Kwanini mtoto anampiga mama yake (3years)

Mkuu, jaribu huyo mtoto anyimwe vitu vingine akileta za ovyo kwa mama. Akimkasirisha mama, naye mama hamnunulii vitam tam vyake hadi awe mtulivu, pia saa ingine mama achukue fito zile, aki jam, kamata yeye tandika za miguu, sio na hasira lakini usije mkajitia hasara bure hapo!
 
Hio tabia ya huyo mtoto haitabadilika kama wadau wanavyoshauri ndo kwanza atakua kiburi zaidi. Samaki mkunje angali mbichi

Kanakula tu fimbo au kifinyo kawe na adabu. ka hivyo katakuaibisha mbele za wageni
Kweli, mama anafaa a deal nako solo, bila hivyo kataleta mhadhara mbele ya umati, hapo maji hayazoleki tena, keshayamwaga peupe. 😂
 
First things first,
Who let the two of you reproduce?! 😡
 
Kwa mujibu wa utafiti wangu ninaoendela kuufanya nimegundua kuwa kuna tabia watoto wanakuwa nazo ambazo zinatokana na vile mtoto anavyolelewa tokea anazaliwa.

Wazazi wanajisahau kuwa mtoto akianza kuongea na kutembea hapo anakuwa sio amejifunza kuongea tu,sio amejifunza kuongea tu bali kajifunza pia namna gani ahandle pale anapoudhiwa na kugombwa jjuu ya jambo fulani.

Wazazi wengi wanadhani mtoto akijua kuongea na kutembea ati amejifunza mambo hayo tu.

No,kumbuka wakati anajjifunza kuonngea huku amezaliwa na mdomo kumbuka pia amezaliwa na macho yake ushawahi kujiuliza hayo macho tokea anazaliwa mpska anafikia kuongea na kutembea hayo macho kwake yana kazi gani ?

Kazi ya macho sio kujifunza kwa kusikia bali kazi ya macho ni kujifunza kwa kuona.

Kuna matukio mtoto anayaona na kuyasikia hivyo anajua kwamba tukio hili likitokea nifanye vipi baada ya kuwa ashaliona.

Jambo la ajabu zaidi ni kuwa namna unavyoishi na mtoto ndivyo naye atakua hivyo hivyo.

Kuna mtoto wa jirani yangu hanakaribia miaka miwili anatembea,anaongea vizuri tu huwa ni mkorofi korofi,siku moja nimekaa akanichapa na kitu ikaniuma nikamuangalia tu kwa hasira kisha nikaondoka pale nikamuhama,tokea siku hiyo kila nikimuona nampotezea mpaka akajua kuwa jamaa hataki ujinga sasa hivi kaacha ujinga wake wa kunipiga bila kutumia nguvu.

Watoto ni viumbe tunahitaji uweledi kuishi nao,usimuache mtoto atazame mambo ambayo wewe hupendi aje kuwa nayo baadae ni hatari.

Movie za kupigana,movie za mapenzi ni mbaya kwa mtoto kwa sababu mtoto ni mtu ambaye anatafuta matukio ili ayaishi hivyo liwe zuri ama baya yeye analidaka tu mradi baadae atakuja kulitumia katika kuishi kwake.

Leo mtoto wa mwaka miaka miwili hajui hili zuri au baya,hivyo ukimuona na baya mkemee kabla hajakuwa.
 
Mlete Kanisani, abandikwe mikono na watumishi wa Mungu aliye hai. Hiyo ni roho chafu itamtoka tu.




YESU NI MWOKOZI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…