Kwanini Mkuu wa Majeshi hapewi heshima?

Isue inayojadiliwa ni Escort wewe unaanzisha story zako zakufikirika eti sijui fulani kupindua sijui nini. Stick kwenye Hoja. Halafu hata hayo uliyoandika kwa kweli Hujui lolote zaidi kuwa ni ILUSION tu.
 
Nadhani kunakuchanganya mada mtoa mada anauliza kusafishiwa njia nasio msafara
Kova akiwa anaenda nakutoka kazini magari huitwa mpaka yaishe vivyo hivyo kwa IGP huyu huwa ananikera zaidi ukitaka kujuwa hajapita tumia barabara ya muhimbili kuelekea town pale salenda mtasimama zaidi ya 15dk mpaka apite wakati jamaa CDF akikuta wamesimamisha magari nayeye anasimama anasubiri mpaka aruhusiwe
 

Halafu kuku wa chini kabisa utakuta wanapiga trafik eti wanachelewa!!!!!!.
 
CDF akichelewa kazini nani wa kumuuliza.?
kama ana sababu za msingi kuwahi anapokwendwa sidhani kama atakaa kusubiria foleni na akikaa hivo sidhani kama itakua ni busara.
 
Nakumbuka, ilitokea mara moja Afande Ma.hit.a alisafishiwa njia kwa pikipiki kadhaa mwaka fulani, haikujirudia tena.
 
Umechanganya, mkuu wa majeshi ni mteule wa rais, akiwa kama kiongozi wa majeshi yote, na amiri jeshi mkuu ni raisi ambae indie mwenye amri ya mwisho katika kuamua masuala ya kiusalama wa nchi ikiwemo amri ya nchi kuingia vitani
 
mkuu jamaa ni mkuu wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), lazima awe humble kwa wananchi anaowalinda,ila wale wengine ni viongozi wa watumishi kwahio lazima wawe wababe, hivi mkuu wa jeshi la polisi - lazima awe na hulka za kipolisi,
 

kweli "dawa" mbaya, unasema kanali/capt vyeo vya chini? labda kwenye jeshi la joseph konyi.
 
Mkuu wa majeshi kila anapokuwa kuna msafara ...gari yake Ina Nyota Nne ...na gari Moja au Mbili nyuma Zenye namba private ...uwepo wa kimuli muli hutegemea Hali ...especially kwa Mkuu tulie naye Hana Makuu na hutumia sweepers tu pale anapokuwa na uharaka ...Zaidi ukiwa nyuma yake hata bila sweeper traffic wanakuwa wamepewa signal na utaona wanaita Magari ya upande wake .....anapita
Hata Mkuu wa TISS naye kwa wanaojuwa wanaweza ku spot msafara wake wa Magari meusi yenye private number ...hadi UWE unajuwa Ndio utaweza ku spot ..entourage yake .

Mkuu wa Majeshi nafasi yake ni namba mbili Baada ya Rais ....yeye Ana ripoti Moja kwa Moja kwa Rais ...sio kwa waziri ,waziri Mkuu au Makamu wa Rais ...ambao anawatii tu..., Ana access na Rais 24/7 ....hata usiku akiwa amelala Anao uwezo wa kuagiza aamswe ili waongee au amuone ...ikitokea hatari yeyote ya ulinzi na Usalama au maafa ..yeye Ndio mwenye jukumu la kukusanya taarifa Za vyombo vyote na kumpelekea Rais taarifa Rasmi ..muda wowote ...wakuu wote wa vyombo Vya Usalama ( Polisi ,Usalama ,magereza ,zimamoto etc ) yeye Ndio joint chief ..au mwenyekiti wa ulinzi na Usalama ( national security council )

Kwa Nguvu kubwa alionayo ...anatakiwa kuwa humble ...ili asionekane..kuwazidi waziri wake ,waziri Mkuu na Makamu HADHARANI ....kwenye Protocal arrangement ..anawapigia saluti ..lakini behind the scene wanajuwa yeye ni nani ...na anawazidi ...Sasa akianza kutembea na misafara Marefu ....na Nchi Hii ni ya kidemokrasia..atakuwa Ana send wrong message ...
 

Umemaliza yote kaka/ mdau. Inavyosemekana ni kuwa daily briefing ya hali ya Usalama hutolewa nae baada ya kupata kutoka Idara zote yaani Jeshi, UWT, Polisi, Magereza nk. Hivyo yeye ndo humpatia mkuu wa nchi. Hivyo ni kweli kabisa akawa ni Chief of Joint Security Organs kama Marekani wanavyofanya. Kule Marekani mwafrika pekee aliyewahi kushika cheo hicho ni Collin Powel.

Kama kuna anaejua zaidi atueleze lakini kwa asilimia kubwa ni sahihi kabisa yale uliyoyasema.
 
Hisia za kichwani kwako. Kwa taarifa yako kila chombo hapo kina wajibika kivyake kutoa taarifa ngazi za juu. Huwezi kusema mfano mkuu wa magereza atoe taarifa ya WAFUNGWA kwa mkuu wa Majeshi.
 
Hisia za kichwani kwako. Kwa taarifa yako kila chombo hapo kina wajibika kivyake kutoa taarifa ngazi za juu. Huwezi kusema mfano mkuu wa magereza atoe taarifa ya WAFUNGWA kwa mkuu wa Majeshi.

daa kweli nishida habari ni moja lakini kuelewa sasa ndio shidaa.unahisi kama mwenzio kakosea na ww ndio upo sahihi vilee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…