Kwanini matusi dhidi ya Rais Magufuli hayakomi kwenye mtandao?

Kwanini matusi dhidi ya Rais Magufuli hayakomi kwenye mtandao?

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
Wengi washakamatwa kwa kosa la kumtukana rais, na kila anapo kamatwa mtu kwa kosa la kumtukana rais mtu huyo hutangazwa na huishia kupelekwa mahakamani.

Pamoja na hatua zote hizi za kisheria wanazo chukuliwa watu hawa lakini kila uchao ukipita katika mitandao unakutana matusi dhidi Mh rais, au dhidi ya kiongozi yeyote wa serikali.

Unadhani hii inasababishwa na nini?

A. Watu wameichoka sana CCM na serikali kiasi wasiogope lolote? Lakini kama wameichoka kwanini rais Magufuli alishinda?

B. Vitendo vya kumtukana rais ni kosa kama makosa mengine kama vile ya wizi. Kila siku wezi wanafungwa na wengine kuchomwa moto, lakini watu bado wanaendelea kuiba.

C. Vijana wanachochewa na wanasiasa wa upinzani, na wanajua wakikamatwa makada wa vyama hivyo watafanya harambee ya michango, michango ambayo pia kwa namna moja humnufaisha mchangiwa. Ina maana hii ishakuwa fursa aka DILI?

D. Vijana kupenda sifa na kujijenga kisiasa, na ikichangiwa na ile kasumba kuwa ili uwe mpinzani wa kweli dhidi ya serikali ni lazima ufungwe au upate msukosuko kama Mandera au Mwalimu Nyerere. Je, wanamtukana rais na viongozi wenzake kwasababu ya kutafuta "kiki"??

E. Jamii imemomonyoka kimaadili na ndio maana kumekithiri matusi kwenye mitandao, si kwa rais wetu tu, hata hao wanaotukana pia ukifuatilia huwa wanatukanana wenyewe kwa wenyewe.

F. Hotuba za viongozi wa serikali hasa za Mh Rais kujaa vijembe kwa viongozi wa upinzani na wafuasi wao, vijembe ambavyo mara zote na siku zote huibua mijadala kwenye mitandao ya jamii, na katika mijadala hiyo wafuasi wa watu waliopigwa vijembe hutumia kurejesha vijembe hivyo Mh Rais. Kwasababu hiyo, wadhani Mh Rais akiacha vijembe kutapunguza matusi dhidi yake ukilinganisha na hatua hii ya kamatakamata?

Njano5
0622845394
 

Attachments

  • 1473045230775.jpg
    1473045230775.jpg
    33.3 KB · Views: 106
Mi nadhani hapa yoyote mwenye idea ya namna ya kuendeleza nchi yetu ambayo ni tofauti na ya mheshimiwa aipresent kwa namna ya kistaarabu bila kutumia lugha ya matusi.labda kwa jeshi letu pia lisijikite kwebye kukamata wanaomkashifu na kumdhihaki rais tu.wengi wanadhihakiwa mitandaoni na hawana pa kukimbilia.hao pia wakamatwe na juchukuliwa hatua
 
Kukamatwa na kufikishwa mahakamani......

MAHAKAMA (kwa mawazo yangu ) ni DOA (pia kansa) itakayokwamisha sana juhudi za kusonga mbele

(Popote penye rushwa usitegemee kitu)
 
Hili huenda likasababishwa na ugumu wa maisha. Siku ugumu wa maisha ukikoma/ kupungua basi 'sifa na utukufu' kede kede atamwagiwa mhishimiwa...
 
Nawe huna lolote sema ulitaka uje umuanike huku huyo mtu unaedai kamtukana Rais..lakini ukiona watu wanazidi kukutukana na kukusema vibaya japo unawafungulia mashtaka inabidi ujitathimini kuwa nakosea wapi au kuna haja ya kuwaandama watu hao,je wanataka nini hasa?
 
Huu sasa ni Umoja wa Kumsifia Makufuli

Naona umekuja kumchongea adui yako
Hiyo screenshot km huyo jamaa ni jina lake halisi duuh asubiri kubebwa na difenda
 
Utashambuliwa wewe badala ya maswali yako kujibiwa.

Hata hivyo ondoa hiyo attachment uliyoitoa FB....maana umeweka bila ridhaa ya mhusika.
 
