Kwanini mtoto hulia baada ya kuzaliwa?

Kwanini mtoto hulia baada ya kuzaliwa?

hilo la kulia naona si kubwa, kubwa ni nani kinamfundisha mtoto aliyezaliwa dakika chache tu kwamba akipewa kitu mdomoni lazima avute ni nini? (anyonye); sababu hajui chochote kile wala hajui kwamba kashazaliwa tayari duniani.
Hapo sio sayansi tena ni mambo ya Mungu
 
Hapo sio sayansi tena ni mambo ya Mungu
kuna watu huwa hawaamini Mungu, wao wanaamini sayansi - sasa waje watuambie ni kichocheo gani kinachofanya mtoto ajue sasa hupo duniani lazima aanze kuvuta nyonyo ya mama ili maziwa yatoke na asipofanya hivyo atapoteza maisha, kumbuka by the time mtoto anazaliwa haoni kitu.
 
Analia kwasababu kama ni wa kiume anajua siku si nyingi atakula kwa jasho lake kama alivyoambiwa na kama mwanamke atazaa kwa uchungu...
Sema siku hizi kuna watu wanakwepa hizi adhabu bwana kuna wagba hawazai na kuna wanaume wanalelewa
 
Hivi hata ww ukifungiwa kwenye Kabati miezi 9, ukijatolewa hutalia unasubiri nn?
 
Mtoto anapo pata mauvumivu kwa mara ya kwanza lazima alie tu hata kama wewe umepata maumivu mara ya kwanza lazima uchozi utoke na sio kucheka
 
mtoa hoja anasema kwa nini mtoto alie na asitumi njia nyingine? kwa mfano anaweza kucheka na huko kunaweza pia kusababisha mapafu yake yakapanuka siyo.
Hivi mtoto ukimfinya unategemea acheke kwa maumivu aliyoyapata?
Hiyo sudden change of environment husababisha maumivu makali. Kwa hiyo kama yuko normal lazima atalia and this is how mother nature (also known as God) had set things. Atalia kwa baridi hadi atakapokuwa amefunikwa kwa manguo/ blanket na kupatiwa joto kwa kumlaza in contact na mwili wa mama yake (kangaroo style).

Halafu mtoto mchanga hana reflex ya kucheka. Akiwa na furaha hacheki bali huchapa usingizi. Akiwa na shida yo yote (eg ana njaa, amejikojolea, anaumwa, anasikia baridi nk) atalia. Mambo ya kucheka yanaanza baada ya kufikisha umri wa miezi kadhaa.
 
hilo la kulia naona si kubwa, kubwa ni nani kinamfundisha mtoto aliyezaliwa dakika chache tu kwamba akipewa kitu mdomoni lazima avute ni nini? (anyonye); sababu hajui chochote kile wala hajui kwamba kashazaliwa tayari duniani.
Mkuu acha tu...M/ Mungu fundi
 
Kuna rafiki alinambia kun mambo 5 ambayo humfanya Mtoto kulia...
Yeye alinijuza mawili tu

1: Kufungua mapafu ili Kupitisha hewa

2: Huona mabaya yafanywayo duniani.

Je, sababu zingine zipi?
Sasa ataeezaje kulia kama bado hajazaliwa....[emoji15] [emoji15] [emoji15]
 
Kuna portion ya moyo inahitajika kufunguka wakati mtoto ametoka kwenye tumbo la uzazi hivyo inahitajika oxygen wakati huo ili ile sehemu ifunguke ndio maana analia ili kuruhusu oxygen nyingi ipite kwenye mapafu na ndio maana huwa unaona asipolia kuna vitu wanafanya ili aweze kulia kifupi hivyo.
Mkuu naona unatema shule.. kuna portion ya moyo inahitaji kufanyeje??.. [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Mkuu naona unatema shule.. kuna portion ya moyo inahitaji kufanyeje??.. [emoji1] [emoji1] [emoji1]
Vitu kama hivi huwezi kuelezea kama ulivyofunzwa inabidi ueleze ulivyoelewa sikupata mwalimu mzuri wa physiology mkuu.
 
Sayansi, ushirikina, matango pori vyote vipo hapa teh....
 
Mabadiliko ya ghafla ya mazingira/ hali ya hewa kutoka ya joto la nyuzi 37 degrees centigrade ndani ya tumbo la mama yake hadi hali ya baridi na upepo mkali wa dunia yetu, humfanya alie sana. Kitendo cha kulia husababisha avute hewa ya dunia kwa mara ya kwanza na kuyapanua mapafu yake na kuanzisha automatic breathing process.

NB: Akiwa ndani ya tumbo la mama mtoto huwa hali chakula kwa mdomo wala huwa hapumui kwa pua. Mahitaji yake ya chakula na hewa huyapata kwa mama yake kupitia kitovu chake hadi kwenye kondo la mama yake. Hivyo mapafu huwa yame collapse. Akizaliwa akashindwa kulia basi atashindwa kupumua na baada ya dakika chake lazima ataaga dunia.
Halafu niliwahi kusikia kuna uhusiano wa karibu kabisa kati ya kuwahi/kuchelewa kulia na akili yaani mtoto akiwahi kulia mara tu anapozaliwa atakuwa na akili sana na akichelewa sana kuna uwezekano akawa taahira. Je kuna ukweli katika hili?
 
Anakuwa amekuja mazingira tofauti ambayo humfanya imechukue muda kuyazoea.Lakin pia hurahisisha kujua uhai wa mtoto
 
kuna watu huwa hawaamini Mungu, wao wanaamini sayansi - sasa waje watuambie ni kichocheo gani kinachofanya mtoto ajue sasa hupo duniani lazima aanze kuvuta nyonyo ya mama ili maziwa yatoke na asipofanya hivyo atapoteza maisha, kumbuka by the time mtoto anazaliwa haoni kitu.
Nadhani Ni survival instinct tu.
Hata mtoto wa mbuzi au mbwa atakimbilia tu nyonyo akizaliwa.
 
Hivi mtoto ukimfinya unategemea acheke kwa maumivu aliyoyapata?
Hiyo sudden change of environment husababisha maumivu makali. Kwa hiyo kama yuko normal lazima atalia and this is how mother nature (also known as God) had set things. Atalia kwa baridi hadi atakapokuwa amefunikwa kwa manguo/ blanket na kupatiwa joto kwa kumlaza in contact na mwili wa mama yake (kangaroo style).

Halafu mtoto mchanga hana reflex ya kucheka. Akiwa na furaha hacheki bali huchapa usingizi. Akiwa na shida yo yote (eg ana njaa, amejikojolea, anaumwa, anasikia baridi nk) atalia. Mambo ya kucheka yanaanza baada ya kufikisha umri wa miezi kadhaa.
Well said Dr Akili
 
Back
Top Bottom