Kwanini matokeo ya PRIVATE CANDITATE huwa si mazuri?????

Kitanto

Member
Joined
Apr 6, 2011
Posts
26
Reaction score
1
Mimi kwa mtazamo wangu si vizuri kwamba kila mwaka watahiniwa wa kujitegemea huwa hawaambulii kitu.,naona dhana hii imekaririwa sana. Naomba wizara ibadilishe utaratibu huo.
 
maandalizi hafifu....na hili ni tatizo la watahiniwa wenyewe,hawajiandai but wanataka matokeo!
 
maandalizi hafifu....na hili ni tatizo la watahiniwa wenyewe,hawajiandai but wanataka matokeo!

dah! Mkuu ungejua usingelisema ulichokisema, ila poa tu kwa kuwa "isiyokuwasha hujailamba" ni msemo wa wahenga lakini sio wangu
 
Mmmh ! Lakini nahic siyo hujma bali PC hawana maandalizi ya kutosha huku wakibakia kuwa walalamishi tu. Mi naamini NECTA wako fair.
 
Hujui kuwa pass mark yao iko juu zaidi halafu wao wenyewe hawjiandai vizuri wakat mwingine wanasoma ili mradi kusoma tu hawaangalii hata syllabus inataka nini na kusoma kwenyewe wanasoma past paper na wala sio kuelewa somo husika
 
Mimi kwa mtazamo wangu si vizuri kwamba kila mwaka watahiniwa wa kujitegemea huwa hawaambulii kitu.,naona dhana hii imekaririwa sana. Naomba wizara ibadilishe utaratibu huo.

Sababu nyingine kubwa ni kwamba Private Candidates hawana Course Work au tuziite Taarifa ya Mwanafunzi kama wengine ambao taarifa zao za kila mwaka zinatumwa NECTA. Na hizo Course zina nafasi katika mtihani wa mwisho. Kwa Private Candidate, akipata A au D basi ndiyo hicho alichokipata kwenye Paper.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…