Kwanini Mmeniua?

Kwanini Mmeniua?

JMP Mchungu

Member
Joined
Jun 30, 2015
Posts
49
Reaction score
127
KWANINI MENIUA"
Mama baba acha kulia, akwilini sijafa mejilalia
Waloniua wanashangilia,moyo wangu unaumia
Bahati mbaya tajisemea,ukweli moyonpia ajua
Usifadhahika mama tulia,baba mimi natangulia
Askari kwanini meniua?,moyo wangu hujatulia.

Mauti angu mekusudia,bahat mbaya mwasema
Risasi watu mwawapigia, mtaulizwa kihama,
Langu lengo lapotea, watu washika tama
Vita pia yakaribia, wananchi sikate tamaa
Haki yenu pigania, watu meli yaanza kuzama
Askari kwanini meniua? Moyo wangu hujatulia.

Sauti ya uchungu kusikika,mbali yatokea
Uchungu wa uzazi wamshika,mama vumilia
Watu waishi kwa mashaka,amri juu kitokea
Demokrasia wanaibaka,wakubwa furahia
Wawaua bila shaka,damu yenu wachekelea
Askari kwanini meniua,moyo wangu hujatulia

Eti wapiga juu risasi, iweje chini ikaelekea
Askar wako kama fisi,roho za watu wazichukua
Watoto wenu wako kwa ofisi,wetu mwawaua
Maskin mtakula ngisi,viongoz wala yenu mioyo
Ukimya wenu makasisi,watu wanakula vinono
Askari kwanini meniua?moyo wangu hujatulia

Nahodha chombo kimekushinda,wacha kutuua
Mengi twajua japo makinda,mamia yanngamia
Nahodha yako meli imepinda,mbali kupindukia
Roho za abiria waziponda,hiyo damu yakulilia
Dereva kawa konda,usukani mbali katupilia
Nahodha paza sauti, asikari wako watuuwa
Baba wanao usituuwe,tuache tuione asubuhi

Moyo umejawa na uchungu,damu yabubujika
Kiongozi aso na uchungu,watu awapukutisha
Macho yake yana ukungu,mbele tunaangamia
Kichaa kashika rungu,masikini mtaangamia
Askari wako nyoka, waisikza sauti yako chatu
Baba legeza kutuua, naomba tuachie uhai wetu

Baba kwanini watuua,sis binadamu kama we
Wanao tunakulilia,baba huruma yako tuonee
Usitupige risasi,sisi pia viumbe wa Mola
Baba weka moyo wa uzazi,twahitji yako malezi
masikini nchi angu,damu iso hatia inamwagwa
Baba mioyo yetu yanyama, inaumia pia usituue

Taratibu naona giza,wingu kuu limeghubika
Nuru nayo yaangaza,vumbi nalo linatimka
Vita wanatangaza,walo wengi hawajaamka
Vifo vyashangaza,mtetemo chini yasikika
Asikari wasambaza,damu nayo yatiririka
Baba kila kitu akataza,wanae anawaua
Baba mauti inatuumiza,kumbuka nawe utakufa.

Kademokrasia kameondoka,kademoghasia kamerejea
Kademo amani kamefukiwa,kademo piga risasi kametawala
..
Katika nchi ya Tanzagiza pekee risasi inapigwa juu angani....
Inauwa mtu kwenye gari..
Na sio kwenye ndege au helkopta...
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
Jr.elly
641c0fbf06dabf6c0d8dabe49b9de7d5.jpg
 
Nimesoma sentesi ya mwanzo tuu nilivyojua Nia nimeacha kusoma[emoji24][emoji24]
 
Mkuu, nimejikuta natoka machozi, kisha hawa Mbwa watakuja wajisifie! Hivi unapata wapi raha ya kushangilia Ushindi wa Damu?? Mungu niepushie Hii hasira
 
Hivi ndivyo "mshindi" atakavyosherehekea ushindi wa kumuunga mkono huyo mtu wake kwa vifo vya watu wawili. Bila maamuzi yake ya kijinga na kiwendawazimu haya yasingetokea! Inatia hasira sana kusema kweli! Polisi wa nchi hii nao ni bora ukutane na Simba mwenye njaa kuliko wao wakiwa wameshika bunduki zao na virungu. Hawana akili nyingine zaidi ya kupiga na kuua! Wameua Mwangosi Iringa, wakapandishwa vyeo. Mikono yao inanuka damu!
 
Back
Top Bottom