Kwanini ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki sisi ni "DR. NO"?

Kwanini ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki sisi ni "DR. NO"?

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
1._ Ukweli ni vyema tukautamka hadharani bila ya kujiumauma.


Ndani ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki ni ukweli usiofichika ya kuwa tumechokwa kwa sababu tumekuwa tukipinga kila hatua ambayo ndiyo msingi na sababu ya kuanzishwa Jumuiya hiyo.

2. Sababu ya kuanzishwa Jumuiya mbona tumeiweka kando?

EAC ilianzishwa ili kuziunganisha nchi za ukanda wa mashariki mwa afrika ili ziwe na sauti kubwa katika uendeshaji wa dunia kwa msingi mmoja tu "umoja ni nguvu" lakini sisi na werevu wetu kama upo wa tambo za tuna ardhi na na maliasili lukuki na kwamba kujiunga na wenzetu tutafukarika huku tukujua hatuna nyenzo za kunufaika na yale yote ambayo Muumba katupatia.

Ukizifanyia kazi kwa undani ngonjera zetu utabaini kuna upotoshaji wa khali halisi na huku wageni wanajiporea ardhi na maliasili nyinginezo bila ya shari au zengwe lolote lile ili mradi wenye nafasi serikalini wapoozwe kwa ulaji wa bei poa.................
Ama kwa uhakika, wajinga ndiyo tuliwao!


3. Kama ardhi tunayo mbona migogoro ya ardhi imetuchachamalia?

Wanandugu ni vyema tukawa wazi yawaje kila kukicha tunakatana viwiliwili kisa ni mapambano ya umiliki ardhi kati ya wafugaji na wakulima ukiachilia mbali uvamizi wa maeneo ya wazi, miliki za barabara na hifadhi za mbuga zetu ambazo kwa pamoja zinathibitisha ardhi siyo nyingi kama tunavyojigamba na haipaswi kuwa kikwazo cha kulisukuma gurudumu ndani ya EAC.........................

4. Kama Jumuiya hatuko tayari nayo mbona tunawakwaza wenzetu ambao wako tayari?

Muungwana anapoona hana ubavu na jambo fulani huwaruhusu washiriki wenzie waendelee siyo kujitetea ya kuwa anasubiri........"kulimwa talaka."

Huu ni utetezi wenye lengo la kuonyesha hatupendwi kumbe hatupendeki kutokana na misimamo yetu ya kukwamisha utekelezaji wa malengo ya msingi ya kuanzishwa kwa EAC............................

5. Mfumo wa Kupiga kura ndani ya EAC ni lazima ugeuzwe kulinda masilahi ya wengi wape!

"Wengi wape" ndiyo njia pekee ya kuinusuru EAC na mfumo uliopo wa kila nchi inaweza kupiga "kura ya veto" itasababisha EAC kufa kama kile kifo chake cha mbwakoko 1977.........................kama nchi yetu yenye utapeli lukuki haitaki suala la ardhi na maliasili kuwa sehemu ya EAC basi turuhusiwe kuwa mwanachama asiyelazimishwa kushiriki katika maamuzi fulani fulani lakini nasi tusiwe kikwazo cha kuwaruhusu wenzetu kuendelea kufanikisha maamuzi ya EAC...........That is what I call a fair deal to all!

 
Kwa maoni yangu binafsi watanzania hawakujiandaa na globalization. Hawana mfumo mzuri wa elimu kwa soko la kazi la kimataifa. Hivyo wanaogopa ushindani. Hawakuwa na sheria nzuri za haki ya kumiliki ardhi. Hivyo NO nyingi ni za kujilinda hili wasije kujiona wanyonge ndani ya nchi yao wenyewe.
 
Rutashubanyuma,

..kwa uelewa wangu tumekataa mambo matatu: 1.Ardhi 2.Federation 3. mkataba wa ulinzi.

..Kenya na Uganda nao wanaonekana kuogopa suala la monetary union. kwa msingi anayekwamisha jumuiya siyo Tanzania peke yake.

..kuhusu ardhi, ni kweli kwamba migogoro baina yetu wa-Tz imekuwa mingi. je ni tukikaribisha majirani zetu migogoro hiyo itapungua? kwa maneno mengine, je dawa ya migogoro ya ardhi Tanzania ni kukaribisha wanyarwanda,wakenya, waganda,na warundi??

..pia sheria ya uwekezaji ya Tanzania inaruhusu watu wa nje kukodisha ardhi kwa muda mrefu mpaka miaka 99. je, kwanini majirani zetu hawataki kufuata sheria hiyo kama wanavyofanya wawekezaji wengine? je, majirani zetu wanaogopa ushindani??

..zaidi, hivi nchi kama Rwanda na Burundi zinapotushauri wa-Tanzania tugawane nao ardhi, does that really make sense to anyone?

..all member states are guilty as charged linapokuja suala la kuachana na msingi wa "umoja ni nguvu." badala kujenga umoja na ushirikiano nchi wanachama zimejielekeza zaidi katika kushindana baina yao wenyewe.

..Binafsi nadhani tuwe na umoja wa kibiashara kama ule wa NAFTA. Mambo ya kisiasa yasiingizwe kabisa katika jumuiya.


cc Zakumi, Kubwajinga, Mdondoaji, Nguruvi3, Ngongo
 
Last edited by a moderator:
Ruta
Nadhani umemsoma vema jokaKuu.

Jiulize katika mambo yote wenzetu wadhani msingi wa EA ni ardhi.
Endapo ni msingi tujiulize je kutakuwa na fair deal? Angalia population density


Kwanini wasikubaliane na mpango wa kukodi kwa miaka 99 kama wengine.

