Kwanini Ndege inaelea angani?

Socratic

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2014
Posts
568
Reaction score
308
Aulizaye anataka kujua, hebu saidia huyu mtoto anauliza, ''Baba...baba..Kwanini ndege inaelea angani''?.

Mwenye kujua jibu asaidie hapa.
 
Unamjibu:~ Mwanangu ndege hiyo imeundwa kuwa na mabawa na mtambo wenye nguvu na kasi ya kuirusha anagani !!
Ndege iyo .......................... imeigwa kwa ndege mnyama huyu!! ....
 
Swali la kitaalam jibu lake huwa ni la kitaalam kama unataka jibu rahisi basi mjibu ni uwezo wa Mungu muumbaji wa vyote, vinavyoelea, vinavyotambaa na vinavyopaa.

Duh hiyo ngumu zaidi kueleweka
 
Na akikuuliza hivi utamjibuje? baba.. na mimi nikiwekewa mabawa na mtambo wenye nguvu na kasi naweza kuruka hadi marekani?
Of Cozi mwananngu wewe utakuwa bingwa !! Tutakufungia mitambo miwili mgongoni yennye kupuliza hewa na kukurusha juu na kupaa hadi utakapo!! Sasa ona mfano wake.............
tulianazaga mwaka 1961 siku ya huru hivi... Tukaendelea kuboresha hadi leo tupo hivi.. .... sawa mwanangu sasa jitahidi ukasome upate kupaa!!
 
Kasome Bernoulli's Principle of Aerodynamics, Newton's third law of motion in relation to rocket /jet propulsions na combustion.

Baada ya hapo naamini utaelewa kwanini ndege inapaa
 
Swali la kitaalam jibu lake huwa ni la kitaalam kama unataka jibu rahisi basi mjibu ni uwezo wa Mungu muumbaji wa vyote, vinavyoelea, vinavyotambaa na vinavyopaa.

Khaaa!! ha ha haa..
 
cha kutambua ni kuwa miracle does not exist only your ignorance is miracle.

ndege inavyoruka ni jambo rahisi sana ni kitu kinaitwa "up lift force"

hebu angalia tiara kama unaijua imetenngenezwa kwa mkunjo fulani sasa unapoivuta kwenda mbele kwa kasi ile hewa mahali tiara inakopita inakuwa ni kama upepo unapita kurudi nyuma. sasa ule msuguano kati ya tiara na upepo kutokana na ule mgongo uliojikunja kama kuinuka juu kuna nguvu inatokea ya kuelekea juu na hiyo ndiyo inainua tiara.

ndege hivyo hivyo mabawa yake yametengengezwa kwa mgongo kama wa tiara hivyo injini zinaposukuma ndege kwenda mbele kwa kasi ule mgongo wa kwenye mabawa kutokana na msuguano na hewa unatengeneza uplift force.

hivyo ndege ina injini ambazo zinaisukuma kwa mbele na ile kasi inatengeneza nguvu ya mwinuko katika mabawa.

Aulizaye anataka kujua, hebu saidia huyu mtoto anauliza ....Baba...baba..kwanini ndege inaelea angani? Mwenye kujua jibu asaidie hapa.
 
Labda iwe ni kutokana na Anti - gravitational force, jamani science hapa mi simo. Nimejaribu tu kufikilia jibu la haraka kimtindo, kwamba gravitational force - unaporusha kitu juu kinaenda zen kinarudi chini, y? koz of gravitational force.

Nahisi ndege kuna Anti gravitational force ili kuifanya ndege isirudi chini, na hiyo force ya ziada siijui...., nimetumia tu hilo neno ili kuwasilsha wazo langu. ila cha msingi elewa ili kitu kipae lazima kuwe na force itakayopinga ukinzani - gravitational force. Maelezo zaidi kamuona mwl wa Physics

NB: Sayansi niliacha tangu 4m 2, coz nilikua siwezi chemistry, ila physics nilikua nooma na hesabu. hivyo tusitupiane mawe kama nimekosea toa jibu lako, wengine hapa wanajifunza
 
Majibu ya hili swali yapo..... Fuatilia post humu....
 
Kasome Bernoulli's Principle of Aerodynamics, Newton's third law of motion in relation to rocket /jet propulsions na combustion.

Baada ya hapo naamini utaelewa kwanini ndege inapaa

Duh kweli haya ndio ya kumwambia mtoto?
 

Unadhani mtoto atakuelewa kweli?
 
Duh kweli haya ndio ya kumwambia mtoto?

Hapa hakuna cha mtoto bana watu wanajifunza mi mwenyewe nitakitafuta nikasome, hivi vitu muhimu kuvijua hata kwa idea vinaweza kukutoa siku moja kimaisha kwa jibu swali tu
 
Kasome Bernoulli's Principle of Aerodynamics, Newton's third law of motion in relation to rocket /jet propulsions na combustion.

Baada ya hapo naamini utaelewa kwanini ndege inapaa

Asante mkuu kwa faida yangu pia niliipenda sana physics, bt chemistry ilinitupa mbali test ya kwanza 4m 1 nilipata 5/100
 
Asante mkuu kwa faida yangu pia niliipenda sana physics, bt chemistry ilinitupa mbali test ya kwanza 4m 1 nilipata 5/100

Mkuu tuna tatizo moja, niliipenda sana Physics, bado naipenda na ntaendelea kuipenda, ila Chemistry nilifaulu form four kwa sababu tu ya kua na mwalimu mzuri.

Tatizo kwenye hili swali kama ni mtoto kauliza jibu lake inabidi lisiwe la kitaalam lakini liwe la kueleweka kwa uwezo wake na kiwango cha ufaham wake.
 
hapa wewe unayeuliza unaelewa uplift force ni kitu gani sasa kazi kwako kama unaielewa itafsiri katika michezo yake na kilugha chenu umueleze kama ukishindwa basi ujue wewe ndo hujaelewa sio mtoto.

Unadhani mtoto atakuelewa kweli?
 
hapa wewe unayeuliza unaelewa uplift force ni kitu gani sasa kazi kwako kama unaielewa itafsiri katika michezo yake na kilugha chenu umueleze kama ukishindwa basi ujue wewe ndo hujaelewa sio mtoto.

Uplift force ni nini ndugu yangu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…