Matanga
JF-Expert Member
- Nov 13, 2019
- 2,281
- 3,976
MAKOCHA WAZAWA WANAVYOKUBALI KUACHWA NA MUDA KUELEKEA SOKA LA KISASA NA LA KISHINDNI
Tanzania ni moja ya Nchi iliyobarikiwa kuwa na vijana wengi wenye Taranta ya kusakata kabumbu kwa umaridadi mkubwa sana, kwa miaka mingi sasa Nyota wengi wamepita wakina Kitwana Manara, Abeid Mziba, Mohammed Hussein "Mmachinga", Leodgar Tenga, Bakari Marima "Jembe ulaya", Adolf Richard, Jamal Malinzi, Selemani Matola, Mussa Hassan "mgosi" na wengine wengiii.
Kwa upande wa ulaya kuna kawaida ya wachezaji wanapomaliza kalia zao za Soka huwa wanaendelea kuutumikia mpira kwenye nafasi Tofautitofauti ikiwemo ukocha na uongozi kwenye nafasi mbalimbali kwenye Soka. Kwa hapa nyumbani pia swala hili lipo Japo sio kwa kiasi kikubwa kam wenzetu kule Duniani. Kuna baadhi ya wachezaji wanaamua kukaa Nje ya Soka Mara baada ya kumaliza maisha yao ya uchezaji. Lakini baadhi yao pia wanaendelea kuhudumu kwenye tasnia ya Soka kama wachambuzi, Makocha, viongozi wa mpira.
Katika soka letu Tuna makocha waliowahi kucheza mpira lakini pia tunao wale ambao hawajawahi kucheza kabisa ama walicheza kwenye madaraja ya chini.
Karamu yangu inanishawishi hii Leo kuandika kuhusu Jinsi ambavyo walimu wetu wa Soka (makocha) wanakubali kuachwa na muda huku wakipigwa bao na makocha wa mataifa ya hapahapa Africa ya mashariki na kati katika kuzisaka Ajira Nje ya nchi zao kama Burudi, Uganda, Kongo nakadhalika.
Makocha wetu hawana uthubutu kwa kiasi kikubwaa, ni idadi ndogo sana ya makocha Raia wa Tanzania ambao walishawahi kwenda nje ya nchi kufundisha Soka. Tatizo ni uthubutu, kazi ya ukocha ni kazi ambayo Nafasi ikiwepo kwenye timu Fulani lazima upekeke CV zako kuomba kazi. Na hapa ndipo makocha wa Uganda, Burundi, Kenya, na mataifa mengine wanapotupiga bao. Naamini Tuna makocha wengi wenye CV nzuri za kufundisha Soka nje ya nchi, lakini hawana utayari kiasi kikubwa.
Pia mchezo wa Soka ni sayansi inayobadilika jinsi muda unavyokwenda, mbinu za miaka ya tisini ni tofauti na za sasa. Makocha wetu hawana kawaida ya kuhudhuria kozi mbalimbali zinazofanyika hapa kwetu na Nje ya nchi huko ili kuongeza maarifa zaidi kimbinu. Ukitaka kulijua hili Fwatilia CV za makocha kama Mwinyi Zahera, Ettiene Ndayiragije utang'amua ni kozi ngapi wamehudhuria kwenye maisha yao ya ualimu wa Mpira na wanakwambia wataendelea kusoma zaidi.
Inaumiza sana kuona makocha wengii wa hapahapa Afrika mashariki wamejazana kwenye ligi yetu wakati huohuo wakwetu wanang'ang'ania kubakia hapa kwetu miaka mingii, badala ya kwenda kutafuta changamoto mpya Nje ya nchi.
Ettiene Ndayiragije, Hitimana thiery, Haruna Hererimana, Noely Mwandila, Jackson Mayanja, Masoud Juma, Hao ni baadhi ya makocha kwa Siku za karibuni waliokuja kufundisha Hapa Tanzania wakitokea ukanda huuhuu wa Afrika mashariki na kati.
Kumbukumbu zangu zinanionyesha idadi ndogo ya makocha wetu waliojaribu kutoka Nje ya nchi,, Boniface Mkwasa "master", Dennis Kitambi na Sandey Kayuni.
Ni muda wakuamka sasa walimu wetu wa soka, Muda unatuacha mbalii, kwani hatuoni Faida wanazopata makocha wakigeni wakija hapa kwetu?? Timu ya Taifa ya Burundi imepata kipa kijana mwenye uwezo mkubwa sana Jonathan Nahimana kupitia kwa Ettiene Ndayiragije aliekuja Tanzania kufundisha na kumpa nafasi kubwa ya kucheza hali iliyopelekea kijana Huyo kuimalika na kuitwa Timu ya Taifa ya Burundi ilokwenda AFCON.
Hivyo hata sisi tunaweza tukanufaika na walimu wazawa kutoka nje ya nchi kwasababu wanaweza wakatengeneza njia kwa wachezaji wetu kucheza Soka la kulipwa na kupata wachezaji wakomavu zaidi kwenye timu yetu ya Taifa, kama ambavyo akina Ndayiragije wanafanya kuwapa nafasi wachezaji wa Mataifa yao (Emmanuel Mvuyekure, Jonathan Nahimana, Yusuph Ndikumana)
Selemani Matora,Malale Hamsini, Juma Mwambusi, Amri Said,Kessy Mziray,Adolf Richard,Hemed Morroco,Iddy Cheche, Juma Mgunda,Fred Felix minziro "Baba isaya" Amkeni Amkeni Amkeni,wakati unatuacha , tusikubali kupigwa bao kiurahisi na majirani zetu Hawa
Sent using Jamii Forums mobile app
Tanzania ni moja ya Nchi iliyobarikiwa kuwa na vijana wengi wenye Taranta ya kusakata kabumbu kwa umaridadi mkubwa sana, kwa miaka mingi sasa Nyota wengi wamepita wakina Kitwana Manara, Abeid Mziba, Mohammed Hussein "Mmachinga", Leodgar Tenga, Bakari Marima "Jembe ulaya", Adolf Richard, Jamal Malinzi, Selemani Matola, Mussa Hassan "mgosi" na wengine wengiii.