Migogoro ya ardhi iliyopo ni kiashirio kuwa hilo ni tatizo, sasa sijui ukifungulia milango ndio utakuwa ume solve!!

Ruta nadhani unaongozwa na hisia zaidi kuliko ukweli. Kama ardhi si tatizo kwanini Kenya na Uganda walikaribia kuzipiga kwasababu ya KM 1 ya Migingo! kwanini?

Tanzania haijakataa wenye nia kuendelea, lakini yafanyike kufuata utaratibu wa EAC.
Tanzania ilishatoa msimamo kuwa kwa yale yanayo onekana yana tatizo wenzetu waendelee tukiwa tayari tutawaunga mkono. Hilo lifanyike hadharani na si kwa siri. Ndipo malalamiko yalipo na si kwanini wanafanya.

Ruta nikuulize

Hatujafikia hatua ya free capital na human movement na monetary union tunawezaje kwenda kwenye shirikisho kabla ya msingi kujengwa?


Unapojenga block mataifa yanaanglia stability yake.

Kwasasa kuna wasi wasi wa stability EA na huo wa coalition of willing kwa vile kumeonekana kutoaminiana.


Kama mamamuzi yangekuwa yamefanywa kwa taratibu za EA wala lisingeonekana tatizo, kwasasa investors wana machale kwasababu ya ‘kuzungukana'.
Wao wataliona kama instability ya block.

Je, hilo litaisaidia EAC au hiyo coalition of willing?


Kuhusu VETO lazima uangalie muundo wa EAC. Hapa unamuunga mkono M7 aliyelazimisha uiningiaji wa Rwanda na Burundi kuweka wingi.


Kumbuka haya ni mataifa si vikao vya madiwani na hivyo lazima kuwepo na utaratibu na si vurugu za wingi wa kura. Inatakiwa consensus na si kunyanyua vidole kama unavyoshauri

Mistrust kubwa sana ni pale wenzetu wanapokataa kusema tatizo halisi wanatafuta sababu za kipuuzi. Wanaficha ukweli na kusema TZ inaogopa ushaindani wa ajira. Kama inaogopa ushindani kwanini isiogope Kenya kuwa mwekezaji namba 2 nchini? Hata hivyo watueleze ni taifa gani lisilolinda masilahi yake!
Mbona Kenya wanasita single visa

Nini kinatokea kwa NAFTA na malalamiko kwa Marekani.

 
Rutashubanyuma,

..kwa uelewa wangu tumekataa mambo matatu: 1.Ardhi 2.Federation 3. mkataba wa ulinzi.

..Kenya na Uganda nao wanaonekana kuogopa suala la monetary union. kwa msingi anayekwamisha jumuiya siyo Tanzania peke yake.

..kuhusu ardhi, ni kweli kwamba migogoro baina yetu wa-Tz imekuwa mingi. je ni tukikaribisha majirani zetu migogoro hiyo itapungua? kwa maneno mengine, je dawa ya migogoro ya ardhi Tanzania ni kukaribisha wanyarwanda,wakenya, waganda,na warundi??

..pia sheria ya uwekezaji ya Tanzania inaruhusu watu wa nje kukodisha ardhi kwa muda mrefu mpaka miaka 99. je, kwanini majirani zetu hawataki kufuata sheria hiyo kama wanavyofanya wawekezaji wengine? je, majirani zetu wanaogopa ushindani??

..zaidi, hivi nchi kama Rwanda na Burundi zinapotushauri wa-Tanzania tugawane nao ardhi, does that really make sense to anyone?

..all member states are guilty as charged linapokuja suala la kuachana na msingi wa "umoja ni nguvu." badala kujenga umoja na ushirikiano nchi wanachama zimejielekeza zaidi katika kushindana baina yao wenyewe.

..Binafsi nadhani tuwe na umoja wa kibiashara kama ule wa NAFTA. Mambo ya kisiasa yasiingizwe kabisa katika jumuiya.

Ili kuinusuru Jumuiya inabidi wengi wape itumike na yule asiyetaka jambo fulani awe na uhuru wa kutoshiriki lile asilolitaka badala ya utaratibu wa sasa wa ya kuwa tunawazuia wale ambao wako tayari kupiga hatua fulani kwa madai ya matumizi ya veto ya nchi moja.............
 
Ruta
Nadhani umemsoma vema jokaKuu.

Jiulize katika mambo yote wenzetu wadhani msingi wa EA ni ardhi.
Endapo ni msingi tujiulize je kutakuwa na fair deal? Angalia population density


Kwanini wasikubaliane na mpango wa kukodi kwa miaka 99 kama wengine.

Migogoro ya ardhi iliyopo ni kiashirio kuwa hilo ni tatizo, sasa sijui ukifungulia milango ndio utakuwa ume solve!!

Ruta nadhani unaongozwa na hisia zaidi kuliko ukweli. Kama ardhi si tatizo kwanini Kenya na Uganda walikaribia kuzipiga kwasababu ya KM 1 ya Migingo! kwanini?

Tanzania haijakataa wenye nia kuendelea, lakini yafanyike kufuata utaratibu wa EAC.
Tanzania ilishatoa msimamo kuwa kwa yale yanayo onekana yana tatizo wenzetu waendelee tukiwa tayari tutawaunga mkono. Hilo lifanyike hadharani na si kwa siri. Ndipo malalamiko yalipo na si kwanini wanafanya.

Ruta nikuulize

Hatujafikia hatua ya free capital na human movement na monetary union tunawezaje kwenda kwenye shirikisho kabla ya msingi kujengwa?


Unapojenga block mataifa yanaanglia stability yake.

Kwasasa kuna wasi wasi wa stability EA na huo wa coalition of willing kwa vile kumeonekana kutoaminiana.


