Kwanini mabenki mengine hayapunguzi riba?

lendila

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2012
Posts
5,806
Reaction score
4,370
Kwanini mabank mengine hayapunguzi riba,na kuongeza muda wa mkopo kama yalivyofanya baadhi ya bank?
 
Nenda kaombe mkopo kwa zile Benki zilizopunguza riba na kuongeza muda wa mkopo ambazo bado achana nazo, mambo mengine mnajipa tabu bure tu.Kila kitu hakiwezi kuwa sawa. Benki nyingine sio kupunguza riba tu hazitoi kabisa mikopo masharti yao ni Kama unaomba VIZA ya CANADA.
 
Kuna Banks ambazo credibility zake zipo juu..

Zimeshatengeneza majina " Brand " all over the World na hazibabaishwi sana na yanayoendelea katika Banks nyingine..

Mfano Barclays Bank, Citi Bank, Standard Chartered Bank...
Hizi ni Brand kubwa.

Usitegemee kila kitakachofanywa na Banks nyingine mfano kwenye hili la kupunguza riba nazo itakuwa ivyo.
 
Barclays wameshusha nao
 
Tatizo mikopo Sasa hivi hailipiki kabisa
 
Ni kweli mkuu. Tena hizi global brands kwa kiasi kikubwa zinashughulika na makampuni makubwa duniani kama Barrick, Exxon, Agrium, Monsanto na kadhalika.

Na zinaweza zisishushe riba lakini kwa kiasi kikubwa zinanunua sana amana za serikali. Kwa hao jamaa kuwa na amana za bilioni 800, 900 na hata trilioni 1 sio shida.

Na hata mkopo wa trilioni 3.3 tuliochukua kwa ajili ya SGR utalipiwa hapa hapa kupitia Standard Chartered ya Tanzania.
Ndio maana hawababaiki na moves za mabenki mengine kama NMB na CRDB
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…