Kwanini Mzee Kilomoni anaishikiria hati ya Simba je ndiye mmiliki au anaidai Simba?

Asante kwa kunipanikia
Swali lako ni la msingi sana kwa mtazamo wangu, namna alivyoipata ndio kunampa nguvu ya kuishikilia kana kwamba ndiye mmiliki wa simba au mmiliki wa lile jengo. Tuanzie hapo.
 
KILOMONI, KILOMOMI UNAITAKIA NINI SIMBA WEWE KILOMONI, HUONI MAMBO YALIVYO MUKIDE, in Maulidi Kitenge's voice
 
Si uhakika sana lakini baada ya mzee Kilomoni kuchaguliwa kuwa mdhamini wa mali za Simba pamoja na wenzake wawili ndipo akautumia mwanya huo kung'ang'ania hati za jengo la Simba. Kuna wakati viongozi walijaribu kumuondoa kwenye udhamini lakini ilishindikana kwa sababu walikosea utaratibu. Kiutaratibu hizo hati ni mali ya Simba na zinatakiwa zihifadhiwe ofisini Msimbazi kwenye safe (kasiki) na sio nyumbani kwa mtu.

Lakini nafasi ya kumuondoa bado ipo cha msingi wanachama wanatakiwa wafuate utaratibu kama katiba ya Simba inavyotaka. Akishaondolewa kuwa mdhamini kama katiba inavyotaka kitakachofuata ni kusajili muhtasari wa maamuzi ya wanachama RITA na ofisi nyingine za serikali hapo itatakiwa kisheria Mzee Kilomoni akabidhi hati za jengo na mali zote za Simba alizonazo mikononi mwake kwa wadhamini wapya akigoma sheria itachukua mkondo wake.

Ukiangalia hili suala la Kilomoni linakuzwa tu bila sababu kwa sababu suluhisho lake ni viongozi kufuata taratibu za kisheria kupitia katiba ya Simba basi.Itachukua muda kidogo lakini kutakuwa na suluhisho la kudumu. Lakini kinachoonekana ndani ya viongozi wenyewe kuna kuzunguukana kama alivyosema Mo. Inaonekana kuna viongozi waligombea wakitegemea Simba itakuwa ya upigaji/ulaji kama miaka iliyopita lakini sasa walipogundua kuwa mirija imekatwa wakabaki mchana kuwa na Mo ikifika usiku wapo na Kilomoni lengo lao timu iende kwenye bakuli kama Yanga kwani bakuli halina usimamizi kuwa zimeingia ngapi, zimetumika ngapi na zimetumikaje tumikaje.

Nafikiri ni wakati muafaka kwa viongozi badala ya kulia lia waitishe mkutano waangalie viongozi gani wanaikwamisha Simba kuendelea kutoka hapa ilipofika. Utaratibu ufuatwe viongozi wasaliti waondolewe wachaguliwe viongozi wengine na baraza la wadhamini jipya basi mjadala ufungwe.
 
Kweli mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…