Kwanini nitumie dawa za kuzuia mafua?

Kwanini nitumie dawa za kuzuia mafua?

safuher

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2019
Posts
11,837
Reaction score
17,412
Mwili kikawaida huwa una njianzake pekee za kujilinda dhidi ya vitu mbalimbali(defense mechamism).

Mtu akipaliwa na punje ya wali atakohoa na hakuna anayezuia kwamba usikohoe kwa sababu kukohoa ni njianya mwili kujilinda na baada ya hapo mtu anapata afadhali.

Sasa kwenye mafua, yale mafua ni body fluid ambayo miongoni mwa kazi zake ni kuondoa uchafu kwa kutumia njia ya kujizalisha kwa wingi fluid hiyo na hatimae kuanza kuvuja nje.

Kama hali iko hivyo kwamba mafua yanayotoka kwa mtu ni njia moja wapo ya kusafisha mwil i basi maana yake ni kwamba kuyazuia mafua hayo ni kusema kwamba hautaki uchafu huo utoke ndani ya mwili.

Hiyo ina maana ya kwamba unapotumia dawa ya kuzuia mafua maana yake unatumia dawa ya kuzuia uchafu usitolewe ndani ya mwili.

Je, hii haiwezi kutufanya tuwaze kwamba matumizi ya dawa za kuzuia mafua kwa muda mrefu inaweza kusababisha matatizo makubwa kama kushusha kinga ya mwili?

Maana unapozuia mafua maana yake unazuia ulinzi wa mwili,unapouzuia kwa muda mrefu hatimae utaudhoofisha mfumo wa kinga,na hatimae sasa kifua kitavamiwa kwa kasi hapo baadae na kusababisha COPD
yaani matatizo ya kifua sugu?
 
Mafua husababisha kichwa kuuma, pua(nasal cavity) kuuma na kuwasha, kukosa hamu ya kula, koo kuwasha, kwa nini uvumilie hali hiyo wakati dawa zipo kuponya ugonjwa huo?
 
We jamaa mafua noma sana mimi nikiumwa mafua napata hadi homa halafu umasema nisitumie dawa we jamaa bure kabisa
 
  • Kicheko
Reactions: EEX
Mafua husababisha kichwa kuuma, pua(nasal cavity) kuuma na kuwasha, kukosa hamu ya kula, koo kuwasha, kwa nini uvumilie hali hiyo wakati dawa zipo kuponya ugonjwa huo?
Kama kweli kazi ya mafua ni kuondoa uchafu,je kuna haja ya kuyazuia mafua wakati kuyaacha kwake yanatusaidia kuondoa uchafu ?

Thread yangu imekuja kwa mfumo wa swali..
 
We jamaa mafua noma sana mimi nikiumwa mafua napata hadi homa halafu umasema nisitumie dawa we jamaa bure kabisa
Thread yangu ni swali.

Kama mafua hutusaidia kuondoa uchafu,je kwa nini tutumie dawa za kuzuia mafua hayo ?
 
Mwili kikawaida huwa una njianzake pekee za kujilinda dhidi ya vitu mbalimbali(defense mechamism).

Mtu akipaliwa na punje ya wali atakohoa na hakuna anayezuia kwamba usikohoe kwa sababu kukohoa ni njianya mwili kujilinda na baada ya hapo mtu anapata afadhali.

Sasa kwenye mafua, yale mafua ni body fluid ambayo miongoni mwa kazi zake ni kuondoa uchafu kwa kutumia njia ya kujizalisha kwa wingi fluid hiyo na hatimae kuanza kuvuja nje.

Kama hali iko hivyo kwamba mafua yanayotoka kwa mtu ni njia moja wapo ya kusafisha mwil i basi maana yake ni kwamba kuyazuia mafua hayo ni kusema kwamba hautaki uchafu huo utoke ndani ya mwili.

Hiyo ina maana ya kwamba unapotumia dawa ya kuzuia mafua maana yake unatumia dawa ya kuzuia uchafu usitolewe ndani ya mwili.

Je, hii haiwezi kutufanya tuwaze kwamba matumizi ya dawa za kuzuia mafua kwa muda mrefu inaweza kusababisha matatizo makubwa kama kushusha kinga ya mwili?

Maana unapozuia mafua maana yake unazuia ulinzi wa mwili,unapouzuia kwa muda mrefu hatimae utaudhoofisha mfumo wa kinga,na hatimae sasa kifua kitavamiwa kwa kasi hapo baadae na kusababisha COPD
yaani matatizo ya kifua sugu?

Mafua hutokea panapokuwa na maambukizi (hasa ya virusi) kwenye njia za juu za mfumo wa hewa (pua, koo na masikio) au uchafu/vumbi kuingia kwenye njia za juu za mfumo wa hewa (pua, koo na masikio).

Mafua huwa na dalili mbalimbali mfano kukohoa, kuwasha pua/masikio/koo, homa, kichwa kuuma nk.

Dalili hizo hutokea pale mwili unapopambana kuondosha kile kitu kilichoingia kwenye njia ya hewa kwa kukohoa pamoja na kuzalisha kemikali mbalimbali mfano histamines ambazo huchangia baadhi ya dalili hapo juu.

Mtu anapotumia au anapopewa dawa akiwa na mafua lengo ni kupunguza makali ya hizo dalili na kuusaidia mwili kuondosha visababishi vya mafua mfano uchafu/vumbi kupitia makohozi.

Kwa hiyo hakuna dawa za kuzuia au kutibu mafua bali dawa zinazotolewa ni za kupunguza tu makali ya dalili ambazo mtu hupata anapokuwa na mafua. Mara nyingi kinga mwili hupambana na kumaliza mafua yenyewe.

Pia dawa hizo zinazotolewa ni kwa ajili ya kupunguza makali ya dalili na si kushusha kinga ya mwili.

Kila la kheri.
 
Hapa nilipo tangu jumapili nina mafua, kichwa kinauma, pua, koo na masikio yanawasha, macho yanauma, nimekosa hamu ya kula, mwili kuuma, nakohoa na kupiga chafya, homa juu ikabidi niende duka la dawa nipate dawa ya mafua. Leo naendelea vizuri najisikia kupona baada ya kunywa dawa
 
Uchafu unatoka kwa njia nyingi hivyo mafua ni ya kuyadhibiti mapema la sivyo homa kali itakupeleka hospital kulazwa
 
K
Hapa nilipo tangu jumapili nina mafua, kichwa kinauma, pua, koo na masikio yanawasha, macho yanauma, nimekosa hamu ya kula, mwili kuuma, nakohoa na kupiga chafya, homa juu ikabidi niende duka la dawa nipate dawa ya mafua. Leo naendelea vizuri najisikia kupona baada ya kunywa dawa
kitunguu maji ndio suluhisho kata kachumbari
 
Zaman mafua na kikohozi nilikuwa situmii dawa ila sahv kikohozi nakiheshimu hasa nikikipata tu lazima nikimbilie dawa ya maji

Kiliwah nifanya nisilale kwa wiki nzima,yaan ikifika usiku nakohoa mpaka asubuh
 
Back
Top Bottom