Kama mamamuzi yangekuwa yamefanywa kwa taratibu za EA wala lisingeonekana tatizo, kwasasa investors wana machale kwasababu ya ‘kuzungukana'.
Wao wataliona kama instability ya block.

Je, hilo litaisaidia EAC au hiyo coalition of willing?


Kuhusu VETO lazima uangalie muundo wa EAC. Hapa unamuunga mkono M7 aliyelazimisha uiningiaji wa Rwanda na Burundi kuweka wingi.


Kumbuka haya ni mataifa si vikao vya madiwani na hivyo lazima kuwepo na utaratibu na si vurugu za wingi wa kura. Inatakiwa consensus na si kunyanyua vidole kama unavyoshauri

Mistrust kubwa sana ni pale wenzetu wanapokataa kusema tatizo halisi wanatafuta sababu za kipuuzi. Wanaficha ukweli na kusema TZ inaogopa ushaindani wa ajira. Kama inaogopa ushindani kwanini isiogope Kenya kuwa mwekezaji namba 2 nchini? Hata hivyo watueleze ni taifa gani lisilolinda masilahi yake!
Mbona Kenya wanasita single visa

Nini kinatokea kwa NAFTA na malalamiko kwa Marekani.


Tatizo ni kuwa mkataba wa EAC un dosari nyingi ambazo zinatakiwa kurekebishwa huwezi nchi moja kuzikwamisha nchi nyingine ambazo wako tayari kwenda mbelekwa mbele. Sisi kama hatuko tayari ni sawa tu lakini wanaona wako tayari kutimiza malengo ya Jumuiya waache waendelee.

Suala la ardhi kwetu linakuzwa mno. ukweli ni kuwa hatuna ardhi ya kututosheleza hata sisi. Na ndiyo maana vurugu za ardhi kwetu hivi sasa zimechachamaa.

Wengi wape usipowapa watajichukulia. Huwezi ukaungana na wenzio ukategemea isiwe "a give and take" utajidanganya. Dunia ya sasa hivi kubwa ni information age na wala siyo ardhi. Ardhi nchi masikini kama yetu itaendelea kuhodhiwa na wageni kutoka nje ya bara hiili kwwa visingizio ni wawekezaji so it is not really a big issue in integration of EAC.
 
Ruta
Nadhani umemsoma vema jokaKuu.

Jiulize katika mambo yote wenzetu wadhani msingi wa EA ni ardhi.
Endapo ni msingi tujiulize je kutakuwa na fair deal? Angalia population density


Kwanini wasikubaliane na mpango wa kukodi kwa miaka 99 kama wengine.

Migogoro ya ardhi iliyopo ni kiashirio kuwa hilo ni tatizo, sasa sijui ukifungulia milango ndio utakuwa ume solve!!

Ruta nadhani unaongozwa na hisia zaidi kuliko ukweli. Kama ardhi si tatizo kwanini Kenya na Uganda walikaribia kuzipiga kwasababu ya KM 1 ya Migingo! kwanini?

Tanzania haijakataa wenye nia kuendelea, lakini yafanyike kufuata utaratibu wa EAC.
Tanzania ilishatoa msimamo kuwa kwa yale yanayo onekana yana tatizo wenzetu waendelee tukiwa tayari tutawaunga mkono. Hilo lifanyike hadharani na si kwa siri. Ndipo malalamiko yalipo na si kwanini wanafanya.

Ruta nikuulize

Hatujafikia hatua ya free capital na human movement na monetary union tunawezaje kwenda kwenye shirikisho kabla ya msingi kujengwa?


Unapojenga block mataifa yanaanglia stability yake.

Kwasasa kuna wasi wasi wa stability EA na huo wa coalition of willing kwa vile kumeonekana kutoaminiana.


Kama mamamuzi yangekuwa yamefanywa kwa taratibu za EA wala lisingeonekana tatizo, kwasasa investors wana machale kwasababu ya ‘kuzungukana’.
Wao wataliona kama instability ya block.

Je, hilo litaisaidia EAC au hiyo coalition of willing?


Kuhusu VETO lazima uangalie muundo wa EAC. Hapa unamuunga mkono M7 aliyelazimisha uiningiaji wa Rwanda na Burundi kuweka wingi.


Kumbuka haya ni mataifa si vikao vya madiwani na hivyo lazima kuwepo na utaratibu na si vurugu za wingi wa kura. Inatakiwa consensus na si kunyanyua vidole kama unavyoshauri

Mistrust kubwa sana ni pale wenzetu wanapokataa kusema tatizo halisi wanatafuta sababu za kipuuzi. Wanaficha ukweli na kusema TZ inaogopa ushaindani wa ajira. Kama inaogopa ushindani kwanini isiogope Kenya kuwa mwekezaji namba 2 nchini? Hata hivyo watueleze ni taifa gani lisilolinda masilahi yake!
Mbona Kenya wanasita single visa

Nini kinatokea kwa NAFTA na malalamiko kwa Marekani.


Tatizo ni kuwa mkataba wa EAC un dosari nyingi ambazo zinatakiwa kurekebishwa huwezi nchi moja kuzikwamisha nchi nyingine ambazo wako tayari kwenda mbelekwa mbele. Sisi kama hatuko tayari ni sawa tu lakini wanaona wako tayari kutimiza malengo ya Jumuiya waache waendelee.

Suala la ardhi kwetu linakuzwa mno. ukweli ni kuwa hatuna ardhi ya kututosheleza hata sisi. Na ndiyo maana vurugu za ardhi kwetu hivi sasa zimechachamaa.

