econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 20,189
- 29,663
Katika hotuba yake ya Jana, Mwenyekiti wa CHADEMA alitumia muda kutetea maridhiano na kuonesha ya kwamba Kuna mafanikio tumepata baada ya kufanya maridhiano.
Kwa mfano anadai tumeweza kujenga jengo la makao makuu baada ya kupokea Ruzuku, pia amedai kuwa tumeruhysiwa kufanya siasa na kufutiwa kesi zaidi ya mia nne.
Shida yangu sio hayo mafanikio ya Maridhiano Bali ni unduminakuwili wa Mwenyekiti baada ya juzi yeye mwenyewe kudai ya kwamba CCM waliwaingiza mjini ila Leo anadai mafanikio yalikuwa makubwa.
Nimeshangaa Sana. Hakuna katiba Mpya, sheria za uchaguzi za hovyo na chama kimepata Asilimia 0.78 kwenye serikali za mitaa kutokana na uharamia wa CCM na serikali yake. Inakuaje Mbowe yeye anaangalia Ruzuku na mikutano? Chama kimepoteza wanachama wake katika Hali ya kutatanisha na wengine wamekufa wakati wa huo uchaguzi, yeye Mbowe mafanikio yake ni Ruzuku tu?
Ni kwanini Mbowe anashangilia Vitu ambavyo vilikuwepo kabla na kuviaacha ambavyo ni vya msingi?
Kwa mfano anadai tumeweza kujenga jengo la makao makuu baada ya kupokea Ruzuku, pia amedai kuwa tumeruhysiwa kufanya siasa na kufutiwa kesi zaidi ya mia nne.
Shida yangu sio hayo mafanikio ya Maridhiano Bali ni unduminakuwili wa Mwenyekiti baada ya juzi yeye mwenyewe kudai ya kwamba CCM waliwaingiza mjini ila Leo anadai mafanikio yalikuwa makubwa.
Nimeshangaa Sana. Hakuna katiba Mpya, sheria za uchaguzi za hovyo na chama kimepata Asilimia 0.78 kwenye serikali za mitaa kutokana na uharamia wa CCM na serikali yake. Inakuaje Mbowe yeye anaangalia Ruzuku na mikutano? Chama kimepoteza wanachama wake katika Hali ya kutatanisha na wengine wamekufa wakati wa huo uchaguzi, yeye Mbowe mafanikio yake ni Ruzuku tu?
Ni kwanini Mbowe anashangilia Vitu ambavyo vilikuwepo kabla na kuviaacha ambavyo ni vya msingi?