LGE2024 Kwanini Mkoa wa Rukwa wameshika Mkia na Kujitokeza kwa uchache kujiandikisha kupiga kura?

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Nimeshangaa sana kuona Mkoa wa Rukwa zaidi ya 30% ya wananchi hawajajitokeza katika kujiandikisha katika daftari la mkazi kwa ajili ya kupiga kura ya kuchagua viongozi wao mwezi ujao. Hii ni kwa kuwa ni 64.58% pekee ndio waliojitokeza kujiandikisha.

Hivyo kuufanya mkoa huu kushika nafasi ya Mwisho kabisa yaani mkiani kabisa. Sijaelewa nini tatizo ya Mkoa huu kufanya vibaya kwa zoezi hili muhimu kabisa na lenye kumpa nafasi mwananchi kupaza Sauti yake katika sanduku la kura.

Kazi iendelee Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Soma Pia: Waziri Mchengerwa: Jumla ya wapiga kura milioni 31, 282,331 wamejiandikisha kupiga kura Uchaguzi Serikali za Mitaa 2024

Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Nenda kamuulize mkuu wao wa Mkoa atakuwa na jibu sahihi.
 
Mmeteka na kumpeleka kusikojulikana kiongozi wao wa Chadema halafu mnataka wawachekee tu!
 
Uchache wa waliojiandikisha ni zao la chaguzi tata zilizopita(2019&2020) Tafakari kwa kurejea 2019 na 2020. Hatupaswi kulaumu kwa kupata mazao duni ilhali kulikuwa na palizi duni.
 
wako bize na uvuvi wa samaki, wafipa hawapendagi ujinga
 
Wamekuwa wa mwisho kwenye hii idadi ya kupika au ya kweli?
 
ni zamu ya elimu kushuka Rukwa sasa
Ni wapi Tanzania elimu iko juu hadi useme itashuka huko Rukwa? Au ule uafaulu hadi wasiojua kuandika majina yao ndio unakudanganya?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…