Wengi wape usipowapa watajichukulia. Huwezi ukaungana na wenzio ukategemea isiwe "a give and take" utajidanganya. Dunia ya sasa hivi kubwa ni information age na wala siyo ardhi. Ardhi nchi masikini kama yetu itaendelea kuhodhiwa na wageni kutoka nje ya bara hiili kwwa visingizio ni wawekezaji so it is not really a big issue in integration of EAC.
 
Rutashubanyuma,

..kama ARDHI ni chache huku Tanzania kama unavyosema, basi serikali imefanya busara kutokuruhusu ardhi yetu kuwa ya jumuiya.

..mimi nadhani hata kwenye AJIRA tungechukua msimamo huo huo. tuna tatizo kubwa sana la ukosefu wa ajira kwa vijana wetu, kwa msingi huo tusiruhusu wageni unless ni wale wenye utaalamu wa hali ya juu unaohitajika.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo ni kuwa mkataba wa EAC un dosari nyingi ambazo zinatakiwa kurekebishwa huwezi nchi moja kuzikwamisha nchi nyingine ambazo wako tayari kwenda mbelekwa mbele. Sisi kama hatuko tayari ni sawa tu lakini wanaona wako tayari kutimiza malengo ya Jumuiya waache waendelee.

Suala la ardhi kwetu linakuzwa mno. ukweli ni kuwa hatuna ardhi ya kututosheleza hata sisi. Na ndiyo maana vurugu za ardhi kwetu hivi sasa zimechachamaa.

Wengi wape usipowapa watajichukulia. Huwezi ukaungana na wenzio ukategemea isiwe "a give and take" utajidanganya. Dunia ya sasa hivi kubwa ni information age na wala siyo ardhi. Ardhi nchi masikini kama yetu itaendelea kuhodhiwa na wageni kutoka nje ya bara hiili kwwa visingizio ni wawekezaji so it is not really a big issue in integration of EAC.
Hapa unajaribu kuficha ukweli ndugu yangu.
Mkataba una masuala yanayohusu VETO. Hili jambo umeliongelea tofauti kabisa na mkataba unavyosema.

Lazima uelewe kuwa mkataba uliandikwa na nchi tatu na zilikubaliana hivyo. Maana ya VETO ililenga nchi tatu ili kuondoa kile kinachoitwa wengi kwasababu hakukuwa na wengi by then.

Pili, kuna kifungu kinachoruhusu ushirikiano wa mataifa 'variable geometry'. Sisi na Kenya tuliamua kuanza kujenga miundo mbinu ya barabara kwa kupitia EAC kama nchi mbili. Barabara ya Namanga-Nairobi

Tanzania, Rwanda na Burundi zilikuwa na mpango wa kujenga reli ya pamoja. Hayo yote yalikuwa ndani ya EAC bila kuzuiwa na nchi nyingine.

Kenya na Rwanda wana makubaliano ya ajira miongoni mwao na EAC inajua hivyo.

Tanzania imetoa msimamo kuhusu suala la ardhi na kusema kuwa wale walio tayari kufanya ardhi kuwa ya pamoja waendelee. Kwabahati mbaya hawakufanya kwasababu hilo halikuwa lengo lao.

Mkutano wa mwisho Tanzania ikasema haipo tayari kutumia ID bali passport, lakini wale wanaoweza kuendelea waendelee.

Ukiangalia mambo yote hakuna mahali ambapo Tanzania imewakwaza kama unavyodai.
Madai yako ni ya kutunga na kuyakuza na nina hofu sana kama kweli una nia njema.
Hakuna mahali ambapo Tanzania inaweza kutumia VETO kama yenyewe ina mipango niliyoeleza.

Kuhusu suala la ardhi, hilo ndilo lilianzisha mgogoro kwa taarifa yako. Hata kabla ya kujadili soko la pamoja, mitaji na uhamiaji ikiwa ni pamoja na ushuru wa forodha suala la ardhi ndilo lilikuwa la kwanza.

Kama utakumbuka Kenya ilikuwa inamtumia Kamau Warigi kuhusu suala hili wakisema Tanzania inakwamisha EAC kwa masuala ya ardhi.

Sababu wanazozitoa wao ni kuhusu ajira ambazo si kweli.
Watanzania wengi wanafanya kazi katika nchi za EAC.

Wenzetu wanasema watu waje na ID zao na kupewa ajira. Sasa kama Tanzania ilikataa ID kwanini ikubali ID za ajira. Na pili hakuna anayenyimwa ajira kwa kuomba.

Sababu wanzozitoa wao ambazo unaamini ni hafifu kuliko suala la ardhi. S
uala la ardhi hawawezi kuliongelea kwasababu nyingi.

Angalia population density ya Rwanda na Burundi halafu uniambie.
Kenya 10% ya watu inamiliki 90% ya ardhi. 90% YA WATU WANAMILIKI 10% sasa watazungumzia nini kuhusu hilo. Uganda hawana mfumo. Suala la ardhi ndilo limeleta kizai zai na Rwanda baada ya kugundua kuwa walishatanguliza 20,000 kabla ya mkataba kufikiwa, vipi ukifikiwa.

Unaposema ili kufaidi matunda ni kauli zinazotolewa na Wakenya nawe unazimba tu bila kuangalia facts.
Nimekuuliza kwanini wao wafike mahali pa kupigana kwa KM 1 endapo suala ni kutoa ili uvune?

Nakuomba sana urudi na kuliangalia suala hili kwa utafiti, kwa habari, kwa uchambuzi na kisayansi kuliko kusema tunawakwaza watu kwa VETO ambayo haipo to begin with unajaribu ku insinuate.

Rutashubanyuma nina wasi wasi sana kama hutumiki. I am sorry to say this but reading between the lines na unavyo sema mambo na kuacha facts ninashawishika.