KWASABABU huko jela bado kuna nafasi y kuwachukua watu kama hao

Wengi washakamatwa kwa kosa la kumtukana rais, na kila anapo kamatwa mtu kwa kosa la kumtukana rais mtu huyo hutangazwa na huishia kupelekwa mahakamani.

Pamoja na hatua zote hizi za kisheria wanazo chukuliwa watu hawa lakini kila uchao ukipita katika mitandao unakutana matusi dhidi Mh rais, au dhidi ya kiongozi yeyote wa serikali.

Unadhani hii inasababishwa na nini?

A. Watu wameichoka sana CCM na serikali kiasi wasiogope lolote? Lakini kama wameichoka kwanini rais Magufuli alishinda?

B. Vitendo vya kumtukana rais ni kosa kama makosa mengine kama vile ya wizi. Kila siku wezi wanafungwa na wengine kuchomwa moto, lakini watu bado wanaendelea kuiba.

C. Vijana wanachochewa na wanasiasa wa upinzani, na wanajua wakikamatwa makada wa vyama hivyo watafanya harambee ya michango, michango ambayo pia kwa namna moja humnufaisha mchangiwa. Ina maana hii ishakuwa fursa aka DILI?

D. Vijana kupenda sifa na kujijenga kisiasa, na ikichangiwa na ile kasumba kuwa ili uwe mpinzani wa kweli dhidi ya serikali ni lazima ufungwe au upate msukosuko kama Mandera au Mwalimu Nyerere. Je, wanamtukana rais na viongozi wenzake kwasababu ya kutafuta "kiki"??

E. Jamii imemomonyoka kimaadili na ndio maana kumekithiri matusi kwenye mitandao, si kwa rais wetu tu, hata hao wanaotukana pia ukifuatilia huwa wanatukanana wenyewe kwa wenyewe.

F. Hotuba za viongozi wa serikali hasa za Mh Rais kujaa vijembe kwa viongozi wa upinzani na wafuasi wao, vijembe ambavyo mara zote na siku zote huibua mijadala kwenye mitandao ya jamii, na katika mijadala hiyo wafuasi wa watu waliopigwa vijembe hutumia kurejesha vijembe hivyo Mh Rais. Kwasababu hiyo, wadhani Mh Rais akiacha vijembe kutapunguza matusi dhidi yake ukilinganisha na hatua hii ya kamatakamata?

Njano5
0622845394
 
Kama yote hapo juu ndio sababu unategemea nini pia urais ni tasisi kama mtu anafanya nje yake ujue shida zitaingia tuu hakuna namna serikali moja ya chama kimoja hicho hicho ndani ya mwaka mmoja mambo tofauti kuna kitu hakipo sawa tumuombee mambo yawe kama tunavyotarajia.
 
Wapinzani kila siku wapo usitegemee hayo matusi yataisha leo au kesho. Ugumu wa maisha pia unachangia na kwa kawaida binadamu hatuna ile kasumba ya kukubali kuwa tumekosea hivyo huwa tunatafuta kitu cha kukilaumu kwa matatizo yetu, Hivyo rais ametokea kuwa kitu hicho kwa wakati huu miongoni mwa watu wengi.
 
Tatizo ni kutokujua maana halisi ya tusi.
Wengi wakiambiwa ukweli wasipoukubali huubadili ukweli huo na kuuita matusi.
Hivi kwa mfano, mi ni mwanaume mweusi, mwembamba .. mtu akinisema kuhusu weusi na wembamba wangu atakuwa amenitukana? Hapana.
Mimi sijui kuendesha gari .. hivi nikiongelea uendeshaji wa gari mbele ya madereva nikakosea mahali; mmoja wa madreva hao akaniita mjinga atakuwa amenitusi - Hapana.
Hivyo tujenge tabia ya kujikubali kwa hali tulizonazo na pale tutakaposemwa tusihamaki - badala yake tujirekebishe.
MWENYE MASKIO NA ASIKIE!
 
Ukisikia unaa ndio huu sasa.Kilichokufanya uattach na hayo uliyoyatoa huko FB ni nini?
Na huyu ni miongoni mwa wale ..... Km alikuwa anataka kufikisha ujumbe wake kwa watu fulani ilikuwa sio lazima aattach na hizo post za FB.Nway umuombealo mwenzako na wewe ndilo litakalo kutokea either direct or indirect.Mkuu unachoma kibanda asee!!
 
Back
Top Bottom