawajanijibu hadi leo, jana nimewatumia email kupitia kwa DG wao bado pia naona kimya.

Hii kitu imeekaaje kwa hapa bongo, au ndo bank inadhulumu wateja wao…, nakumbuka nilikopaga pesa stanbic bank nikiwa Kenya kwa mda wa mwaka mmoja na baada ya mkopo kuisha nikarejesehewa hii pesa tena wakani email kabisa kunitaarifu.

Najua wakopaji kwenye hizi taasisi za kifedha wako wengi na najua na wao hawajui kama wanatakiwa kurudishiwa hii pesa baada ya mikopo kumalizika , naombeni kujulishwa kama hapa bongo hii pesa huwa hairudi hata kama deni lao umemaliza lote?
Mimi sijui sana lakini nimepata swali kutokana na bandiko lako.

Je, walikuambia kwamba hiyo fedha ya bima utarudishiwa?

Ninavyofahamu mimi ni kwamba huduma za bima zinatumia mfumo wa kuchangiana nikiwa na maana kuwa kama ulikopa M5 ukalipia bima 200k halafu ikatokea hauwezi kulipa benki itakua imepata hasara.Hivyo kinachofanyika ni kutumia fedha nyingine za bima kutoka kwa wateja wengine ili kufidia hasara.

Hata magari tunakatia bima na pale inapoisha hata kama hujawahi kuitumia hela yako hairudi na utaikatia bima nyingine.
 
Back
Top Bottom