Otherwise go back to the drawing board and learn more about EAC. Do not discuss the issue not well informed the least to say.

cc JokaKuu Jasusi
 
Last edited by a moderator:
Rutashubanyuma,

..kama ARDHI ni chache huku Tanzania kama unavyosema, basi serikali imefanya busara kutokuruhusu ardhi yetu kuwa ya jumuiya.

..mimi nadhani hata kwenye AJIRA tungechukua msimamo huo huo. tuna tatizo kubwa sana la ukosefu wa ajira kwa vijana wetu, kwa msingi huo tusiruhusu wageni unless ni wale wenye utaalamu wa hali ya juu unaohitajika.
Tuangalie NAFTA na jinsi Marekani inavyosakamwa kwa kulinda ajira na viwanda vyake.

Uingereza imeanza kutenga watu kutoka ulaya mashariki kwa utaratibu wa ajira kwa namna ambayo huwezi kuiona lakini ipo. Vurugu zinazotokea Spain na Italy nyingi zina chuki ya ajira.

Ujerumani wanalalamikiwa na wananchi wake kuwa inatoa sana katika EU na sawa ''Deutch Mark irudi'' n.k.
Ufaransa ubaguzi wa ajira ume base katika lugha. Yaani ni kama sisi tuseme usipojua kiswahili basi hakuna ajira.

Haya ya ajira ni kuficha ukweli, lakini la ardhi ni la wazi kabisa. Rura anasema ardhi ni suala dogo!! Ninashindwa kumwelewa kabisa. Kama ni dogo Kenya/Uganda kwanini wafikie kuzichapa kwa KM 1

Huyu bwana hafahamu kuwa suala la ardhi lilipogonga mwamba kwa mara ya kwanza wenzetu wakaja na suala la kutumia ID kuvuka mpaka ili kupata uhalali ule ule wa kile wanachokusudia.

Rutashubanyuma ameshindwa kusoma malalamiko ya Tanzania. Tanzania haisemi kwanini haijashirikishwa. Inachosema ni kuwa mambo kama hayo hufanyika under the spirit of EAC kukiwa na taarifa katika sekretariati.

Leo Dr Sezibera maeulizwa kuhusu utaratibu unaotumika ameshindwa kujibu kwasababu ni gross violation of the treaty.

Tanzania inasema kufanya mambo kwa siri ni kutengeneza mistrust. Hakuna sababu za kuwa na shirikisho nje ya shirikisho. Ima tuwe na shirikisho au basi iondolewe ili wanaotaka kwenda mbele waendelee. Hilo lina hoja kubwa sana kwasababu kufanya mikutano kinyume na spiri ya EA ni kujenga mistrust ya hali ya juu.

Asichofahamu Rutashubanyuma ni kuwa mkataba wa kijeshi ulichomekwa ili kuzuia Tanzania kushiriki katika majeshi ya SADC. Hilo lilifanyika haraka haraka tena mkataba mkubwa na sensitive kama huo ukiwa ni kifungu tu ndani ya kabrasha kubwa lililojaa hadithi za Dr Sezibera. Tanzania ilipokataa kwa kusema lazima bunge liulizwe tayari ikawa ngongwa.

Nyuma ya coalition of willing kuna mambo mengi ambayo Ruta ima kwa kujua au kutojua hataki kuyasema analeta flimsy argument za ajira. Ndio maana namwambia he is not well informed or else he wants to spin the story.....
 
..kama ARDHI ni chache huku Tanzania kama unavyosema, basi serikali imefanya busara kutokuruhusu ardhi yetu kuwa ya jumuiya.

..mimi nadhani hata kwenye AJIRA tungechukua msimamo huo huo. tuna tatizo kubwa sana la ukosefu wa ajira kwa vijana wetu, kwa msingi huo tusiruhusu wageni unless ni wale wenye utaalamu wa hali ya juu unaohitajika.

Kama tunaona tunajitosheleza basi tujitoe tubaki wenyewe kwani hakuna sababu ya kuwemo kwenye jumuiya ambayo lengo lake ni kuunganisha nchi zote ziwe moja khalafu useme mimi hiki ni changu na chenu ni changu pia.

Kadri uchumi unavyokuwa wengi wanahamia mijini na kilimo kinabakia kwa wachache. Karne ya 21 siyo ya kulima ila ni mashindano ya tekinolojia za kuboresha mawasiliano...............information age.

Kama na soko la ajira unataka lilindwe basi tukatae wawekezaji maana wanafungua milango kwa wageni kunyakau ajira zetu...................ardhi tuongeavyo inaporwa na wageni na sisi tunaishia kusukumwa.
 
Hapa unajaribu kuficha ukweli ndugu yangu.
Mkataba una masuala yanayohusu VETO. Hili jambo umeliongelea tofauti kabisa na mkataba unavyosema.

Lazima uelewe kuwa mkataba uliandikwa na nchi tatu na zilikubaliana hivyo. Maana ya VETO ililenga nchi tatu ili kuondoa kile kinachoitwa wengi kwasababu hakukuwa na wengi by then.

Pili, kuna kifungu kinachoruhusu ushirikiano wa mataifa 'variable geometry'. Sisi na Kenya tuliamua kuanza kujenga miundo mbinu ya barabara kwa kupitia EAC kama nchi mbili. Barabara ya Namanga-Nairobi

Tanzania, Rwanda na Burundi zilikuwa na mpango wa kujenga reli ya pamoja. Hayo yote yalikuwa ndani ya EAC bila kuzuiwa na nchi nyingine.

Kenya na Rwanda wana makubaliano ya ajira miongoni mwao na EAC inajua hivyo.

