Kwanini msemaji wa Club ya Simba anatangaza bidhaa za pinzani kibiashara? Inawezekana vipi?

Nyumba ndogo ruksa.

On a serious note, tusisahau kuwa Mbumbumbu FC na Azam wana undugu fulani japo si wazi sana (ni kama ule wa Vyura FC na Singida).
 
Nyumba ndogo ruksa.

On a serious note, tusisahau kuwa Mbumbumbu FC na Azam wana undugu fulani japo si wazi sana (ni kama ule wa Vyura FC na Singida).
Na kwa wafuatiliaji wa soka la TZ, undugu huu unafahamika kabisa manake nasikia Mzee Bakhresa miaka ya nyuma alishawahi kuwa Mweka Hazina wa Msimbazi!
 
Nyumba ndogo ruksa.

On a serious note, tusisahau kuwa Mbumbumbu FC na Azam wana undugu fulani japo si wazi sana (ni kama ule wa Vyura FC na Singida).
Na ukumbuke pia Bakhresa mpaka anaenda kuanzisha Azam FC ni baada ya kutoka Simba na kuona hela zinaliwa tu haoni cha maana akaenda kuanza from scratch na kaisimamisha imefikia hapo. Ni kama tu tapeli wa 20 biruwon alivyoenda kuanzisha African Lyon( kwa kununua timu) ila ikamshinda naona karudi.

Simba,coastal union na Azam FC ni kweli kuna undugu wa kimya kimya
 
Acheni wivu, wewe unajua mkataba wake na Simba ukoje? Umeambiwa asitangaze bidhaa zozote za Azam? Mnapenda Sana kuingilia maisha binafsi ya watu. Yeye anatengeneza pesa nyie mnakaa kupiga majungu.... Wewe kazi yako Kama shabiki no kushangilia na kuzomea Basi, Mambo binafsi ya watu achana nayo hayakuhusu.. Kwani akifukuzwa hapo Simba Kama unavoombea iwe, wewe utapewa hiyo nafasi yake?
 
Kwahiyo tumkute mwanaccm anapost Mambo ya Chadema kwenye account Yake kisa ni account binafsi.

Unajua terms and conditions za mkataba kuhusu conflict of interest ?

Ni hujuma Sana tena iko wazi, ataanzaje kutangaza bidhaa za jirani wakati boss wake nae anabidhaa kama izzo, bidhaa za boss wake zisipo toka atawalipa Nini.?

Hata ukiwa mfanyakazi wa Pepsi , hafu ukapiga picha unakunywa kokakola unafukuzwa kazi, au tbl hafu ukapiga picha na Serengeti lite

Kwani Simba SC ni kiwanda cha kuzalisha bidhaa kama juisi nk?
 
Umeandika kwa hisia sana mzee vipi kwani
 

Mkuu unasemaje kuhusu Azam Sports Federation Cup?
Hakuna mgogoro wa kimaslahi hapo?
Kwamba SSC inakwenda kushiriki maahindano yanayoitangaza Azam “mshindani” wake?

Kuna timu zina dhaminiwa na Nike halafu wachezaji wake wanadhaminiwa na Puma, Adidas nk, unalizungumziaje hili?

Nifafanulie tu na mimi ni jue mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…