Kwa upande wa ulaya kuna kawaida ya wachezaji wanapomaliza kalia zao za Soka huwa wanaendelea kuutumikia mpira kwenye nafasi Tofautitofauti ikiwemo ukocha na uongozi kwenye nafasi mbalimbali kwenye Soka. Kwa hapa nyumbani pia swala hili lipo Japo sio kwa kiasi kikubwa kam wenzetu kule Duniani. Kuna baadhi ya wachezaji wanaamua kukaa Nje ya Soka Mara baada ya kumaliza maisha yao ya uchezaji. Lakini baadhi yao pia wanaendelea kuhudumu kwenye tasnia ya Soka kama wachambuzi, Makocha, viongozi wa mpira.
Katika soka letu Tuna makocha waliowahi kucheza mpira lakini pia tunao wale ambao hawajawahi kucheza kabisa ama walicheza kwenye madaraja ya chini.
Karamu yangu inanishawishi hii Leo kuandika kuhusu Jinsi ambavyo walimu wetu wa Soka (makocha) wanakubali kuachwa na muda huku wakipigwa bao na makocha wa mataifa ya hapahapa Africa ya mashariki na kati katika kuzisaka Ajira Nje ya nchi zao kama Burudi, Uganda, Kongo nakadhalika.
Makocha wetu hawana uthubutu kwa kiasi kikubwaa, ni idadi ndogo sana ya makocha Raia wa Tanzania ambao walishawahi kwenda nje ya nchi kufundisha Soka. Tatizo ni uthubutu, kazi ya ukocha ni kazi ambayo Nafasi ikiwepo kwenye timu Fulani lazima upekeke CV zako kuomba kazi. Na hapa ndipo makocha wa Uganda, Burundi, Kenya, na mataifa mengine wanapotupiga bao. Naamini Tuna makocha wengi wenye CV nzuri za kufundisha Soka nje ya nchi, lakini hawana utayari kiasi kikubwa.
Pia mchezo wa Soka ni sayansi inayobadilika jinsi muda unavyokwenda, mbinu za miaka ya tisini ni tofauti na za sasa. Makocha wetu hawana kawaida ya kuhudhuria kozi mbalimbali zinazofanyika hapa kwetu na Nje ya nchi huko ili kuongeza maarifa zaidi kimbinu. Ukitaka kulijua hili Fwatilia CV za makocha kama Mwinyi Zahera, Ettiene Ndayiragije utang'amua ni kozi ngapi wamehudhuria kwenye maisha yao ya ualimu wa Mpira na wanakwambia wataendelea kusoma zaidi.
Inaumiza sana kuona makocha wengii wa hapahapa Afrika mashariki wamejazana kwenye ligi yetu wakati huohuo wakwetu wanang'ang'ania kubakia hapa kwetu miaka mingii, badala ya kwenda kutafuta changamoto mpya Nje ya nchi.
Ettiene Ndayiragije, Hitimana thiery, Haruna Hererimana, Noely Mwandila, Jackson Mayanja, Masoud Juma, Hao ni baadhi ya makocha kwa Siku za karibuni waliokuja kufundisha Hapa Tanzania wakitokea ukanda huuhuu wa Afrika mashariki na kati.
Kumbukumbu zangu zinanionyesha idadi ndogo ya makocha wetu waliojaribu kutoka Nje ya nchi,, Boniface Mkwasa "master", Dennis Kitambi na Sandey Kayuni.
Ni muda wakuamka sasa walimu wetu wa soka, Muda unatuacha mbalii, kwani hatuoni Faida wanazopata makocha wakigeni wakija hapa kwetu?? Timu ya Taifa ya Burundi imepata kipa kijana mwenye uwezo mkubwa sana Jonathan Nahimana kupitia kwa Ettiene Ndayiragije aliekuja Tanzania kufundisha na kumpa nafasi kubwa ya kucheza hali iliyopelekea kijana Huyo kuimalika na kuitwa Timu ya Taifa ya Burundi ilokwenda AFCON.
Hivyo hata sisi tunaweza tukanufaika na walimu wazawa kutoka nje ya nchi kwasababu wanaweza wakatengeneza njia kwa wachezaji wetu kucheza Soka la kulipwa na kupata wachezaji wakomavu zaidi kwenye timu yetu ya Taifa, kama ambavyo akina Ndayiragije wanafanya kuwapa nafasi wachezaji wa Mataifa yao (Emmanuel Mvuyekure, Jonathan Nahimana, Yusuph Ndikumana)
Selemani Matora,Malale Hamsini, Juma Mwambusi, Amri Said,Kessy Mziray,Adolf Richard,Hemed Morroco,Iddy Cheche, Juma Mgunda,Fred Felix minziro "Baba isaya" Amkeni Amkeni Amkeni,wakati unatuacha , tusikubali kupigwa bao kiurahisi na majirani zetu Hawa
Sent using Jamii Forums mobile app