Tanzania imetoa msimamo kuhusu suala la ardhi na kusema kuwa wale walio tayari kufanya ardhi kuwa ya pamoja waendelee. Kwabahati mbaya hawakufanya kwasababu hilo halikuwa lengo lao.

Mkutano wa mwisho Tanzania ikasema haipo tayari kutumia ID bali passport, lakini wale wanaoweza kuendelea waendelee.

Ukiangalia mambo yote hakuna mahali ambapo Tanzania imewakwaza kama unavyodai.
Madai yako ni ya kutunga na kuyakuza na nina hofu sana kama kweli una nia njema.
Hakuna mahali ambapo Tanzania inaweza kutumia VETO kama yenyewe ina mipango niliyoeleza.

Kuhusu suala la ardhi, hilo ndilo lilianzisha mgogoro kwa taarifa yako. Hata kabla ya kujadili soko la pamoja, mitaji na uhamiaji ikiwa ni pamoja na ushuru wa forodha suala la ardhi ndilo lilikuwa la kwanza.

Kama utakumbuka Kenya ilikuwa inamtumia Kamau Warigi kuhusu suala hili wakisema Tanzania inakwamisha EAC kwa masuala ya ardhi.

Sababu wanazozitoa wao ni kuhusu ajira ambazo si kweli.
Watanzania wengi wanafanya kazi katika nchi za EAC.

Wenzetu wanasema watu waje na ID zao na kupewa ajira. Sasa kama Tanzania ilikataa ID kwanini ikubali ID za ajira. Na pili hakuna anayenyimwa ajira kwa kuomba.

Sababu wanzozitoa wao ambazo unaamini ni hafifu kuliko suala la ardhi. S
uala la ardhi hawawezi kuliongelea kwasababu nyingi.

Angalia population density ya Rwanda na Burundi halafu uniambie.
Kenya 10% ya watu inamiliki 90% ya ardhi. 90% YA WATU WANAMILIKI 10% sasa watazungumzia nini kuhusu hilo. Uganda hawana mfumo. Suala la ardhi ndilo limeleta kizai zai na Rwanda baada ya kugundua kuwa walishatanguliza 20,000 kabla ya mkataba kufikiwa, vipi ukifikiwa.

Unaposema ili kufaidi matunda ni kauli zinazotolewa na Wakenya nawe unazimba tu bila kuangalia facts.
Nimekuuliza kwanini wao wafike mahali pa kupigana kwa KM 1 endapo suala ni kutoa ili uvune?

Nakuomba sana urudi na kuliangalia suala hili kwa utafiti, kwa habari, kwa uchambuzi na kisayansi kuliko kusema tunawakwaza watu kwa VETO ambayo haipo to begin with unajaribu ku insinuate.

Rutashubanyuma nina wasi wasi sana kama hutumiki. I am sorry to say this but reading between the lines na unavyo sema mambo na kuacha facts ninashawishika.

Otherwise go back to the drawing board and learn more about EAC. Do not discuss the issue not well informed the least to say.

Tatizo ni kuwa unadai unaelewa lakini naona hufahamu vyema kama haya unaytoyasema ni kweli kwanini tunalalamikia wenzetu kuendelea na hatua mbele kwa mbele za integration na kufikia Membe kudai tunasubiri "talaka"?

Waziri wa Afrika mashariki Sitta amekiri kuwa sasa tunatengwa ingawaje fedha za bajeti ya EAC ndizo zinazotumika. Sitta kasema kwa mdomo wake wanasubiri vikao vya EAC kupata ufafanuzi wa zaidi.

Pitia tena EAC treat utagundua nchi moja ikikataa kitu basi hakifanyiki. Kwa mfano kama kujiunga kwa Rwanda na Burundi tungelikataa basi wasingelijiunga.
Na ndiyo maana ninachoshauri mkataba wa EAC uondoe kifungu cha veto ya mshiriki mmoja pale asipokubaliana na lolote lile. Mimi sipendi kuzungumzia masuala ya ardhi na ajira kwa sababu sisi ni wanafiki sana. Hatuna nia ya kumpatia raia wetu ajira wala ardhi na nia ingelikuwepo hii bomoaboma ya "mpishe mwekezaji" isingelikuwepo.

tatizo letu tunapenda ionakane kila kitu ni shwari na ukihoji mapungufu wewe unapakazwa hujui na mpotoshaji. Kama kila kitu ni shwari.............why are we so poor?
 
Tanzania imetoa msimamo kuhusu suala la ardhi na kusema kuwa wale walio tayari kufanya ardhi kuwa ya pamoja waendelee. Kwabahati mbaya hawakufanya kwasababu hilo halikuwa lengo lao.
Wenzetu wanasema watu waje na ID zao na kupewa ajira. Sasa kama Tanzania ilikataa ID kwanini ikubali ID za ajira. Na pili hakuna anayenyimwa ajira kwa kuomba.

kama nilikosea kujiita sisi ni "Dr. No"..................mbona hapa unakubali kuwa sisi ni "Dr. No"?

Unabisha khalafu unathibitisha..........which side are you? Of the truth or the lies of our government?

Labda niambie matarajio yetu ndani ya EAC kama siyo shirikisho na kuwa na serikali moja ni nini?
 
Kwa maoni yangu binafsi watanzania hawakujiandaa na globalization. Hawana mfumo mzuri wa elimu kwa soko la kazi la kimataifa. Hivyo wanaogopa ushindani. Hawakuwa na sheria nzuri za haki ya kumiliki ardhi. Hivyo NO nyingi ni za kujilinda hili wasije kujiona wanyonge ndani ya nchi yao wenyewe.

Hongera Zakumi kwa kuukubali ukweli badala ya baadhi ya wachangiaji ambao waunda simulizi kuwa hatukatai wenzaetu wasisonge mbele kama sisi tunakwazwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Ruta Nadhani umemsoma vema jokaKuu. Jiulize katika mambo yote wenzetu wadhani msingi wa EA ni ardhi. Endapo ni msingi tujiulize je kutakuwa na fair deal? Angalia population density Nguruvi3 anachosema JokaKuu ni kuwa anatambua yapo matatizo kila mahali lakini tofauti na wewe hutaki kukiri sisi tuna matatizo pia tena siyo ardhi ila katika maeneo mengi kama haya:- 1) Ardhi 2) Ajira 3) Kodi 4) Non-tarif barriers 5) Shirikisho la kisiasa 6) Mahakama 7) Sarafa Moja 8) Matumizi ya ID 9) Ulinzi na Usalama 10) N.k
 
Kama tunaona tunajitosheleza basi tujitoe tubaki wenyewe kwani hakuna sababu ya kuwemo kwenye jumuiya ambayo lengo lake ni kuunganisha nchi zote ziwe moja khalafu useme mimi hiki ni changu na chenu ni changu pia.

Kadri uchumi unavyokuwa wengi wanahamia mijini na kilimo kinabakia kwa wachache. Karne ya 21 siyo ya kulima ila ni mashindano ya tekinolojia za kuboresha mawasiliano...............information age.

Kama na soko la ajira unataka lilindwe basi tukatae wawekezaji maana wanafungua milango kwa wageni kunyakau ajira zetu...................ardhi tuongeavyo inaporwa na wageni na sisi tunaishia kusukumwa.
Rutashubanyuma,

..umesema ardhi ni chache huku Tanzania na hicho ndicho chanzo cha migogoro isiyokwisha.

..sasa ukishasema hayo basi ni lazima ukubaliane na uamuzi wa serikali kukataa kwamba ardhi isiwe ya jumuiya.

..hakuna mahali ambapo wa-Tanzania wamedai wamilikishwe ardhi ya majirani zetu. majirani zetu hawana ardhi ya kutoa kwa wa-Tanzania. kwa msingi huo sioni sababu ya wewe kusema wa-Tanzania tuna tabia ya "chetu chetu, chenu chetu."

..kuhusu ardhi vs industries: ikiwa industrialization itaongezeka basi wananchi wengi zaidi wataondoka kwenye kilimo. tatizo ni kwamba industrial sector in our region haikuwi kwa kasi ya kutosha kuweza kuwa ndiyo mwajiri mkubwa wa wananchi.

..labda ktk hili tuwaase majirani zetu kwamba solution ya matatizo yao ya ardhi siyo kuendelea kulilia ardhi ya Tanzania, bali ni wao kuchukua hatua zitakazowawezesha ku-industrialize kwa kasi kubwa zaidi ili kupunguza demand ya ardhi kwa ajili ya kilimo.

..mwisho, kodi na ajira ni moja ya faida za uwekezaji ambazo nchi husika inapaswa kuzipata. kama mwekezaji hawezi kutoa ajira kwa wa-Tanzania basi mimi namuona hana faida kwetu. kama mwekezaji hawezi kulipa kodi ni bora akaondoshwa.

..Marekani wana un-employment rates lower than Tanzania, lakini kila siku wanaweka sheria za kulinda ajira za wananchi wao. Wamarekani wanafanya hivyo wakielewa kabisa kwamba waajiriwa wazawa ni aghali kuliko immigrants. Sielewi kwanini inaonekana ni kosa kwa Tanzania kudai kwamba ktk shughuli za uwekezaji toka nje wananchi wetu wapewe kipaumbele ktk ajira.

NB:

..Canada,Marekani, na Mexico, wana ushirikiano wa kibiashara unaitwa NAFTA. Pamoja na kuwepo ushirikiano huo Marekani amejenga UKUTA ktk mpaka wake na Mexico. Kwa msingi huo utaona kwamba tunaweza kushirikiana na majirani zetu wakati huohuo tukihifadhi ardhi yetu, na kulinda ajira za wazawa.

..kuna njia mbili za kulinda ajira za wazawa. mosi, ni kuhakikisha wa-Tz has the best trained labor force in the region. pili, tuzilinda ajira hizo kwa restrictions za kisheria. kwa maoni yangu we need to do both.

cc Mchambuzi, Ngongo, Tuko
 
Last edited by a moderator:
Rutashubanyuma,

..umesema ardhi ni chache huku Tanzania na hicho ndicho chanzo cha migogoro isiyokwisha.

..sasa ukishasema hayo basi ni lazima ukubaliane na uamuzi wa serikali kukataa kwamba ardhi isiwe ya jumuiya.

..hakuna mahali ambapo wa-Tanzania wamedai wamilikishwe ardhi ya majirani zetu. majirani zetu hawana ardhi ya kutoa kwa wa-Tanzania. kwa msingi huo sioni sababu ya wewe kusema wa-Tanzania tuna tabia ya "chetu chetu, chenu chetu."

..kuhusu ardhi vs industries: ikiwa industrialization itaongezeka basi wananchi wengi zaidi wataondoka kwenye kilimo. tatizo ni kwamba industrial sector in our region haikuwi kwa kasi ya kutosha kuweza kuwa ndiyo mwajiri mkubwa wa wananchi.

..labda ktk hili tuwaase majirani zetu kwamba solution ya matatizo yao ya ardhi siyo kuendelea kulilia ardhi ya Tanzania, bali ni wao kuchukua hatua zitakazowawezesha ku-industrialize kwa kasi kubwa zaidi ili kupunguza demand ya ardhi kwa ajili ya kilimo.

..mwisho, kodi na ajira ni moja ya faida za uwekezaji ambazo nchi husika inapaswa kuzipata. kama mwekezaji hawezi kutoa ajira kwa wa-Tanzania basi mimi namuona hana faida kwetu. kama mwekezaji hawezi kulipa kodi ni bora akaondoshwa.

..Marekani wana un-employment rates lower than Tanzania, lakini kila siku wanaweka sheria za kulinda ajira za wananchi wao. Wamarekani wanafanya hivyo wakielewa kabisa kwamba waajiriwa wazawa ni aghali kuliko immigrants. Sielewi kwanini inaonekana ni kosa kwa Tanzania kudai kwamba ktk shughuli za uwekezaji toka nje wananchi wetu wapewe kipaumbele ktk ajira.

NB:

..Canada,Marekani, na Mexico, wana ushirikiano wa kibiashara unaitwa NAFTA. Pamoja na kuwepo ushirikiano huo Marekani amejenga UKUTA ktk mpaka wake na Mexico. Kwa msingi huo utaona kwamba tunaweza kushirikiana na majirani zetu wakati huohuo tukihifadhi ardhi yetu, na kulinda ajira za wazawa.

..kuna njia mbili za kulinda ajira za wazawa. mosi, ni kuhakikisha wa-Tz has the best trained labor force in the region. pili, tuzilinda ajira hizo kwa restrictions za kisheria. kwa maoni yangu we need to do both.

cc Mchambuzi, Ngongo, Tuko

Mkuu mimi kuna kitu ambacho nimehoji sana huku but sijapata jibu. Ni katika kipengele kipi cha majadiliano ya EAC ambapo wamesema ardhi iwe ya wote. Najua kila nchi ardhi yake inalindwa na katiba na sheria zake. Viongozi wetu wanapojitoa katika mchakato watupe taarifa sahihi but nadhani hili la ardhi wanaliongea tu kutafuta mass support. Kwa sasa wapo katika stage ya ushuru wa forodha. Ardhi inaingiaje hapa?...
 
Last edited by a moderator:
Rutashubanyuma,

..kama ARDHI ni chache huku Tanzania kama unavyosema, basi serikali imefanya busara kutokuruhusu ardhi yetu kuwa ya jumuiya.

..mimi nadhani hata kwenye AJIRA tungechukua msimamo huo huo. tuna tatizo kubwa sana la ukosefu wa ajira kwa vijana wetu, kwa msingi huo tusiruhusu wageni unless ni wale wenye utaalamu wa hali ya juu unaohitajika.

I second you on this!
Lazima tujilinde usalama wetu kiuchumi ndani kabla ya kufungua milango
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: TGN
Mkuu mimi kuna kitu ambacho nimehoji sana huku but sijapata jibu. Ni katika kipengele kipi cha majadiliano ya EAC ambapo wamesema ardhi iwe ya wote. Najua kila nchi ardhi yake inalindwa na katiba na sheria zake. Viongozi wetu wanapojitoa katika mchakato watupe taarifa sahihi but nadhani hili la ardhi wanaliongea tu kutafuta mass support. Kwa sasa wapo katika stage ya ushuru wa forodha. Ardhi inaingiaje hapa?...
Tuko,

..masuala ya ardhi yaliibuka wakati wa majadiliano ya Common Market Protocoal.

..hili suala linaumiza baadhi ya wanachama wa EAC ambao malengo yao kujiunga na jumuiya yalikuwa ni ardhi.

..nime-quote makala ya mtafiti Nyambura Githaiga ili kukupa mwanga zaidi.

This July marks a year since the ratification of the EAC Common Market Protocol. Despite the apparent integration synergies, there was resistance to concede to the aspect of right of establishment, as contained in the draft protocol for the Common Market, due to its implications for LAND use, access and ownership. The final concession acknowledged the national policies and laws of member states as the governing frameworks for land use and access. Land has long been a source of conflict among the EAC member states and in that context it is hardly surprising that integration would add a regional dimension to existing land conflicts. On a regional level, while the majority of the EAC countries, namely Burundi, Kenya, Rwanda and Uganda, uphold a more private land ownership system, Tanzania has a more public land tenure system. So, while some member states would be open to foreign ownership of land within the EAC, other states would prefer to restrict land ownership to citizens with respect to existing land regimes.

source:ISS Africa | Much Ado About Land in the EAC

cc Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
Tuko,

..masuala ya ardhi yaliibuka wakati wa majadiliano ya Common Market Protocoal.

..hili suala linaumiza baadhi ya wanachama wa EAC ambao malengo yao kujiunga na jumuiya yalikuwa ni ardhi.

..nime-quote makala ya mtafiti Nyambura Githaiga ili kukupa mwanga zaidi.



source:ISS Africa | Much Ado About Land in the EAC

cc Nguruvi3

Sasa mkuu kwa hizi sentensi mbili kutoka kwenye hiyo quote ya Githaiga;
"The final concession acknowledged the national policies and laws of member states as the governing frameworks for land use and access".
"So, while some member states would be open to foreign ownership of land within the EAC, other states would prefer to restrict land ownership to citizens with respect to existing land regimes"


Mgogoro uko wapi sasa!!! Kama tulishafikia "final concession" kuwa sheria na taratibu za nchi husika ndizo zitatumika katika masuala ya ardhi, hatuoni kwamba tunapambana na "a dead devil"?... Baada ya hiyo common market protocol kuwa ratified mwaka 2010 (kwa mujibu wa hiyo quote), nategemea majadiliano ya ardhi yalifungwa.
Swali: Ni nini kimekuja kutokea baadae hadi mwaka 2013 wenzetu wakaanza kusonga mbele na kutuacha sisi tudaduwaa na kudai talaka?...
 
Back
Top Bottom